madaktari wote Tanzania ni madaktari?

madaktari wote Tanzania ni madaktari?

lovey62

Senior Member
Joined
Apr 13, 2013
Posts
132
Reaction score
112
wakuu,last week nilikuwa Kenya kuudhuria jambo fulani hivi.nikapata kusocialize na baadhi ya wakenya.niliulizwa maswali mengi ikiwemo utata wa kuwepo kwa watu wengi wenye tittle ya "DOCTOR" ndipo nilipoulizwa kama je hata waganga wa kienyeji waitwa madaktari hapa kwetu?tulijadili hili ndugu zangu
 
Mzizimkavu naye anataka aitwe Dr, hii ni tatizo kwa wapenda sifa wote wanataka waitwe madaktari, JK mwenyewe from my heart hastahili kuitwa Dr kama hajakwenda shule, sasa kama rais wa nchi anapenda kuitwa Dr wakati hastahili je wengine huku mtaani si kila mtu atajiita Dr
 
Mkuu lovey62, nadhani hii ingekuwa kule kwenye jukwaa la hoja mchanganyiko, hata hivyo ningesema;

Daktari, hapa neno hili linaweza kutumika kama vile Tabibu (mtu wa fani/taaluma ya Afya, hasa ya binadamu) yaani MD na pia inaweza kutumika kama cheo, yaani mtu fulani aliyepata(acquire) elimu fulani ya juu ya Falsafa), yaani PhD.

Tofauti na hapo, ni ngumu kuthibitisha 'udaktari' wa kila aliye daktari!
 
Last edited by a moderator:
Mzizimkavu naye anataka aitwe Dr, hii ni tatizo kwa wapenda sifa wote wanataka waitwe madaktari, JK mwenyewe from my heart hastahili kuitwa Dr kama hajakwenda shule, sasa kama rais wa nchi anapenda kuitwa Dr wakati hastahili je wengine huku mtaani si kila mtu atajiita Dr
Mkuu Mupirocin mimi sijiiti Doctor ila wanachama wa humu ndani ndio

walionipachika jina la Doctor mkuu. Kwani kuna ubaya gani mimi kuitwa Doctor? au wewe hupendelee Mimi kuitwa Doctor Mupirocin? Kwani

nikitwa Doctor kutakuwa na ubaya wowote ule? Si heshima tu au unaonaje? Basi mimi ningewaomba Wanachama wakwite wewe

Doctor Mupirocin? unaonaje? acha wivu wako wa kijinga huo Mkuu Mupirocin. Kuna ubaya gani Rais wetu na Kiongozi wetu wa nchi kuitwa

Doctor JK. hata kama hajakwenda shule wewe kinachokuuma kitu gani? Mbona tunamwita Mwalimu Nyerere Baba wa Taifa hili la

Tanzania kwani sisi Wa-Tanzania hatuna Baba yetu mpaka tukamwita Mwalimu Nyerere Baba wetuwa Taifa hili la Ki-Tanzania? Acha

Siasa zako za kipotufu wewe Doctor Mupirocin Mzima huwezi hata kutumia akili zako za U-Doctor?ndivyo ulivyofundishwa huko Shule

uliposoma nini kudharau watu wengine?
 
DR Nchimbi= Dr Matunge=DR Remmy(RIP)

Anaitwa Dr Emmanuel Nchimbi kama kionjo cha lugha lakini academically NUNGE PhD Fake za Mzumbe
 
Hapana.... Wengine nikama JK, wanajibandika vyeo tu
 
wakuu,last week nilikuwa Kenya kuudhuria jambo fulani hivi.nikapata kusocialize na baadhi ya wakenya.niliulizwa maswali mengi ikiwemo utata wa kuwepo kwa watu wengi wenye tittle ya "DOCTOR" ndipo nilipoulizwa kama je hata waganga wa kienyeji waitwa madaktari hapa kwetu?tulijadili hili ndugu zangu

Digirii za kuhenya:
Kuna wenye shahada kutoka vyuo stahiki (k.m., PhD, MD, DDS, DPT, JD, n.k.) ambao wanastahili kuheshimiwa kwa kuitwa ma-Dr. Kama chuo alichopatia hii shahada kina utata basi tuchunguze lakini anastahili kupewa title yake mpaka hapo tutakapothibitisha kuwa hastahili.

