Madaktari wameshauri akatwe miguu

Madaktari wameshauri akatwe miguu

Nenda Tanga,njia ya Kwenda Mombasa Kenya,njiani upande wa Tanzania,kuna Kijiji kinaitwa Kibiboni,ukipanda bus za Dar Tanga Msa,mwambie konda akushushe hapo,yupo mtaalam,Mtanzania,ni dr wa tiba za asili(tibap mbadala wa mifupa,hapo nina uhakika tatizo la mtoto wako litakwisha.

Asante mkuu nitaangalia cha kufanya
 
ni mfupa gani anao..???
-kama mfupa alionao ni fibula(yani hana tibia) sidhani kama ataweza kutembea
-ila kama ana tibia(yani hana fibula) nadhani ataweza kutembea maana kuna watu kibao wanafanyiwa "bone grafting" kwa kuondolewa fibula na wanatembea kama kawaida tu na hata kukimbia yani wanakuwa normal kabisa
ushauri wangu jaribu kwenda hospitali kubwa zaidi na hata ikibidi hospitali za nje

Nimeshindwa kuiweka report kwa sababu si mtaala anasimamamu sana wa mambo haya isipokuwa mfupa aliokuwa hana ni tibia kwa sababu wameandika tibia not palpable both legs sasa ninachojiuliza mbona kuna baadhi ya wakati huwa akipata sehemu ya kushika au sasa nyingine huwa kama vile anataka kusimama yaani anakuwa amekaa halafu kama vile anapata hamu ya kusimama anashika mikono chini then anainuka miguu yote inainuka kabisa yaani huwa anafanya jana vile wanavyofanya watoto wanaojifunza kusimama
 
pole sana mkuu, huo ni mtihani mgumu kweli jamani,naomba Mungu akuongoze ufanye maamuzi sahihi
 
pole sana mkuu! sijajua kiundani tatizo la mtoto wako ni lipi , ila kutokana na maelezo yako naona linafanana na hemimelia (fibular hemimelia au tibial hemimelia au fibular and tibial hemimelia)ki

hayo ni miongoni mwa matatizo makubwa sana katika afya ya mtoto na matibabu yake ni magumu sana,,,,,,,,,

ninaweza kurudi baadae na shule kamili ila kwa kifupi kuna option 2 za matibabu........

1. ya kwanza ni hiyo ya kukata mguu ( amputation) ili kuweza kujifunza matumizi ya miguu ya bandia katika umri mdogo , huku akibadilishiwa kila mwaka kulingana na anavyokua.

2. ni upasuaji wa mfululizo wa kurekebisha hiyo hali kila anapokua , hii ina athari nyingi sana ikiwemo deformities na maumivu ya mara kwa mara bila kusahau ni bei ghali sana na inafanyika marekani.[/
QUOTE]


Report iko hivi mkuu
Diagnosis
.congenital bilateral tibia hemimelia with dislocation of both ankle joint and subluxation of knee joint


Examination.
.bilateral prominent femoral condyles
.tibia not palpable both legs
.Rom knee flexion 0-100 degrees
.bilateral dislocation of ankle and subluxation of knee joint

Nadhani umeipata picha mkuu kwa sababu nahitaji kuamua njia gani na yenye manufaa kwa mtoto nichague
 
pole sana mkuu, huo ni mtihani mgumu kweli jamani,naomba Mungu akuongoze ufanye maamuzi sahihi

Asante sana mkuu nashukuru Mungu kanitia nguvu sana juu ya hilo jambo sijawahi kutetereka namuona mtoto wa kawaida tu
na isitoshe mtoto mwenyewe ni mchangamfu sana ukimkuta anacheza wala huwezi gundua kama anamatatizo
 
Asante sana mkuu nashukuru Mungu kanitia nguvu sana juu ya hilo jambo sijawahi kutetereka namuona mtoto wa kawaida tu
na isitoshe mtoto mwenyewe ni mchangamfu sana ukimkuta anacheza wala huwezi gundua kama anamatatizo
zidi kumtegemea yeye na kumshukuru kila uchao kwa ajili ya huyo mtoto na wala usije kumlaumu kwa kukupa mtoto mwenye tatizo km hilo, naamini ipo siku huyu anaeumba kwa namna anayoijua yeye atakisikia kilio chako na kumsaidia mwanao mpenzi ktk hilo........Mungu azidi kukutia nguvu mkuu
 
Hata kama ingekuwa Marekani wameshauri hivyo, usikubaliane na huo ushauri mkuu. Mungu pekee ndo mwenye final say on whether miguu inakatwa au inabaki. Ushauri wangu do not pursue with the Doctors' option.
Rudini mbele za Mungu nae atamponya na atatembea kama kawaida. Kumbuka injili aliyoleta Yesu iliponya wagonjwa vilema wakatembea. Hakuna kisichowezekana kwake yeye aaminiye. Kama huamini nakushauri uendelee kuwasikiliza hao madaktari ila kama unaamini kuwa Mungu muumba anaweza acha kijana aje kutembea na miguu yake ikiwepo.
Ni hayo tu


duh! mmmmmmmmmh!
 
Ni kweli.
Kama alivyoshauriwa yule ndugu mwenye kansa ya figo, hebu onana na madaktari wengi iwezekanavyo. Nenda ccbrt na ingia mtandaoni ufanye mawasiliano na hospitali za ulaya kwa email. Scan ripoti ya dr na uwatumie tu waambie natafuta 2nd opinion.

Mungu awasaidie kwa wakati. Kila la kheri
Mkuu kwanini apelekwe India badala ya CCBRT Hospital, Msasani, Dar es Salaam???????

Piga namba hizi kwa uhakika zaidi; + 255222602192 ‎
 
mkuu je unaweza kunipa detail ya hizo hospital za marekani ama popote duniani wanapoweza kufanya hiyo tiba nipate kuwasiliana nao ili nione uwezekano wa kumpeleka huko kama tutafikia muafaka na uwezo utaruhusu
 
Nina mtoto mwenye umri wa mwaka moja na busy na amezaliwa na ulemavu wa miguu yaani anamfupa mmoja kila mguu madaktar Wanasema akatwe miguu kuanzia kwenye magoti ili aanzishwe mazoezi ya viungo bandia sasa ninachojiuliza jee taratibu za kitabibu zinasemaje kuhusu ya kukata viungo vya mtoto mdogo kama huyu na jee nyie akizaliwa na mfupa mmoja hawezi kutembea kwamba ile mfupa hauna uwezekano wa kutembea
jamani, Mungu awape ufumbuzi wa hii shida. Mungu awatendee muujiza kwa huyu malaika wake.
 
Back
Top Bottom