The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,951
- 12,541
CCM ndiyo inaongoza serikali kwa sasa. Kwa sasa haijalishi sana kujadili namna walivyopata mamlaka ya kiutawala aidha ni kwa uhalali au kwa uharamia.
Lakini muhimu ni hili, kuwa, wanadhani kuwa madai ya katiba mpya ya wananchi ni ili wao wanyang'anywe mamlaka na madaraka yao ya utawala wa kiserikali ya nchi hii leo au kesho tu ambayo wamedumu nayo tangu uhuru wa Tanganyika Desemba 9, 1961..
Hii ni dhana iliyojengwa juu ya fikra potofu na hatari sana zinazokwenda kuleta maumivu kwa kila mmoja wetu iwe kwa wao watawala au sisi wananchi yaani watawaliwa.
Na dhana hii potofu ndiyo inayosababisha physical confrontation inayoendelea sasa kati ya wananchi wanaodai mabadiliko ya kikatiba na wenye mamlaka ya kiserikali (CCM) wanaodhani na kujiona wako hatarini kufurushwa kwenye viti vyao vya kiutawala wanavyotumia "kula". Na sasa wanajaribu kutumia kila njia mbaya kuzima sauti hizi za kudai mabadiliko. Habari mbaya kwao ni kuwa, kwa vyovyote vile hawatazima moto wa sauti za madai haya...!
Kwanini watu wanadai mabadiliko mapya ya kikatiba (new constitutional reforms) Tanzania?
1. KWANZA, tunataka mabadiliko ya kikatiba lengo kuu (core objective) likiwa siyo kuiondoa CCM madarakani. Lakini inawezekana uwepo wa katiba mpya ikawa ni accelerating factors ya kuifurusha CCM madarakani. Ikiwa vile, so what? Maana itakuwa ni majibu kuwa kumbe walikuwa pale kimakosa na kwa njia haramu...!!
Lakini pia, ni vyema na haki kuelewa kuwa, katiba ya nchi ni instrument kubwa sana iliyo juu ya kila mtu, kila taasisi na kila chama cha siasa...
KATIBA YA NCHI ni determinant factor ya existence ya kila mtu, kila taasisi, kila chama cha siasa, uzuri au ubovu wa huduma za za jamii, uimara ama ulegevu wa uchumi wa nchi, uwepo serikali mbaya au nzuri ya nchi, shughuli zote za kiuchumi nk nk katika nchi...
2. PILI, kwa uchache sana tunataka KATIBA MPYA YA WANANCHI kwa sababu katiba ndiyo inayotoa mwongozo (guidance) wa;
å Mwelekeo bora wa nchi kiuongozi na kiutawala
å Namna ya kupata viongozi wa serikali kwa njia sahihi, za wazi na za haki..
å Kudhibiti mamlaka na madaraka ya viongozi wa serikali waliopewa dhamana hizo...
å Utekelezaji na utoaji wa haki na hukumu kwa kila mtu kwa njia ya wazi, huru na haki..
å Mgawanyo sahihi wa majukumu ya kiutawala, uongozi na usimamizi wa shughuli za serikali...
3. Tunataka KATIBA mpya ya wananchi ili kwa pamoja kama wananchi wa nchi hii tujenge nchi yenye taasisi na mifumo imara ya kiutawala (unshakeable government administrayive institutions) isiyoyumba wala kutikisika bila kujali ni mtawala mkuu wa aina gani anatawala nchi, mwehu au kichaa; mwerevu au mjinga...
4. Tunataka Katiba mpya ili kuleta USAWA na HAKI kwa kila mwananchi wa nchi hii kushiriki kikamilifu na kwa UHURU kwenye shughuli za kiutawala wa nchi yake...
Labda mtu anaweza kujiuliza maswali haya. Na kiukweli ndiyo utetezi wa wafuasi wa CCM kupinga madai ya katiba mpya:
å Kwamba, Je, kwani kwa katiba hii iliyopo ya 1977 haiwawezeshi wananchi kushiriki kwenye shughuli za kiutawala wa nchi yao? Mbona huwa tunafanya uchaguzi mkuu kila baada ya miaka 5 tunachagua Rais, wabunge na madiwani na wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji? Je, hiyo siyo demokrasia, Uhuru na haki kwa wananchi?
