MADAKTARI: Vipimo vya UTI kama ni hivi ni balaa

MADAKTARI: Vipimo vya UTI kama ni hivi ni balaa

Kwani chief ,maabara wanaripoti kwamba patient ana UTI ? Or wanaripoti presence of pus cells in urine na ku-quantify only?

Nan humwambia patient ana UTI?

Mimi nafikiri kote kuna matatizo .....msomaji na mtafsiri wa majibu.
Chukulia mfano,
Urinalysis ripoti ambayo iko mfano wa picha hapo chini (zingatia leucocyte esterase + nitrite).

Most likely daktari ata suspect mgonjwa yuko na UTI. Kwa hospital ambazo hazina uwezo wa kufanya urine culture & sensitivity, daktari atafanya empirical treatment kwa kuprescribe antibiotic ampe mgonjwa.

Kama hayo majibu kila kitu kingekua normal, daktari asingetoa antibiotic ya aina yoyote kumpa mgonjwa.

Daktari hawezi kususpect UTI kwa kumuangalia mgonjwa kwa macho, lazima kuwe na report flani kutoka maabara itakayompa alert kwamba huyu mgonjwa kwa ripoti hii ya mkojo anaweza kuwa na UTI ndio maana wakati anamsikiliza mgonjwa mwanzo hakumpa dawa za UTI ila akasema nenda lab kapime urine. Ripoti ilipokuja alipoiona ndio akaandika dawa.

Kama mtaalamu wa maabara kafanya makosa katoa ripoti fyongo basi itaharibu mlolongo mzima wa matibabu.
images%20(5).jpg
 
Jaribio la tatu

Kama hiyo haitoshi, nilikwenda katika moja ya zahanati za umma kujiridhisha na vipimo, nikitumia maji ya bombani na hatimaye nayo yalikutwa na UTI.

Katika zahanati hii niliambiwa tatizo ni UTI na wingi wa damu na nilipewa dawa aina ya SPOTCLAV 625 na Meloxicam.

Jaribio la mwisho

Sikuishia hapo, katika kuthibitisha zaidi madai ya Mwanahamisi nilikwenda katika moja ya hospitali za rufaa jijini Dar es Salaam kuendelea na uchunguzi.

Hapa nilitumia maji ya bombani na tofauti na hospitali nilizoanza awali, hapo ilinichukua saa tatu kusubiri majibu ya vipimo na hata hivyo daktari alinijibu mkojo wangu haukuwa na shida.

Niliyoyakuta katika hospitali hiyo ndiyo yaliyotokea katika hospitali nyingine ya umma jijini humo, ambayo pia hakukuwa na changamoto ya vipimo, kwani sikukutwa na ugonjwa licha ya kutumia jaribio lile la kupima maji.

Si Mwanahamisi pekee

Kilichotokea kwa Mwanahamisi, pia kimetokea kwa Magreth Mondi na Abdallah Mpache wakazi wa Dar es Salaam, ambao nao wamelalamika kukutwa na ugonjwa huo mara kadhaa wanapokwenda hospitali.

“Yaani huchomoi hata ufanyeje lazima ukutwe na UTI. Zamani walikuwa wanasema si kila homa ni malaria, sasa hivi kila homa ni UTI,” anasema Magreth.

Ukweli kuhusu UTI

Licha ya majibu mazuri ya vipimo katika hospitali hizi, madaktari wa maabara walishindwa kugundua maji niliyopeleka badala ya mkojo, ambao kwa mujibu wa mtaalamu wa magonjwa ya binadamu, Profesa Andrea Pembe, vimiminika hivyo vina tofauti kubwa katika vipimo vya UTI.

Profesa Pembe anasema kuna tofauti kubwa ya mkojo na maji, hivyo wakati wa upimaji ni rahisi kugundua.

Akisisitiza hilo alisema: “Kwa sababu kinachopimwa ni specific gravity (tathmini ya ufanyaji kazi wa figo ili kutambua magonjwa ndani ya mkojo) ambayo kwa mkojo na maji ni tofauti kabisa.”

Katika kipimo cha UTI, anasema kinachoangaliwa ni kiwango cha wadudu ndani ya mkojo, chembe hai nyeupe za kupambana na magonjwa na naitrojeni inayozalishwa na wadudu kuwa ‘nitrates’ pamoja na seli zilizokufa za usaha, mambo ambayo hayapatikani katika maji.

Kuhusu maji kukutwa na UTI, Profesa Pembe kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), anasema UTI ni ugonjwa unaoambukizwa kwa njia ya mkojo pekee na si vinginevyo, hivyo maji hayawezi kuwa nao.

