Madaktari wa Tanzania waweka rekodi mpya Afrika na dunia kwa ujumla

Madaktari wa Tanzania waweka rekodi mpya Afrika na dunia kwa ujumla

Katika hali inayotia hamasa katika elimu ya Tanzania wakati wakenya wakiendelea kubeza elimu ya Tanzania ,watanzania wajivunia elimu yao na kufanya maajabu



Madaktari Tanzania wafanya upasuaji wa kihistoria

Saa 4 zilizopita

Mshirikishe mwenzako

ImageMadaktari wamewafanyia upasuaji wagonjwa wawili

Madaktari wa Tanzania katika hospitali ya taifa ya Muhimbili, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, wakishirikiana na wenzao wa India wamefanikiwa kufanya upasuaji wa moyo wa aina yake Tanzania.

Upasuaji huo ujulikanao kama ‘bypass surgery’ ulishirikisha kupandikizwa kwa mishipa ya damu kutoka sehemu nyingine ya mwili moyoni bila kutumia mashine ya kusimamisha moyo na mapafu.

Kwa kawaida madaktari wanasema upasuaji wa moyo hufanyika baada ya moyo na mapafu kusimama, lakini upasuaji huo ulifanyika wakati moyo na mapafu vikifanya kazi.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa Bashir Nyangasa ameambia BBC kuwa upasuaji huo wa kupandikiza mishipa ya damu nje ya mshine ni wa kihistoria nchini Tanzania.



“Mgonjwa anaweza kutolewa mishipa ya damu kutoka miguuni au mikononi baada ya kupewa dawa ya usingizi na mishipa hiyo kupandikizwa kwenye mshipa wa moyo uliokuwa umeziba ili kuruhusu mzunguko wa damu wa moyo kama kawaida bila kutumia mashine,” amesema.

Upasuaji huo wa moyo kwa njia ya kupandikiza umefanyika kwa watu wawili, ambao umeonesha mafanikio makubwa kwa kuwa hali zao zinaendelea vizuri .

Dkt Nyangasa amesema kwa sasa hakuna haja ya Watanzania wenye matatizo ya moyo kwenda nje ya nchi kwa kuwa wao kama wataalam wameweza kufanya upasuaji huo.



Anasema madaktari sasa wanaweza kuhudumia wagonjwa wengi zaidi wenye uhitaji na kupunguza gharama kwa serikali ya kusafirisha wagonjwa wa moyo nje ya nchi.

Mwandishi wa BBC aliyepo Dar es Salaam Esther Namuhisa anasema wengi wa wagonjwa wamekuwa wakisafiri hadi India ambapo wengi hukumbana na changamoto nyingi kupata huduma hiyo kifedha na hata kwenye upande wa lugha.


Source BBC SWAHILIView attachment 350990View attachment 350991


Jamani, naomba sana Watanzania acheni tabia ya kukimbila media ili kupata sifa.

Sijafahamu ni technolojia gani inayotoa assurance ya successful operation kabla hata mtu hajapata fahamu.

Lakini kingine, hakuna asiyejua ubingwa wa wahindi. Ninaona kwenye picha anayefanya procedures hapo ni kama mtu wa rangi. Au ndiye nyangasa? Wengine nawaona wanachunguilia kwa mbali ingawa wako kwenye plicha kama vile wanashuhudia. Tunajuaje wamefanya wao au walikuwa wanaonyeshwa inavyokuwaga?

Ninakumbuka uchunguliaji wa Ngeleja wakati akiwa kwenye msafara na vasco da gama eti kuonyesha naye alikuwa kwenye msfara wa raisi ulaya. Yasie kuwa yanajirudia.

Ninaobma mtotot apone, waendelee kufanya hizo operations bila ulazlima wa kuwa na wahindi, ndipo tushangilie .Kwa sasa tunaona ni wale wanaompa mgonjwa wa diabetes glucose halfu wanabadki wametoa mimacho na stethoscope kama wacheza sinema.

Tunaombea sana mabadiliko huduma za afya TAnzania na ndiyo sabbu tunahtaji waganga wetu wawe serious pamoja na serikali iwakumbuke Watnzania wanaokufa kama kuku wa kideli kwa kukosa huduma za afya. Usaanii wa kukimbila kwenye media kwa masuala ambayo hawajafanya wao, waache. Seriakli haiwezi kuwarubni wananchi kwa kutumia sinema na maigizo hatika kila jambo. La afya halpana. Tunahitaji uhalisia na ambao hauhitaji kupigiwa debe maana kila mtu atafahamu tu.
 
Wakenya wataendelea na misifa yao huku TZ inatusua.
 
Pambaffuuuuu...... weye bichwa kubwa, katika fani ya Utabibu Tanzania ina heshima yake, kuanzia kwenye ufundishaji.

Ndio bwana Kyenju sifa za madaktari wa Bongo tunazifahamu vizuri Kenya, maana wamejitangaza kila mahali. Mabango kama hili hapa chini yamejaa Kenya yote, wana ujuzi wa kutibu kila kitu. Wengine wanajinadi kutibu hata "ndoa","umaskini" sasa sijui mbona wameshindwa kuwatibu nyie.

20160428_090134.jpg
 
Wakenya wataendelea na misifa yao huku TZ inatusua.

Annael TZ inasua wapi? mmepata sauti juzi Magu alipoingia, side shows zishawaponza. Nawapa mwaka moja tu, mtarudi kuingiza mkia katikati ya miguu kama ilivyo desturi.
 
Pambaffuuuuu...... weye bichwa kubwa, katika fani ya Utabibu Tanzania ina heshima yake, kuanzia kwenye ufundishaji.
Pambaffuuuuu...... weye bichwa kubwa, katika fani ya Utabibu Tanzania ina heshima yake, kuanzia kwenye ufundishaji.

Tiba na elimu za kiasili hapo mmebobea, hata hamlinganishwi na nchi yeyote duniani, lakini upande wa modern medicine, hapo nina shaka.
 
Sasa mbona unaleta uzi huku ukijishuku na kuogopa ogopa Wakenya. Kwa taarifa yako tatizo kwenu ni nyie wenyewe, wala Wakenya hawahusiki. Elimu yenu ni duni kwa nyie watu wa kawaida, maana wenye hela zao hupeleka watoto wao kwa shule zenu za kimataifa zenye walimu Wakenya na Waganda.

Halafu hili la madaktari wenu kufanya vyema nalipatia hongera, lakini kumbuka Watanzania wenye hela na wanasiasa hawawezi kuwaamini hao madaktari na ndio kila akipata mafua anakimbilia Ulaya. Magonjwa kama tezi dume yakutibiwa hapo Muhimbili, lakini mkulu kaona vyema asiwaamini Waswahili wake.

Hivyo mjiangalie wenyewe na kutathimini, manweza kwenda mbali lakini huwa hamjiamini wala kuaminiana wenyewe kwa wenyewe.
Kazi yenyewe inajieleza hata usema hatujiamini au sijui walimu, lakini kazi imefanyika na mafanikio umeyakubali welcome you too for trusted service.
 
Kweli huu itakuwa ni upasuaji wa kihistoria hapa nchini ila sidhani kuwa hiyo elimu hasa elimu ya juu ni kutoka Tanzania.Thumbup!!
 
Back
Top Bottom