å Au, je, kwani katiba ya 1977 haiwapi wananchi UHURU na HAKI ya kufanya shughuli zao za kila siku za kijamii, kiuchumi, na kisiasa?
Majibu ya maswali hayo yote ni mawili tu, ambayo ni:
Kwamba, katiba ya mwaka 1977 tunayotumia sasa ina kasoro kubwa mbili na hivyo kuifanya ikose uhalali wa kisiasa (political legitimacy) kuwa mwongozo HURU na wa HAKI kutumika ktk nchi hii...
Na hii ndiyo imeleleta matatizo yote haya tuliyayo leo kwa kiasi kikubwa yaani uwepo wa mifumo mibaya na dhaifu ya kiutawala, ya kiuchumi, na kiuongozi katika taasisi kuanzia ile ya juu ya Urais hadi huku chini..
Kwa kifupi, kasoro za katiba ya mwaka 1977 ambayo ndiyo inatumika sasa ni:
[A.] MOSI, si makubaliano ya WANANCHI WOTE kwa ujumla wao. Haikuandikwa na wananchi bali iliandikwa na watawala wachache...
Msingi wa katiba hii ya 1977 ni wa kikoloni iliyokuwa inalenga kulinda maslahi ya utawala wakoloni dhidi ya wenye nchi. Nasi baada yq uhuru tumerithi mfumo huohuo wa kikatiba huku watawala (CCM) wakichukua nafasi ya wakoloni na hivyo kujiwekea ulinzi wa kikatiba. Na ndiyo chanzo cha msemo huu, "CCM ni wakoloni weusi..". Maana yake ni hii..
Kumbukumbu za kihistoria zinasema iliandikwa na watu wasiozidi 22 tu waliojifungia sehemu chini ya Mwasisi wa taifa hili Mwl. Julius K. Nyerere..
[B.] PILI, katiba hii ya mwaka 1977 kuanzia mwanzo A to Z imerundika mamlaka ya kiutawala kwa mtu mmoja mwenye cheo na madaraka makubwa kupita kiasi ya kimaamuzi anayeitwa Rais...
Kwa mujibu wa katiba hii ya sasa ya 1977, Rais ndiye kila kitu. Ndiye anayeamua hata huko kijijini kwenu muishi vipi, mpate maendeleo gani na muwe na kiongozi gani...
HITIMISHO
1. Ndiyo maana kuna harakati za madai ya mfumo mpya wa kiutawala wa nchi hii kupitia madai ya katiba mpya ya wanachi..
2. Ndiyo maana kuna msuguano huu unaoendelea kati ya WATAWALA wanatetea mfumo unaowanufaisha na WATAWALIWA (wananchi) waliokwisha kugundua tatizo la mkwamo wa nchi yao.
3. Madai ya katiba hayana lengo la kuiondoa CCM madarakani japo yaweza kuleta matokeo hayo...
Lengo na kudai Katiba mpya ya wananchi ni kuwatengenezea mwongozo mzuri na wa haki ili waweze kutawala na kuhukumu kwa haki ktk nchi hii...
4. Kwa katiba hii tunayotaka kuiandika SISI WANANCHI WA TANZANIA itamweka yeyote kutawala nchi hii. Kama CCM watajinadi na wananchi kuwaelewa na wakawapa ridhaa ya kuongoza nchi hii tena na tena na tena, so be it so long as watayapata mamlaka ya uongozi huo wa nchi hii kwa njia za WAZI na HAKI...
THIS IS WHAT WE WANT. Sasa kwa nini tupigane? Kwa nini tunataka kuanza kuuana? Kwa nini tuanze kumbakiziana kesi za ugaidi?
AMA KUMBE NI KWELI:
"...mwanamke mjinga, huivunja Nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe...!!"
MWANAMKE MJINGA HAPO: ni CCM na serikali yao chini ya Rais Mama Samia Suluhu Hassan na NYUMBA HAPA ni Tanzania nchi yetu mzuri...
Sasa huyu wanamke mjinga anataka kuisambaratisha nyumba yake mwenyewe...!!
