Madaktari na Posho za Wabunge

Madaktari na Posho za Wabunge

sijui ni mlaumu nani kwa hili!ngoja nifikiri kidogo,ila wagonjwa wanaumia,na serikali nayo sio sikivu.sifungamani na upande wowote.

Una busara sana kuna wengine wanadhani mtu akifa anaweza kufufuliwa sio hekima kuunga mkono eti wagonjwa waendelee kufa ni bora usiwe na upande katika sakata kama hili.
 
Nyongeza za posho za wabunge zimefutwa hadi hapo serikali inatakapojiridhisha kwa nini waongezwe wao na sio sekta nyingine lakini pia kanuni inaagiza kwamba ni Rais anayetakiwa kuidhinisha posho hizo na nyongeza zake Waziri Mkuu alikosea kuidhinisha posho.


Waziri mkubwa alisema alipewa faili la kuongeza posho za wabunge kutoka kwa Rahisi wa CCM ( kikwete) na alipewa ruhusa kusaini au kutosaini.
 
nadhani serikali inapoendea ni kubaya sababu kuna sehemu nyingine nguvu haitakiwi bali ni busara
 
Kila kukicha afadhali ya jana. Matatizo kila leo source mfumo mbovu kama tungekuwa na mfumo mzuri haya yote yasingetukuta
Hivi kweli wangekuwa wanatibiwa ktk hospitali tunazotibiwa sisi mambo yangekuwa hivi. Hiyo katiba ingewabana watibiwe hapa na watoto wao wasome shule za serikali wasingekubali haya yatoke.
 
sijui ni mlaumu nani kwa hili!ngoja nifikiri kidogo,ila wagonjwa wanaumia,na serikali nayo sio sikivu.sifungamani na upande wowote.

Kwa haraka haraka daktari anayeanza kazi atakuwa analipwa milion 8 kwa mwezi,madai ya madaktari duh! Wakati haya yakitokea serikali imefunga baadhi ya vyuo vya uuguzi kwa kukosa hela ya gharama za uendeshaji!
 
Suala la posho ni tata sana na maangamizi makubwa kwa uchumi wenu.
Ningekuwa miongoni ningeshauri JMTz iziondoshe kabisaaaaa ili kuleta amani na mustakabali mzuri kwa Taifa na wananchi na kuondoa fitna.
 
mwenye kosa nani "mbunge" aliyejipandishia mshahara au "daktari" aliyeacha wagonjwa wafe??? :smash: inanipa hasira kweli.... haya na baada ya madaktari tujiandae kusikia waalimu, wanafunzi wa vyuo, wafanyakazi wa serikali na wengine wote kugoma..:focus: na ikiwezekana na mkuu wa nchi naye agome sjackia akiongezewa mshahara.. basi na mwisho kabisa wananchi wagome kuwa watanzania, wamama wagome kuzaa, watoto wagome kusoma na kukua dah... lakini msigome KULALAMIKA..... ndo jadi mpya kwenye jamii ya kitanzani msigome kucomment kwenye jf pia.
 
Tatizo la Madaktari ni kama la wabunge; Wala haina ubishi.

Kosa kubwa hapa ni la ubaguzi kama alivyosema Nyerere. Hebu fikiria Daktari mwenye Digrii moja na mhasibu wenye digrii moja eti Dr. 960,000 harafu mhasibu 300,000/-TZS. Makosa haya yamefanyika na serikali na sasa yanawatesa. Tumesome tulichosome kwa vile ni interest tu, sio kwamba daktari aliombwa na watz asome vile yeye anaakili sana, no ni mgawanyiko tu wa kazi ili wengine tufanye kazi zingine, sasa isije ikawa wanadhani ni bora kuliko kila mtu, hakuna. Wote tupo sawa, kama umesoma udaktari ni vile ulipenda, kama nimesoma uhasibu, kompyuta, uhandishi au fani yoyote ni vile tumependa wenyewe sio ombi la waTZ au serikali.

Sikubaliani kabisa na madaktari wa TZ, wanapenda masilahi kuliko hata kuchambua hali ya uchumi wa nchi ukoje, kwanza wangejiunga kukomboa uchumi, kudai vifaa bora vya matibabu na hali nzuri kwa wagonjwa ndipo waongelee mishahara na maposho yao; mbona tangu nipate akili sijawahi sikia dr. amegome kwa vile kina mama wanalala wawili kitanda kimoja, amegome vile hospitali hakuna vifaa vya kisasa, amegoma vile hospitali zipo chake angependa huduma ifike vijiji??? wao ndo wakwanza kutotaka kwenda hata vijijini.

Madaktari ni wataluma wa kwanza kuonesha kuwa wali ni limbukeni kwelikweli; Kwa kuungana na wabunge kudai posho zaidi ya % 100 pamoja na nyongeza ya mshahara kutoka 960,000/- hadi 3,500,000/- hivi hawa madaktari walisoma hata hesabu zile za BAM wakajua hizo % ni ngapi, je kada zingine nazo wakigoma nchi itakuwaje au tukitaka hilo ongezeko itakuwaje.

Nawasihi madaktari kama wanania ya dhati, basi tuungane kupinga posho za wabunge na sio kudai kama wabunge.
 
kwa maoni yangu Pinda yuko kwenye right track, piga chini wote heri tuanze upya tupate challenge nyingine kuliko wehu huu. fro 960,000 hadi 3,500,000/- pia na posho zenye kufikia % 110, kweli hili litawezekana wapi?

Tusiogope tuwapige chini tu, waende kwenye vidispensari vyao.
 
Back
Top Bottom