Digirii za kutunukiwa (heshma):
Sasa kuna hizi digrii za kutunukiwa kama Ph.D. honoris causa (latin: for the sake of the honor). Hizi shahada za heshima zinatolewa na vyuo vikuu kwa mtu katika kutambua mchango wa kazi yake maishani. Hii shahada ina uzito sawa na ile aliohenyea mtu kwa kufanya research, kuandika desertation, na kui-defend kwenye kamati yake. Hivyo basi mtu aliepewa Ph.D. honoris causa anastahili kuitwa Dr.

Dr. Kikwete, Dr. Mengi, late Dr. Nyerere wote wanastahili kupewa heshima hiyo. Wengi wanaopewa hizi Ph.D. honoris causa hawapendi kuitwa hadharani Dr. kama alivyokuwa mwalimu Nyerere. Lakini mara nyingi hii michango inayomfanya mtu apewe honorary degree ni mikubwa sana kuliko hata a simple written desertation ilioandikwa kwa miaka 3 au 4. (my humble opinion, as a holder of a non-honorary Ph.D.)

Nani mwengine ni Dr.?
Katika safu yangu, wa kwanza kuitwa Dr. ni marehemu babu yangu aliekuwa mganga mashuhuri sana wa kienyeji kijijini kwetu who never saw the inside of a formal classroom. Watu wote wengine wanaotoa michango au ushauri mzuri kama ya tiba mbadala (Dr. MziziMkavu), mapenzi/mahusiano (Dr. Love - hivi nani hapa JF anapaswa kupewa hii heshima?), n.k. Kwa maoni yangu mtu yeyote anaejihisi ana ujuzi zamilifu kwenye fani yake anaweza tu kujiita Dr. Udaktari uchwara utajulikana haraka sana.

Nawasilisha.
 
Mzizimkavu naye anataka aitwe Dr, hii ni tatizo kwa wapenda sifa wote wanataka waitwe madaktari, JK mwenyewe from my heart hastahili kuitwa Dr kama hajakwenda shule, sasa kama rais wa nchi anapenda kuitwa Dr wakati hastahili je wengine huku mtaani si kila mtu atajiita Dr



Mkuu Mupirocin, Mheshimiwa MziziMkavu hajasema wala kulazimisha kuitwa daktari....yule mheshimiwa ni daktari kama vile anavyoitwa Mheshimiwa Kikwete japo Kikwete hana faida na watanzania ila MziziMkavu ana faida kubwa sana kwa jamii yetu kwani anatoa mchango mkubwa sana humu JF na katika jamii yote. Binafsi, ndugu yangu (mpwa) amepona magonjwa yaliyomsibu kwa ajili ya MziziMkavu. Huyu mtu ni wa kumwogopa na ndiyo maana nataka nimpe uwaziri wa jamii/afya kunako 2015 nikishinda urais. Kaeni mkao wa kula :msela:
 
Last edited by a moderator:
Ushaanza kwa kuwaita madaktari, halafu unauliza "ni madaktari"?

Nikitaka kukuelewa wewe mwenyewe siwezi. Seuze hao madaktari unaowahoji.

Kwa maana umeanza kwa kujikanganya.Kwa kuuliza kama madaktari ni madaktari.

At the risk of blaming the victim, mimi nitaondoka kwenye madaktari, na kusema "wanaojisema wana elimu ya msingi Tanzania wote wana elimu ya msingi?"
 
Mkuu Mupirocin mimi sijiiti Doctor ila wanachama wa humu ndani ndio

walionipachika jina la Doctor mkuu. Kwani kuna ubaya gani mimi kuitwa Doctor? au wewe hupendelee Mimi kuitwa Doctor Mupirocin? Kwani

nikitwa Doctor kutakuwa na ubaya wowote ule? Si heshima tu au unaonaje? Basi mimi ningewaomba Wanachama wakwite wewe

Doctor Mupirocin? unaonaje? acha wivu wako wa kijinga huo Mkuu Mupirocin. Kuna ubaya gani Rais wetu na Kiongozi wetu wa nchi kuitwa

Doctor JK. hata kama hajakwenda shule wewe kinachokuuma kitu gani? Mbona tunamwita Mwalimu Nyerere Baba wa Taifa hili la