WATOTO TUKATAENI HILI, TUMPINGE HUYU MAMA "MJINGA" ATAKAYE KUIVUNJA NYUMBA YETU...!
Lakini muhimu ni hili, kuwa, wanadhani kuwa madai ya katiba mpya ya wananchi ni ili wao wanyang'anywe mamlaka na madaraka yao ya utawala wa kiserikali ya nchi hii leo au kesho tu ambayo wamedumu nayo tangu uhuru wa Tanganyika Desemba 9, 1961..
Hii ni dhana iliyojengwa juu ya fikra potofu na hatari sana zinazokwenda kuleta maumivu kwa kila mmoja wetu iwe kwa wao watawala au sisi wananchi yaani watawaliwa.
Na dhana hii potofu ndiyo inayosababisha physical confrontation inayoendelea sasa kati ya wananchi wanaodai mabadiliko ya kikatiba na wenye mamlaka ya kiserikali (CCM) wanaodhani na kujiona wako hatarini kufurushwa kwenye viti vyao vya kiutawala wanavyotumia "kula". Na sasa wanajaribu kutumia kila njia mbaya kuzima sauti hizi za kudai mabadiliko. Habari mbaya kwao ni kuwa, kwa vyovyote vile hawatazima moto wa sauti za madai haya...!
Kwanini watu wanadai mabadiliko mapya ya kikatiba (new constitutional reforms) Tanzania?
1. KWANZA, tunataka mabadiliko ya kikatiba lengo kuu (core objective) likiwa siyo kuiondoa CCM madarakani. Lakini inawezekana uwepo wa katiba mpya ikawa ni accelerating factors ya kuifurusha CCM madarakani. Ikiwa vile, so what? Maana itakuwa ni majibu kuwa kumbe walikuwa pale kimakosa na kwa njia haramu...!!
Lakini pia, ni vyema na haki kuelewa kuwa, katiba ya nchi ni instrument kubwa sana iliyo juu ya kila mtu, kila taasisi na kila chama cha siasa...
KATIBA YA NCHI ni determinant factor ya existence ya kila mtu, kila taasisi, kila chama cha siasa, uzuri au ubovu wa huduma za za jamii, uimara ama ulegevu wa uchumi wa nchi, uwepo serikali mbaya au nzuri ya nchi, shughuli zote za kiuchumi nk nk katika nchi...
2. PILI, kwa uchache sana tunataka KATIBA MPYA YA WANANCHI kwa sababu katiba ndiyo inayotoa mwongozo (guidance) wa;
å Mwelekeo bora wa nchi kiuongozi na kiutawala
å Namna ya kupata viongozi wa serikali kwa njia sahihi, za wazi na za haki..
å Kudhibiti mamlaka na madaraka ya viongozi wa serikali waliopewa dhamana hizo...
å Utekelezaji na utoaji wa haki na hukumu kwa kila mtu kwa njia ya wazi, huru na haki..
å Mgawanyo sahihi wa majukumu ya kiutawala, uongozi na usimamizi wa shughuli za serikali...
3. Tunataka KATIBA mpya ya wananchi ili kwa pamoja kama wananchi wa nchi hii tujenge nchi yenye taasisi na mifumo imara ya kiutawala (unshakeable government administrayive institutions) isiyoyumba wala kutikisika bila kujali ni mtawala mkuu wa aina gani anatawala nchi, mwehu au kichaa; mwerevu au mjinga...
4. Tunataka Katiba mpya ili kuleta USAWA na HAKI kwa kila mwananchi wa nchi hii kushiriki kikamilifu na kwa UHURU kwenye shughuli za kiutawala wa nchi yake...
Labda mtu anaweza kujiuliza maswali haya. Na kiukweli ndiyo utetezi wa wafuasi wa CCM kupinga madai ya katiba mpya:
å Kwamba, Je, kwani kwa katiba hii iliyopo ya 1977 haiwawezeshi wananchi kushiriki kwenye shughuli za kiutawala wa nchi yao? Mbona huwa tunafanya uchaguzi mkuu kila baada ya miaka 5 tunachagua Rais, wabunge na madiwani na wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji? Je, hiyo siyo demokrasia, Uhuru na haki kwa wananchi?
