Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan alikuja na mpango kabambe na uliokonga na kugusa mioyo ya mamilioni ya watanzania wa kuwapatia tabasamu, furaha, kicheko na matumaini wagonjwa mbalimbali walioko mikoani .kwa kuwasogezea huduma ya Madaktari Bingwa wa magonjwa mbalimbali karibu yao kabisa au karibu na majumbani kwao.
Hii maana yake nini? Maana yake ni kuwa mgonjwa aliyetakiwa kuuza kuku, ng'ombe, mbuzi, uwanja, mahindi ya chakula, nguruwe ili apate pesa ya nauli na matibabu kwenda Dar es salaam kuonana na madaktari bingwa sasa aliweza kusogezewa huduma ya kuonana na madaktari bingwa Kilometa chache tu kutoka nyumbani kwake pasipo gharama kubwa ya usafiri na matibabu.
Kuna wagonjwa walikuwa wamejikatia tamaa na kujilalia majumbani mwao na kusubiri tu huruma ya Mungu baada ya kuwa hawana uwezo wa kusafiri hadi muhimbili kupata huduma za kibingwa, lakini sasa chini ya mpango huu wa Dkt Samia wa kupeleka madaktari Bingwa mikoani wanakoweka kambi ya siku kadhaa kwa ajili ya kuonana na kutibu wagonjwa.umeweza kuponya wengi,kuwapa tabasamu na matumaini ya maisha watu wengi sana.
Kuna watu nimeshuhudia wakibubujikwa na machozi ya furaha baada ya kufanyiwa upasuaji wa Uvimbe ndani ya miili yao walioteseka nao kwa maumivu na uchungu mkubwa sana kwa muda mrefu, kutokana na umaskini wa kushindwa kusafiri hadi muhimbili kupata matibabu. Lakini leo kwa upendo wa mama, huruma za mama yetu kipenzi Mheshimiwa Mama Samia wameweza kufikiwa huko huko waliko na kupewa matibabu mazuri na kupona matatizo yao.
Madaktari Bingwa hawa wa mama wamesaidia kuokoa maisha ya watu,kuondoa maumivu na machungu ya watu,kuokoa mali za watu ambazo zingeuzwa kwa hasara kwa ajili ya kugharamia matibabu, pamoja na wakati mwingine kupoteza kabisa maisha kwa kukosa tiba sahihi kutokana na wengine kuamua kuanza kutumia mitishamba kwa wingi huku ugonjwa ukiendelea kukua na kukomaa na kuwa mkubwa na sugu.
Kwa huruma na upendo wa Rais Samia kwa watanzania wanyonge ameweza kufikisha mkono wake wa upendo kwa wagonjwa waliopo majumbani na kuwafuta machozi ya maumivu na kuwapatia tabasamu na matumaini ya kuendelea na maisha mapya yenye afya njema na nzuri kwa ajili ya ujenzi wa Taifa letu.
Nani kama Mama? Nani kama Rais Samia?
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan alikuja na mpango kabambe na uliokonga na kugusa mioyo ya mamilioni ya watanzania wa kuwapatia tabasamu, furaha, kicheko na matumaini wagonjwa mbalimbali walioko mikoani .kwa kuwasogezea huduma ya Madaktari Bingwa wa magonjwa mbalimbali karibu yao kabisa au karibu na majumbani kwao.
Hii maana yake nini? Maana yake ni kuwa mgonjwa aliyetakiwa kuuza kuku, ng'ombe, mbuzi, uwanja, mahindi ya chakula, nguruwe ili apate pesa ya nauli na matibabu kwenda Dar es salaam kuonana na madaktari bingwa sasa aliweza kusogezewa huduma ya kuonana na madaktari bingwa Kilometa chache tu kutoka nyumbani kwake pasipo gharama kubwa ya usafiri na matibabu.
Kuna wagonjwa walikuwa wamejikatia tamaa na kujilalia majumbani mwao na kusubiri tu huruma ya Mungu baada ya kuwa hawana uwezo wa kusafiri hadi muhimbili kupata huduma za kibingwa, lakini sasa chini ya mpango huu wa Dkt Samia wa kupeleka madaktari Bingwa mikoani wanakoweka kambi ya siku kadhaa kwa ajili ya kuonana na kutibu wagonjwa.umeweza kuponya wengi,kuwapa tabasamu na matumaini ya maisha watu wengi sana.
Kuna watu nimeshuhudia wakibubujikwa na machozi ya furaha baada ya kufanyiwa upasuaji wa Uvimbe ndani ya miili yao walioteseka nao kwa maumivu na uchungu mkubwa sana kwa muda mrefu, kutokana na umaskini wa kushindwa kusafiri hadi muhimbili kupata matibabu. Lakini leo kwa upendo wa mama, huruma za mama yetu kipenzi Mheshimiwa Mama Samia wameweza kufikiwa huko huko waliko na kupewa matibabu mazuri na kupona matatizo yao.
Madaktari Bingwa hawa wa mama wamesaidia kuokoa maisha ya watu,kuondoa maumivu na machungu ya watu,kuokoa mali za watu ambazo zingeuzwa kwa hasara kwa ajili ya kugharamia matibabu, pamoja na wakati mwingine kupoteza kabisa maisha kwa kukosa tiba sahihi kutokana na wengine kuamua kuanza kutumia mitishamba kwa wingi huku ugonjwa ukiendelea kukua na kukomaa na kuwa mkubwa na sugu.
Kwa huruma na upendo wa Rais Samia kwa watanzania wanyonge ameweza kufikisha mkono wake wa upendo kwa wagonjwa waliopo majumbani na kuwafuta machozi ya maumivu na kuwapatia tabasamu na matumaini ya kuendelea na maisha mapya yenye afya njema na nzuri kwa ajili ya ujenzi wa Taifa letu.
Nani kama Mama? Nani kama Rais Samia?
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.