Tanzania kwani sisi Wa-Tanzania hatuna Baba yetu mpaka tukamwita Mwalimu Nyerere Baba wetuwa Taifa hili la Ki-Tanzania? Acha

Siasa zako za kipotufu wewe Doctor Mupirocin Mzima huwezi hata kutumia akili zako za U-Doctor?ndivyo ulivyofundishwa huko Shule

uliposoma nini kudharau watu wengine?
Huyu jamaa MziziMkavu akiguswa kidogo anatoka povu kama kifutu. Ila ukweli utabaki palepale-mnaojiita madokta bila kusoma ni weupe tu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mupirocin, Mheshimiwa MziziMkavu hajasema wala kulazimisha kuitwa daktari....yule mheshimiwa ni daktari kama vile anavyoitwa Mheshimiwa Kikwete japo Kikwete hana faida na watanzania ila MziziMkavu ana faida kubwa sana kwa jamii yetu kwani anatoa mchango mkubwa sana humu JF na katika jamii yote. Binafsi, ndugu yangu (mpwa) amepona magonjwa yaliyomsibu kwa ajili ya MziziMkavu. Huyu mtu ni wa kumwogopa na ndiyo maana nataka nimpe uwaziri wa jamii/afya kunako 2015 nikishinda urais. Kaeni mkao wa kula :msela:
hizi nyazifa za kupeana ndiyo zitatupeleka kuzimu-eti MziziMkavu apewe uwaziri wa afya na maendeleo ya jamii?
 
Last edited by a moderator:
Digirii za kuhenya:
Kuna wenye shahada kutoka vyuo stahiki (k.m., PhD, MD, DDS, DPT, JD, n.k.) ambao wanastahili kuheshimiwa kwa kuitwa ma-Dr. Kama chuo alichopatia hii shahada kina utata basi tuchunguze lakini anastahili kupewa title yake mpaka hapo tutakapothibitisha kuwa hastahili.

Digirii za kutunukiwa (heshma):
Sasa kuna hizi digrii za kutunukiwa kama Ph.D. honoris causa (latin: for the sake of the honor). Hizi shahada za heshima zinatolewa na vyuo vikuu kwa mtu katika kutambua mchango wa kazi yake maishani. Hii shahada ina uzito sawa na ile aliohenyea mtu kwa kufanya research, kuandika desertation, na kui-defend kwenye kamati yake. Hivyo basi mtu aliepewa Ph.D. honoris causa anastahili kuitwa Dr.

Dr. Kikwete, Dr. Mengi, late Dr. Nyerere wote wanastahili kupewa heshima hiyo. Wengi wanaopewa hizi Ph.D. honoris causa hawapendi kuitwa hadharani Dr. kama alivyokuwa mwalimu Nyerere. Lakini mara nyingi hii michango inayomfanya mtu apewe honorary degree ni mikubwa sana kuliko hata a simple written desertation ilioandikwa kwa miaka 3 au 4. (my humble opinion, as a holder of a non-honorary Ph.D.)

Nani mwengine ni Dr.?
Katika safu yangu, wa kwanza kuitwa Dr. ni marehemu babu yangu aliekuwa mganga mashuhuri sana wa kienyeji kijijini kwetu who never saw the inside of a formal classroom. Watu wote wengine wanaotoa michango au ushauri mzuri kama ya tiba mbadala (Dr. MziziMkavu), mapenzi/mahusiano (Dr. Love - hivi nani hapa JF anapaswa kupewa hii heshima?), n.k. Kwa maoni yangu mtu yeyote anaejihisi ana ujuzi zamilifu kwenye fani yake anaweza tu kujiita Dr. Udaktari uchwara utajulikana haraka sana.

Nawasilisha.
ulianza vizuri lakini ukaharibu mbaya ulipomtaja babu yako eti naye ni dokta.
 