å Au, je, kwani katiba ya 1977 haiwapi wananchi UHURU na HAKI ya kufanya shughuli zao za kila siku za kijamii, kiuchumi, na kisiasa?
Majibu ya maswali hayo yote ni mawili tu, ambayo ni:
Kwamba, katiba ya mwaka 1977 tunayotumia sasa ina kasoro kubwa mbili na hivyo kuifanya ikose uhalali wa kisiasa (political legitimacy) kuwa mwongozo HURU na wa HAKI kutumika ktk nchi hii...
Na hii ndiyo imeleleta matatizo yote haya tuliyayo leo kwa kiasi kikubwa yaani uwepo wa mifumo mibaya na dhaifu ya kiutawala, ya kiuchumi, na kiuongozi katika taasisi kuanzia ile ya juu ya Urais hadi huku chini..
Kwa kifupi, kasoro za katiba ya mwaka 1977 ambayo ndiyo inatumika sasa ni:
[A.] MOSI, si makubaliano ya WANANCHI WOTE kwa ujumla wao. Haikuandikwa na wananchi bali iliandikwa na watawala wachache...
Msingi wa katiba hii ya 1977 ni wa kikoloni iliyokuwa inalenga kulinda maslahi ya utawala wakoloni dhidi ya wenye nchi. Nasi baada yq uhuru tumerithi mfumo huohuo wa kikatiba huku watawala (CCM) wakichukua nafasi ya wakoloni na hivyo kujiwekea ulinzi wa kikatiba. Na ndiyo chanzo cha msemo huu, "CCM ni wakoloni weusi..". Maana yake ni hii..
Kumbukumbu za kihistoria zinasema iliandikwa na watu wasiozidi 22 tu waliojifungia sehemu chini ya Mwasisi wa taifa hili Mwl. Julius K. Nyerere..
[B.] PILI, katiba hii ya mwaka 1977 kuanzia mwanzo A to Z imerundika mamlaka ya kiutawala kwa mtu mmoja mwenye cheo na madaraka makubwa kupita kiasi ya kimaamuzi anayeitwa Rais...
Kwa mujibu wa katiba hii ya sasa ya 1977, Rais ndiye kila kitu. Ndiye anayeamua hata huko kijijini kwenu muishi vipi, mpate maendeleo gani na muwe na kiongozi gani...
HITIMISHO
1. Ndiyo maana kuna harakati za madai ya mfumo mpya wa kiutawala wa nchi hii kupitia madai ya katiba mpya ya wanachi..
2. Ndiyo maana kuna msuguano huu unaoendelea kati ya WATAWALA wanatetea mfumo unaowanufaisha na WATAWALIWA (wananchi) waliokwisha kugundua tatizo la mkwamo wa nchi yao.
3. Madai ya katiba hayana lengo la kuiondoa CCM madarakani japo yaweza kuleta matokeo hayo...
Lengo na kudai Katiba mpya ya wananchi ni kuwatengenezea mwongozo mzuri na wa haki ili waweze kutawala na kuhukumu kwa haki ktk nchi hii...
4. Kwa katiba hii tunayotaka kuiandika SISI WANANCHI WA TANZANIA itamweka yeyote kutawala nchi hii. Kama CCM watajinadi na wananchi kuwaelewa na wakawapa ridhaa ya kuongoza nchi hii tena na tena na tena, so be it so long as watayapata mamlaka ya uongozi huo wa nchi hii kwa njia za WAZI na HAKI...
THIS IS WHAT WE WANT. Sasa kwa nini tupigane? Kwa nini tunataka kuanza kuuana? Kwa nini tuanze kumbakiziana kesi za ugaidi?
AMA KUMBE NI KWELI:
"...mwanamke mjinga, huivunja Nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe...!!"
MWANAMKE MJINGA HAPO: ni CCM na serikali yao chini ya Rais Mama Samia Suluhu Hassan na NYUMBA HAPA ni Tanzania nchi yetu mzuri...
Sasa huyu wanamke mjinga anataka kuisambaratisha nyumba yake mwenyewe...!!
WATOTO TUKATAENI HILI, TUMPINGE HUYU MAMA "MJINGA" ATAKAYE KUIVUNJA NYUMBA YETU...!