“Kwa sababu UTI ni ugonjwa unaoambukizwa kwa njia ya mkojo, maji ya kawaida hayawezi kuwa na UTI, haiwezekani kabisa na hata vimelea haviwezi kuwa huko,” alisisitiza.

Kauli ya mganga mkuu

Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Aifello Sichwale, alisema uwezekano wa kipimo kutoa majibu kinyume na uhalisia, unasababisha na moja kati ya mambo matatu ambayo ni mashine husika, vitendanishi na weledi wa mtaalamu husika.

“Kwa upande wa mashine inaweza kufanya hivyo kama imetumika kwa muda mrefu bila kufanyiwa matengenezo, maana matengenezo yanapaswa kufanywa kutokana na namna mashine inavyotumika,” alisema.

Alisisitiza kuwa jukumu la ubora wa mashine, vitendanishi na taaluma za wataalamu, linapaswa kufuatiliwa na waganga wakuu wa wilaya ama mkoa ilipo hospitali au kituo cha afya husika.

Kwa mujibu wa Dk Sichwale, katika kila robo ya mwaka, mganga wa wilaya au mkoa anatakiwa awe ametembelea vituo vilivyopo katika eneo lake walau mara moja.

“Hawa ndiyo wenye mamlaka ya kuhakikisha hospitali au vituo vya afya vilivyopo katika maeneo yao vinafanya kazi kwa kufuata miongozo ya Wizara ya Afya,” anasema Dk Sichwale. Alisema jukumu hilo hawapaswi kulitekeleza katika hospitali za umma pekee, bali hata binafsi wanatakiwa kufanya hivyo.

Hatari kunywa dawa za UTI

Kwa sababu wananchi hupewa tiba ya UTI ilhali hawaugui, Mfamasia mkuu wa Serikali, Daud Msasi anasema asili ya dawa yoyote ni sumu kwa ajili ya kuulia vimelea vya ugonjwa, hivyo ikitumika bila kuumwa inadhoofisha viungo vya mwili.

Alizitaja dawa hizo huchosha zaidi ini na figo, kwa kuwa zinapoingia mwilini zinapokelewa kama sumu na viungo hivyo huzipokea kwa ajili ya kuchuja hatimaye zigeuke mkojo.

“Figo na ini zinalazimishwa kufanya kazi ya ziada ambayo hazikupaswa kufanya kwa kutumia dawa kinyume na ugonjwa unaoumwa, hivyo madhara yake ni kufeli kwa figo na matatizo ya ini,” anasema.

Alishauri iwapo anayetumia dawa hizo bila kuumwa akafanikiwa kugundua, ni vema amalizie dozi ili kuepuka kuamsha vimelea vilivyopo mwilini kuanza kumshambulia na kisha visitibike kwa dawa yoyote kwa maana ya kutengeneza usugu.

Wataalamu maabara za afya

Wataalamu kutoka Chama cha Wataalamu wa Maabara za Afya ya Binadamu (MeLSATT), walisema kipimo cha UTI hutoka kati ya saa 48 hadi 72.

Kwa mujibu wa Roman Stephen, mwenyekiti wa dawati la habari wa MeLSATT, alisema siyo jukumu la wataalamu wa maabara kusoma matokeo ya vipimo, bali ni daktari.

“Daktari ndiye mtu atakayetoa tafsiri ya majibu ya vipimo kwa mgonjwa kulingana na mpangilio wa matibabu alioamua kuufuata kwa kuzingatia utaalamu wake,” alisema Stephen.

Alisema kuna wataalamu wasiozingatia kanuni za kutoa huduma ya afya, “mwenye ujuzi wa kusoma vipimo na haki ya kumueleza mgonjwa ni daktari,” alisema.

Kuhusu kipimo, Stephen alisema kwa kawaida wanapopokea mkojo wa mgonjwa maabara huuotesha kwa saa 24 hadi 48 ili kutazama kama una wadudu.

“Kufanya utambuzi wa mdudu na dawa inayoweza kumuua mdudu husika nayo inaweza kuchukua saa nyingine 24. Kwa hiyo jumla inaweza kuwa saa 72 au zikaongezeka.”

Hata hivyo, baadhi ya hospitali na zahanati zimekuwa zikitoa majibu ya vipimo hivyo ndani ya dakika 20 hadi 30 kama ambavyo uchunguzi wa gazeti hili umebaini katika maeneo iliyopita kupimwa.

