Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,047
Suala la Hospitali Binafsi kuwaruzuku Madaktari Bingwa na Wa-kawaida kulingana na mapato au Bill ambazo wamesaini kwa mwaka/mwezi kunachangia ongezeko la sumu ya madawa kwa Wagonjwa na kunasababisha watu kujikusanyia magonjwa makubwa ya kudumu wakati wa matibabu. Saa nyingine katika kukuza bill hawa Madaktari wanasababisha wagonjwa kuchanganyikiwa.
Yamemkuta ndugu yangu wiki hii huko Dar. Jamaa alibaini uvimbe usio na maumivu mwilini mwake. Akaamua kwenda kuchunguza katika Hospitali binafsi yenye asili ya Kenya inayotoa hudumia za Bima ya Afya kwa mashirika mengi makubwa katika Mikoa ya Dar, Arusha na sasa wameingia Mwanza. Hapa akakutwa kila kitu kiko sawa. Walichofanya ni kuhakikisha mteja wao anafanya vipimo vya kila kifaa walichonacho kwenye Lab yao na mwisho wakampa magunia ya madawa japo walisema hakukutwa na ugonjwa wowote! Kampuni hii haina vifaa vya operation na uchunguzi mkubwa hivyo inapolazimika upate vipimo au huduma ya operation kubwa, wao hukupeleka kwenye Hospitali zingine. Wakifanya hivi, wao hulipa huko na hivyo hawapati faida sana. Mara nyingi unapoonekana hauna tatizo, hawawezi kukupa rufaa ya kwenda kufanya uchunguzi zaidi kwa watoa huduma wengine.
Jamaa yangu baada ya kupata majibu ya mtoa huduma ya Bima za afya wa kwanza akaamua kwenda kwenye hospitali nyingine binafsi ili alinganishe na awe na uhakika wa afya yake. Zamu hii akaenda katika moja ya Hospitali iliyo katika Mtandao wa Mahospitali makubwa sana katika ukanda wetu. Hospitali hii iko pembeni mwa ufukwe wa Bahari ya Hindi na barabara inayopita mbele yake Jumatatu ijayo itazawadiwa kwa Rais Barak Obama! Alipokutana na Daktari Bingwa kwenye hii hospitali akamuulezea hisia zake na vipimo alivyokwishapima. Daktari akamwambia lazima aanze upya. Vipimo vikachukuliwa, majibu yakaja sare na Hospitali ya kwanza. Daktari baada ya kuyasoma akamtaka afanye vipimo vingine zamu hii vikiwa ni vipimo vikubwa vikubwa. Navyo vikaja na majibu mazuri lakini kukawa na viashiria vya thyroid gland kutanuka. Mgonjwa akaambiwa atapingwa sindano kwenye shingo na pia afanye vipimo vingine vikiwemo vya vya cancer! Baada ya kupata mrejesho huu nikazama mtandaoni na nikajaribu kupata ushauri wa marafiki-Madaktari waliosoma enzi za Mwalimu. Nilichokifahamu na Waliponichambulia Madaktari wa zamani kimenistua sana. Biashara ya huduma ya afya sasa imevuka mipaka. Daktari bingwa anapombambikizia mteja vipimo vikubwa, magonjwa sugu na matibabu feki haina tofauti na askari anayembambikia mwananchi kesi! Ingekuwa amri yangu, afya na elimu zingekuwa huduma za Kikatiba, zingetolewa bure na zingetolewa na hospitali za umma tu. Sekta binafsi isingeruhusiwa kabisa kutoa huduma hizi.
Yamemkuta ndugu yangu wiki hii huko Dar. Jamaa alibaini uvimbe usio na maumivu mwilini mwake. Akaamua kwenda kuchunguza katika Hospitali binafsi yenye asili ya Kenya inayotoa hudumia za Bima ya Afya kwa mashirika mengi makubwa katika Mikoa ya Dar, Arusha na sasa wameingia Mwanza. Hapa akakutwa kila kitu kiko sawa. Walichofanya ni kuhakikisha mteja wao anafanya vipimo vya kila kifaa walichonacho kwenye Lab yao na mwisho wakampa magunia ya madawa japo walisema hakukutwa na ugonjwa wowote! Kampuni hii haina vifaa vya operation na uchunguzi mkubwa hivyo inapolazimika upate vipimo au huduma ya operation kubwa, wao hukupeleka kwenye Hospitali zingine. Wakifanya hivi, wao hulipa huko na hivyo hawapati faida sana. Mara nyingi unapoonekana hauna tatizo, hawawezi kukupa rufaa ya kwenda kufanya uchunguzi zaidi kwa watoa huduma wengine.
Jamaa yangu baada ya kupata majibu ya mtoa huduma ya Bima za afya wa kwanza akaamua kwenda kwenye hospitali nyingine binafsi ili alinganishe na awe na uhakika wa afya yake. Zamu hii akaenda katika moja ya Hospitali iliyo katika Mtandao wa Mahospitali makubwa sana katika ukanda wetu. Hospitali hii iko pembeni mwa ufukwe wa Bahari ya Hindi na barabara inayopita mbele yake Jumatatu ijayo itazawadiwa kwa Rais Barak Obama! Alipokutana na Daktari Bingwa kwenye hii hospitali akamuulezea hisia zake na vipimo alivyokwishapima. Daktari akamwambia lazima aanze upya. Vipimo vikachukuliwa, majibu yakaja sare na Hospitali ya kwanza. Daktari baada ya kuyasoma akamtaka afanye vipimo vingine zamu hii vikiwa ni vipimo vikubwa vikubwa. Navyo vikaja na majibu mazuri lakini kukawa na viashiria vya thyroid gland kutanuka. Mgonjwa akaambiwa atapingwa sindano kwenye shingo na pia afanye vipimo vingine vikiwemo vya vya cancer! Baada ya kupata mrejesho huu nikazama mtandaoni na nikajaribu kupata ushauri wa marafiki-Madaktari waliosoma enzi za Mwalimu. Nilichokifahamu na Waliponichambulia Madaktari wa zamani kimenistua sana. Biashara ya huduma ya afya sasa imevuka mipaka. Daktari bingwa anapombambikizia mteja vipimo vikubwa, magonjwa sugu na matibabu feki haina tofauti na askari anayembambikia mwananchi kesi! Ingekuwa amri yangu, afya na elimu zingekuwa huduma za Kikatiba, zingetolewa bure na zingetolewa na hospitali za umma tu. Sekta binafsi isingeruhusiwa kabisa kutoa huduma hizi.