MOONFISH
Senior Member
- Jul 30, 2022
- 135
- 268
Ni kauli ya Mwanahamisi Ally, mkazi wa Mabibo, jijini Dar es Salaam.
Gazeti linasimulia mbinu kadhaa za uchunguzi alizotumia mwandishi kupima vipimo mbalimbali katika zahanati na hospitali mbalimbali, ili kuthibitisha malalamiko ya Mwanahamisi.
Jaribio la kwanza ‘‘Saa 6:30 mchana natoka Mabibo jijini Dar es Salaam, kuelekea ilipo moja ya zahanati binafsi, umbali wa takriban nusu kilomita kutoka eneo nililokuwepo, nikiwa na maji kwenye chupa ndogo ndani ya begi nililobeba.
Nilipofika kwa daktari nilimweleza kwamba nahisi naumwa UTI, nikitaja dalili zote ninazohisi katika mwili, ikiwemo homa, maumivu wakati wa haja ndogo na kichwa.
Baada ya kuchukua maelezo yangu, daktari alinielekeza kwenda maabara kupimwa malaria na UTI. Nilichukuliwa damu kwa ajili ya kupimwa malaria, kisha nikapewa kichupa cha kuweka mkojo ili upimwe UTI.
Msalani niliingia na begi langu lenye maji niliyoyaandaa, hivyo badala ya mkojo kwenye kichupa nilichopewa na daktari wa maabara niliweka maji hayo, ingawa nilihofu pengine yangegunduliwa.
Ningefanyaje wakati nataka kujua ukweli kuhusu alichoniambia Mwanahamisi? Nilipeleka maji kama yalivyo, yalipokelewa na nikaelekezwa kwenda mapokezi kusubiri majibu ya vipimo.
Baada ya dakika 20 nilitakiwa kuingia katika chumba cha daktari kupokea majibu na maelekezo mengine ya kitabibu kama ulivyo utaratibu wa siku zote hospitalini.
Napata ugumu kueleza hofu niliyokuwa nayo, nikidhani pengine wamegundua kwamba nimepeleka maji na si mkojo. Hapo nikawa najipanga nitakavyojibu iwapo nitagundulika, lakini nikipanga kutumia mbinu hata ya kutimka mbio.
Mungu si Athumani kama wasemavyo wahenga, daktari alinijibu mkojo wangu (kiuhalisia ni maji tu ya kunywa) umekutwa na UTI, aliniandikia dawa na kunielekeza kupeleka taarifa katika dirisha la dawa.
Katika duka hilo nilipewa dawa zilizoandikwa Azuma-500 na nilielekezwa kumeza kidonge kimoja kila siku kwa siku tatu, kulingana na idadi ya tembe zilizokuwapo katika boksi hilo la dawa.
Baada ya mwezi nilirudi tena katika zahanati hiyo kufanya vipimo vile vile na awamu hii daktari alisema, nina maambukizi katika mirija ya mkojo hivyo napaswa kuchoma sindano tano.
Kabla ya kuchoma sindano moja niliyotakiwa kuanza wakati huo, niliomba kuelekezwa ilipo ATM kwa ajili ya kutoa fedha ya kugharamia dawa na nilitumia mwanya huo kutorudi tena kuepuka kudungwa sindano hizo.
Hapo nilijiridhisha kwa kiasi fulani kwamba majibu ya kukutwa na UTI kila unapokwenda zahanati kama alivyosema Mwanahamisi ni tatizo linaloweza kusababishwa na vipimo visivyo na uhalisia katika baadhi ya zahanati, hasa za binafsi.
Jaribio la pili
Katika kuthibitisha zaidi kauli ya Mwanahamisi, nilikwenda katika hospitali nyingine kubwa binafsi, iliyopo wilayani Ubungo.
Safari hii niliwaomba wanadada wawili wanisaidie kufanikisha uchunguzi wangu na tulianza safari kwa bodaboda mbili hadi ilipo hospitali hiyo.
Ilikuwa saa 2:18 usiku, ni mwendo wa dakika 10 kwa bodaboda tuliyokuwa tumepanda kutoka tulipokuwa hadi ilipo hospitali hiyo.
Tukiwa na maji mkononi kwa ajili ya kuyatumia katika uchunguzi huo, tulifika katika hospitali hiyo na kuingizwa katika chumba cha huduma za dharura.
Pamoja na huduma ya kwanza aliyopatiwa mgonjwa (mmoja wa mwanadada niliyekuwa naye) kulingana na maelezo yake, alitakiwa kupimwa UTI, wingi wa damu na sukari.
Wakati wa kupima UTI, alipewa kikopo kwa ajili ya kuweka mkojo na walipofika msalani na dada mwingine waliweka maji ndani yake kisha kurudisha maabara.
Ilichukua dakika 30 vipimo kukamilika, kisha daktari alimwita na kumpa majibu, niliomba kuwepo wakati wa majibu hayo.
Licha ya hospitali hiyo kutupa huduma nzuri ambayo inaweza kumpa faraja mgonjwa yeyote anayefika hapo, tatizo likawa kwenye majibu ya UTI.
Daktari alitujibu alichokuwa anakisoma kwenye kompyuta akisema; “damu yake ipo sawa, shinikizo la damu lipo sawa, hana malaria lakini ana UTI kali sana.”
Hatukupewa nakala ya majibu kwa wakati huo na baada ya kuiomba nilielekezwa kwenda maabara kutaja jina la mgonjwa, kisha nitapewa na baada ya kufuata utaratibu huo, nilifanikiwa kupata ripoti hiyo ya kimaabara.
Daktari alituandikia dawa aina ya Tinidazale, Norflox na Paradenk kwa ajili ya kwenda kuzilipia na kuzichukua katika duka la dawa la hospitali hiyo.
Badala ya kununua dawa nilipopata nakala (gazeti linazo) ya majibu ya vipimo niliyoandikiwa na daktari wa maabara, tuliondoka moja kwa moja hadi nyumbani.
Jaribio la tatu