Aidha, kumekuwa na udanganyifu kupitia ugonjwa wa UTI hivyo kuwatoza wagonjwa gharama za malipo ya kuona daktari, vipimo na dawa hasa kwa wagonjwa wa bi

NHIF yashtukia vipimo

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernard Konga alisema kumekuwa na udanganyifu mwingi ambao umekuwa ukifanywa na watoa huduma kuhusu vipimo, kikiwmao cha UTI, hali inayochangia kuumiza mfuko huo lakini wamekuwa wakipambana na hali hiyo.

“Udanganyifu upo na tumekuwa tukichukua hatua, tutasitisha mikataba ambayo itakuwa inahatarisha uendelevu wa mfuko. Kuna baadhi ya vituo ni rahisi kubambika dawa kwa mwanachama na tumekuwa tukiwabaini.

“Tumekuwa tukifuata mifumo kulingana na miongozo na tumekuwa tukichukua hatua ikiwemo kupiga faini, kuwaripoti wahusika katika mabaraza yao kama ni daktari basi tunatoa taarifa katika baraza la madaktari ili kuhakikisha tumelipia huduma halali kulingana na miongozo,” alisema.

Konga alisema ni kutokana na kuwapo kwa udanganyifu huo, walilazimika kuanza kufanya maboresho.

“Maboresho hayaepukiki na ni endelevu. Tumepokea maelekezo kutoka Wizara ya Afya na tumeyafanyia kazi maana ilileta taharuki,’’ alisema na kuongeza:

“Kwa mfano, maboresho tuliyoyafanya katika vipimo vya MRI na CT Scan kwamba lazima kuwe na kibali tulibaini wizi ulikuwa ukifanyika, vipimo ni Sh250,000 mpaka Sh400,000 walikuwa wanafanyiwa watu 800 kwa siku, lakini baada ya kuja na huo utaratibu wanapima 400 kwa siku, hivyo kulikuwa na udanganyifu.’’
Kila anayekwenda zahanati binafsi kama ana homa ni lazima ataambiwa ana UTI au malaria tena katika malaria wanaongezea na msemo wa malaria ringi 5 au ringi 7 😂nilimsikia aliyekuwa naibu waziri wa afya mbunge wa kigamboni alipokuwa akihojiwa kipindi hicho akiwa bado ni naibu waziri , alisema kwanza katika vipimo vya malaria hakuna kitu kinaitwa Ringi !! Na pia haiwezekani kipimo cha UTI kipatikane siku hiyo hiyo ulipopeleka mkojo !! Ni lazima vile vimelea vioteshwe kitaalamu ndio majibu yapatikane labda mpaka baada ya masaa 36 kwa uchache!! Hatari sana !!
 
1. Kwanza ieleweke hakuna ‘Daktari wa maabara’ bali kuna ‘mteknolojia maabara’
2. Kuna ombwe kubwa la maarifa na elimu kwa wataalamu wetu. Kwa maana ya madaktari, tabibu na wataalamu wa maabara. Kiufupi elimu yetu katika kuwaandaa wataalamu hawa kwasasa ipo chini.

3. ‘Conflict of Interest’ kati ya dhumuni la kituo (kuingiza mapato) vs taaluma.
4. Ujuaji wa wagonjwa hata wakipewa ushauri katika matatizo yao. Wengi siku hizi wamekuwa wabishi hususani wakirelate dalili zao na vile walivyoona mtandaoni. Huwalazimishi madaktari kufanya kile wanachokijua wao na sio anachokijua daktari.
 
Kwa anaefahamu kipimo cha hepatitis B kinachukua muda gani, Maana rafiki yangu alipewa majibu baada ya dkk 20 nikashangaa.
 
Kwa anaefahamu kipimo cha hepatitis B kinachukua muda gani, Maana rafiki yangu alipewa majibu baada ya dkk 20 nikashangaa.
Hepatitis B ipi alipima

Hepatitis B surface antigen?
Hepatitis B surface antibody?
Hep B core antigen/antibody?
Hep B viral load?
.
.
 
Jaribio la tatu

Kama hiyo haitoshi, nilikwenda katika moja ya zahanati za umma kujiridhisha na vipimo, nikitumia maji ya bombani na hatimaye nayo yalikutwa na UTI.

Katika zahanati hii niliambiwa tatizo ni UTI na wingi wa damu na nilipewa dawa aina ya SPOTCLAV 625 na Meloxicam.