Narudia tena. Mkuu georgeallen, kama una ushahidi wa maovu ya huyu MziziMkavu njoo ofisini kwangu utupe ushuhuda ili tujiepushe naye mapema.
sijazungumzia maovu ya mtu bali nazungumzia talanta na merit. waatu wapewe uongozi by merit na wawe na talanta ya uongozi. siyo kwa sababu ya kujuana au alikuponyesha kwa mizizi
 
sijazungumzia maovu ya mtu bali nazungumzia talanta na merit. waatu wapewe uongozi by merit na wawe na talanta ya uongozi. siyo kwa sababu ya kujuana au alikuponyesha kwa mizizi
Mkuu georgeallen Mimi ukiniita kwa jina langu kamili MziziMkavu Hauchimbwi dawa peke yake Tosha usiite doctor wala waziri wa Afya niite kwa jina langu tu poa sana huwa ninafurahi si unajuwa hakuna jina linalofanana na jina langu kwenye hizi forums zote za duniani? Tafuta jina la MziziMkavu kwenye Google hutapata MziziMkavu mwengine ila mimi tu kaka georgeallen jina langu tosha kwa kila kitu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu georgeallen Mimi ukiniita kwa jina langu kamili MziziMkavu Hauchimbwi dawa peke yake Tosha usiite doctor wala waziri wa Afya niite kwa jina langu tu poa sana huwa ninafurahi si unajuwa hakuna jina linalofanana na jina langu kwenye hizi forums zote za duniani? Tafuta jina la MziziMkavu kwenye Google hutapata MziziMkavu mwengine ila mimi tu kaka georgeallen jina langu tosha kwa kila kitu.
Hapa umejibu kiukubwa -hongera sana
 
Digirii za kuhenya:
Kuna wenye shahada kutoka vyuo stahiki (k.m., PhD, MD, DDS, DPT, JD, n.k.) ambao wanastahili kuheshimiwa kwa kuitwa ma-Dr. Kama chuo alichopatia hii shahada kina utata basi tuchunguze lakini anastahili kupewa title yake mpaka hapo tutakapothibitisha kuwa hastahili.

Digirii za kutunukiwa (heshma):
Sasa kuna hizi digrii za kutunukiwa kama Ph.D. honoris causa (latin: for the sake of the honor). Hizi shahada za heshima zinatolewa na vyuo vikuu kwa mtu katika kutambua mchango wa kazi yake maishani. Hii shahada ina uzito sawa na ile aliohenyea mtu kwa kufanya research, kuandika desertation, na kui-defend kwenye kamati yake. Hivyo basi mtu aliepewa Ph.D. honoris causa anastahili kuitwa Dr.

Dr. Kikwete, Dr. Mengi, late Dr. Nyerere wote wanastahili kupewa heshima hiyo. Wengi wanaopewa hizi Ph.D. honoris causa hawapendi kuitwa hadharani Dr. kama alivyokuwa mwalimu Nyerere. Lakini mara nyingi hii michango inayomfanya mtu apewe honorary degree ni mikubwa sana kuliko hata a simple written desertation ilioandikwa kwa miaka 3 au 4. (my humble opinion, as a holder of a non-honorary Ph.D.)

Nani mwengine ni Dr.?
Katika safu yangu, wa kwanza kuitwa Dr. ni marehemu babu yangu aliekuwa mganga mashuhuri sana wa kienyeji kijijini kwetu who never saw the inside of a formal classroom. Watu wote wengine wanaotoa michango au ushauri mzuri kama ya tiba mbadala (Dr. MziziMkavu), mapenzi/mahusiano (Dr. Love - hivi nani hapa JF anapaswa kupewa hii heshima?), n.k. Kwa maoni yangu mtu yeyote anaejihisi ana ujuzi zamilifu kwenye fani yake anaweza tu kujiita Dr. Udaktari uchwara utajulikana haraka sana.

Nawasilisha.
Mkuu Kifyatu Hongera sana kwa maneno yako ya Point, mimi hata wasiponiita Daktari sitoweza kukasirika ningelipenda pia waniite kwa jina langu kamili ninaitwa kwa jina hili (MziziMkavu Hauchimbwi Dawa) huwa ninafurahi mtu kuniita hilo jina langu mkuu kuliko hayo majina mengine ya kupachikwa na watu Daktari au Mganga wa kienyeji, jina langu kamili ndio hili tu MziziMkavu Hauchimbwi Dawa au unaweza kusema jina lingine Mchunguzi na Mtaalamu wa Dawa za mitishamba hilo jina pia langu siwezi kulikataa lakini hayo majina ya kizungu mie wapi na wapi jamani.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom