#COVID19 Madaktari waishauri Serikali chanjo ya Corona kuwa ya lazima

#COVID19 Madaktari waishauri Serikali chanjo ya Corona kuwa ya lazima

... hivi habari za chanjo bado zipo?!... Wapi Gwajigirl?!... Wanaanza lianzisha tena eeeh... Wasituhudumie ambao hatujachanja. FULL STOP
Wachanjwe wao wahudumu wa afya ili wasiambukizwe. Badala ya kujichanje wenyewe wanakwepa!
 
Wao wenyewe wanakazia swaumu kwa K vant then wanatushauri tuchanje
 
Mbona mnaongea utoto, kama wanakufa ina maana hawajapigwa chanjo, na kama wamepigwa chanjo ina maana haina uthibiti au kuimalisha kinga kwa mtu.

Sasa kwa nini mseme madaktari wanakufa ilihali hiyo chanjo haina uthibiti kwenye mwili?.
 
Swali la kujiuliza, madaktari wao wamechanjwa, sasa kama wamechanjwa wanakufaje wakati wamechanjwa na tuliambiwa ukichwanjwa haufi hata ukiugua na wala haulazwi?

Na kama hawajachanja, ina maana na wao hawaamini chanjo hiyo wanayotusisitiza sisi tuchanjwe?

Mbona hatulazimishani kwenda kutibiwa tukiugua, chanjo bure na bado tulazimishane, mbona matibabu mengine hatulazimishani?
Hiki ndio nimehoji hapo. Kuna tatizo sehemu
 
Yaani huna msimamo binadamu wewe? Unasema chanjo kwa lazima si jambo baya na unaliunga mkono. Wakati huo huo una mashaka na maswali mengi kuhusu ufanisi na usalama wa chanjo. Tukueleweje sasa??!!
Hujainelewa, ninasema kuwa lazima sio vibaya ila waondoe hiyo sintofahaamu
Watu tujue je hao madaktari wanaokufa waichanja au hawakuchanja
 
Madaktari wameishauri Serikali chanjo ya Corona iwe lazima. Si jambo baya na wapo sahihi kwa kuwa wao ni wataalamu.

Serikali haipaswi kukataa ushauri wowote wa wataalamu kwa maana mambo yakienda ndivyo sivyo watakuwa hawana wa kumwajibisha. Hivyo ushauri uzingatiwe pia.

Na mimi binafsi Sina shaka na huu ushauri wa hawa madaktari nguli kabisa, Hoja kubwa ni wataalamu wa afya kufariki wakiwa wanaendelea kupambana na ugonjwa wa corona, ila kuna mambo lazima waweke bayana.
  • wataalamu wa afya wanaendelea kufa, Ina maana hawa wataalamu wa afya walikuwa hawajapata chanjo? Ikiwa hawajapata, kwanini? Na wao ndio sisi tunategemea wawe mfano kwenye kutumia sayansi kukabili huu ugonjwa, hapa pana wasiwasi.
  • Ikiwa walipata chanjo, maswali yatabaki kwanini wanakufa kwa Corona ikiwa tayari walipata chanjo. Ina maana tutarudi kuwaambia watu kuwa chanjo haizuii kufa kwa corona?
Nimejaribu kujiuliza hivyo pia si kwa ubaya, ila vyovyote vile bado Kuna nafasi ya kupambana na huu ugonjwa na kuutokomeza.
Inawezekana walipata maambukizi kabla ya chanjo, ujue chanjo haitibu ila inakupunguzia kiwango cha kuugua.
 
Madaktari wameishauri Serikali chanjo ya Corona iwe lazima. Si jambo baya na wapo sahihi kwa kuwa wao ni wataalamu.

Serikali haipaswi kukataa ushauri wowote wa wataalamu kwa maana mambo yakienda ndivyo sivyo watakuwa hawana wa kumwajibisha. Hivyo ushauri uzingatiwe pia.

Na mimi binafsi Sina shaka na huu ushauri wa hawa madaktari nguli kabisa, Hoja kubwa ni wataalamu wa afya kufariki wakiwa wanaendelea kupambana na ugonjwa wa corona, ila kuna mambo lazima waweke bayana.
  • wataalamu wa afya wanaendelea kufa, Ina maana hawa wataalamu wa afya walikuwa hawajapata chanjo? Ikiwa hawajapata, kwanini? Na wao ndio sisi tunategemea wawe mfano kwenye kutumia sayansi kukabili huu ugonjwa, hapa pana wasiwasi.
  • Ikiwa walipata chanjo, maswali yatabaki kwanini wanakufa kwa Corona ikiwa tayari walipata chanjo. Ina maana tutarudi kuwaambia watu kuwa chanjo haizuii kufa kwa corona?
Nimejaribu kujiuliza hivyo pia si kwa ubaya, ila vyovyote vile bado Kuna nafasi ya kupambana na huu ugonjwa na kuutokomeza.
I highly support the advise.
 
Madaktari wameishauri Serikali chanjo ya Corona iwe lazima.
===
Madaktari gani, wa wapi, waliishauri serikali lini, wakiwa wapi?
Nikiweka screenshot ya taarifa chini Ila naona admin kaitoa
Ni madaktari wa mikoa(RMO) walikuwa wakizungumza na katibu wa wizara ya afya.
 
Inawezekana walipata maambukizi kabla ya chanjo, ujue chanjo haitibu ila inakupunguzia kiwango cha kuugua.
Ina maana hao madaktari hawakupima covid kabla ya kuchanja?
Kuna maswali mengi hapo
 
Mbona viongozi wa chadema hatuwaoni wakichoma chanjo? Nakumbuka kipindi cha mwendazake walikuwa mstali wa mbele kudai chanjo
 
Hujainelewa, ninasema kuwa lazima sio vibaya ila waondoe hiyo sintofahaamu
Watu tujue je hao madaktari wanaokufa waichanja au hawakuchanja
Kama tayari una mashaka, unakubalije chanjo iwe lazima??!!
 
Zoezi la chanjo lingeliunganishwa na zoezi la Sensa ili kurahisisha na kuweka takwimu vizuri zaidi.
Hata hivyo Madaktari wangelibuni mbinu mbadala ya kurahisisha utoaji wa chanjo kwenye Hospital zote nchini ikiwa ni pamoja na wenye kutembelea ndugu, jamaa na rafiki kwenye Hospital za Serikali na Binafsi walau miongoni mwao wawe wamepata chanjo.
 
Kama tayari una mashaka, unakubalije chanjo iwe lazima??!!
Wakiondoa hiyo sintofahamu mashaka yanabaki vipi tena?
Ni sawa na wale wanaosema tozo ziwepo ila tuambiwe zinapopelekwa
 
Back
Top Bottom