Jaribio la mwisho

Sikuishia hapo, katika kuthibitisha zaidi madai ya Mwanahamisi nilikwenda katika moja ya hospitali za rufaa jijini Dar es Salaam kuendelea na uchunguzi.

Hapa nilitumia maji ya bombani na tofauti na hospitali nilizoanza awali, hapo ilinichukua saa tatu kusubiri majibu ya vipimo na hata hivyo daktari alinijibu mkojo wangu haukuwa na shida.

Niliyoyakuta katika hospitali hiyo ndiyo yaliyotokea katika hospitali nyingine ya umma jijini humo, ambayo pia hakukuwa na changamoto ya vipimo, kwani sikukutwa na ugonjwa licha ya kutumia jaribio lile la kupima maji.

Si Mwanahamisi pekee

Kilichotokea kwa Mwanahamisi, pia kimetokea kwa Magreth Mondi na Abdallah Mpache wakazi wa Dar es Salaam, ambao nao wamelalamika kukutwa na ugonjwa huo mara kadhaa wanapokwenda hospitali.

“Yaani huchomoi hata ufanyeje lazima ukutwe na UTI. Zamani walikuwa wanasema si kila homa ni malaria, sasa hivi kila homa ni UTI,” anasema Magreth.

Ukweli kuhusu UTI

Licha ya majibu mazuri ya vipimo katika hospitali hizi, madaktari wa maabara walishindwa kugundua maji niliyopeleka badala ya mkojo, ambao kwa mujibu wa mtaalamu wa magonjwa ya binadamu, Profesa Andrea Pembe, vimiminika hivyo vina tofauti kubwa katika vipimo vya UTI.

Profesa Pembe anasema kuna tofauti kubwa ya mkojo na maji, hivyo wakati wa upimaji ni rahisi kugundua.

Akisisitiza hilo alisema: “Kwa sababu kinachopimwa ni specific gravity (tathmini ya ufanyaji kazi wa figo ili kutambua magonjwa ndani ya mkojo) ambayo kwa mkojo na maji ni tofauti kabisa.”

Katika kipimo cha UTI, anasema kinachoangaliwa ni kiwango cha wadudu ndani ya mkojo, chembe hai nyeupe za kupambana na magonjwa na naitrojeni inayozalishwa na wadudu kuwa ‘nitrates’ pamoja na seli zilizokufa za usaha, mambo ambayo hayapatikani katika maji.

Kuhusu maji kukutwa na UTI, Profesa Pembe kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), anasema UTI ni ugonjwa unaoambukizwa kwa njia ya mkojo pekee na si vinginevyo, hivyo maji hayawezi kuwa nao.

“Kwa sababu UTI ni ugonjwa unaoambukizwa kwa njia ya mkojo, maji ya kawaida hayawezi kuwa na UTI, haiwezekani kabisa na hata vimelea haviwezi kuwa huko,” alisisitiza.

Kauli ya mganga mkuu

Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Aifello Sichwale, alisema uwezekano wa kipimo kutoa majibu kinyume na uhalisia, unasababisha na moja kati ya mambo matatu ambayo ni mashine husika, vitendanishi na weledi wa mtaalamu husika.

“Kwa upande wa mashine inaweza kufanya hivyo kama imetumika kwa muda mrefu bila kufanyiwa matengenezo, maana matengenezo yanapaswa kufanywa kutokana na namna mashine inavyotumika,” alisema.

Alisisitiza kuwa jukumu la ubora wa mashine, vitendanishi na taaluma za wataalamu, linapaswa kufuatiliwa na waganga wakuu wa wilaya ama mkoa ilipo hospitali au kituo cha afya husika.

Kwa mujibu wa Dk Sichwale, katika kila robo ya mwaka, mganga wa wilaya au mkoa anatakiwa awe ametembelea vituo vilivyopo katika eneo lake walau mara moja.

“Hawa ndiyo wenye mamlaka ya kuhakikisha hospitali au vituo vya afya vilivyopo katika maeneo yao vinafanya kazi kwa kufuata miongozo ya Wizara ya Afya,” anasema Dk Sichwale. Alisema jukumu hilo hawapaswi kulitekeleza katika hospitali za umma pekee, bali hata binafsi wanatakiwa kufanya hivyo.

Hatari kunywa dawa za UTI

Kwa sababu wananchi hupewa tiba ya UTI ilhali hawaugui, Mfamasia mkuu wa Serikali, Daud Msasi anasema asili ya dawa yoyote ni sumu kwa ajili ya kuulia vimelea vya ugonjwa, hivyo ikitumika bila kuumwa inadhoofisha viungo vya mwili.

Alizitaja dawa hizo huchosha zaidi ini na figo, kwa kuwa zinapoingia mwilini zinapokelewa kama sumu na viungo hivyo huzipokea kwa ajili ya kuchuja hatimaye zigeuke mkojo.

“Figo na ini zinalazimishwa kufanya kazi ya ziada ambayo hazikupaswa kufanya kwa kutumia dawa kinyume na ugonjwa unaoumwa, hivyo madhara yake ni kufeli kwa figo na matatizo ya ini,” anasema.

Alishauri iwapo anayetumia dawa hizo bila kuumwa akafanikiwa kugundua, ni vema amalizie dozi ili kuepuka kuamsha vimelea vilivyopo mwilini kuanza kumshambulia na kisha visitibike kwa dawa yoyote kwa maana ya kutengeneza usugu.

Wataalamu maabara za afya

Wataalamu kutoka Chama cha Wataalamu wa Maabara za Afya ya Binadamu (MeLSATT), walisema kipimo cha UTI hutoka kati ya saa 48 hadi 72.

Kwa mujibu wa Roman Stephen, mwenyekiti wa dawati la habari wa MeLSATT, alisema siyo jukumu la wataalamu wa maabara kusoma matokeo ya vipimo, bali ni daktari.

“Daktari ndiye mtu atakayetoa tafsiri ya majibu ya vipimo kwa mgonjwa kulingana na mpangilio wa matibabu alioamua kuufuata kwa kuzingatia utaalamu wake,” alisema Stephen.

Alisema kuna wataalamu wasiozingatia kanuni za kutoa huduma ya afya, “mwenye ujuzi wa kusoma vipimo na haki ya kumueleza mgonjwa ni daktari,” alisema.

Kuhusu kipimo, Stephen alisema kwa kawaida wanapopokea mkojo wa mgonjwa maabara huuotesha kwa saa 24 hadi 48 ili kutazama kama una wadudu.

“Kufanya utambuzi wa mdudu na dawa inayoweza kumuua mdudu husika nayo inaweza kuchukua saa nyingine 24. Kwa hiyo jumla inaweza kuwa saa 72 au zikaongezeka.”

Hata hivyo, baadhi ya hospitali na zahanati zimekuwa zikitoa majibu ya vipimo hivyo ndani ya dakika 20 hadi 30 kama ambavyo uchunguzi wa gazeti hili umebaini katika maeneo iliyopita kupimwa.

Aidha, kumekuwa na udanganyifu kupitia ugonjwa wa UTI hivyo kuwatoza wagonjwa gharama za malipo ya kuona daktari, vipimo na dawa hasa kwa wagonjwa wa bi

NHIF yashtukia vipimo

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernard Konga alisema kumekuwa na udanganyifu mwingi ambao umekuwa ukifanywa na watoa huduma kuhusu vipimo, kikiwmao cha UTI, hali inayochangia kuumiza mfuko huo lakini wamekuwa wakipambana na hali hiyo.

“Udanganyifu upo na tumekuwa tukichukua hatua, tutasitisha mikataba ambayo itakuwa inahatarisha uendelevu wa mfuko. Kuna baadhi ya vituo ni rahisi kubambika dawa kwa mwanachama na tumekuwa tukiwabaini.

“Tumekuwa tukifuata mifumo kulingana na miongozo na tumekuwa tukichukua hatua ikiwemo kupiga faini, kuwaripoti wahusika katika mabaraza yao kama ni daktari basi tunatoa taarifa katika baraza la madaktari ili kuhakikisha tumelipia huduma halali kulingana na miongozo,” alisema.

Konga alisema ni kutokana na kuwapo kwa udanganyifu huo, walilazimika kuanza kufanya maboresho.

“Maboresho hayaepukiki na ni endelevu. Tumepokea maelekezo kutoka Wizara ya Afya na tumeyafanyia kazi maana ilileta taharuki,’’ alisema na kuongeza:

“Kwa mfano, maboresho tuliyoyafanya katika vipimo vya MRI na CT Scan kwamba lazima kuwe na kibali tulibaini wizi ulikuwa ukifanyika, vipimo ni Sh250,000 mpaka Sh400,000 walikuwa wanafanyiwa watu 800 kwa siku, lakini baada ya kuja na huo utaratibu wanapima 400 kwa siku, hivyo kulikuwa na udanganyifu.’’
Me mwenyewe Kila nikienda hospital kupima.nikipima mkojo lazima niambiwe Nina UTI
 
Back
Top Bottom