Mkataba aliishauvunja kitambo, sema tu tulimkaushiaKwani mkataba ndio unavyosema au maneno ya vijiweni
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkataba aliishauvunja kitambo, sema tu tulimkaushiaKwani mkataba ndio unavyosema au maneno ya vijiweni
Mna uwezo wa kuzitapika zile bilioni zake 20 za kwenye makaratasi?Na sisi tumeamua kumpinga Babra na tutamngoa siku si nyingi. Hata Mo naye siku zake zinahesabika.
Senzo ni next levelSenzo kaja kupiga hela tu hana cha maana vyura, kwa swala la Manara lilishakwisha, tulishatoka huko kwenye makelele sasa ni taaluma tu.
Tena hiyo migogoro yenyewe imezuka baada tu ya kutawazwa kuwa MAPINDUZI CUP CHAMPS.mkuu hujui kinachoendelea ndani ya simba ndo maana umekuja kumtetea babra, babra haelewani karibu na kila kiongoz ndani ya simba isipokua mwekezaji, try again na mpambe wao magori, katengeneza migogoro inayoua teamwork ilotupa ubingwa miaka 4 mfululizo.
migogoro ndani ya uongozi imewaathiri hadi wachezaji wetu kisaikolojia, jambo linalowakosesha umakini wawapo mchezoni, suluhu ya kinachoendelea simba ni kumuondoa babra/akalishwe kitako na kupewa darasa la kuwaheshimu viongozi wenzake.
Mwanaume mzima unashabikia majungu anayopigwa mwana Dada shupavu, acha majungu mtoto wa kiume tafuta hela.mkuu hujui kinachoendelea ndani ya simba ndo maana umekuja kumtetea babra, babra haelewani karibu na kila kiongoz ndani ya simba isipokua mwekezaji, try again na mpambe wao magori, katengeneza migogoro inayoua teamwork ilotupa ubingwa miaka 4 mfululizo.
migogoro ndani ya uongozi imewaathiri hadi wachezaji wetu kisaikolojia, jambo linalowakosesha umakini wawapo mchezoni, suluhu ya kinachoendelea simba ni kumuondoa babra/akalishwe kitako na kupewa darasa la kuwaheshimu viongozi wenzake.
Ndugu yenu Aliyewaita utopolo hakukosea.Pumba tupu,ukweli gani aliousema hadi achukiwe,brain wash imewafanya muamini kabisa simba inahujumiwa na si makosa ya kwenye usajili,aliyewaita mbu3 akukosea kabisa
Misimu minne yote ya makombe yaliyochukuliwa ulikuwa umejificha wapi? Una hela?Na sisi tumeamua kumpinga Babra na tutamngoa siku si nyingi. Hata Mo naye siku zake zinahesabika.
Simama nae na ukae nae pia,ni sawaNi wazi mwanadada huyu anapitia kipindi kigumu na si ajabu hakujua ugumu wa kazi kabla ya kukubali kufanya ya kondoo katikati ya kundi la mbwa mwitu.
Pengine angejua tabia na desturi za watu wa nchi hii wanaojiita watu wa mpira asingekubali kuajiriwa kufanya kazi anayoifanya.
Naamini yeye aliamini anakwenda kufanya kazi na sio vita. Anachokutana nacho sasa ni vita na sio kazi za mpira wa miguu.
Na kibaya zaidi vita hiyo anapigwa na wale wanaojifanya wamevaa ngozi ya kondoo ila ndani mbwa mwitu wanaowaza kumrarua na kula nyama yake.
Vita hii anayokutana nayo inatokana na chuki ya yeye kuamua kuwa mkweli na kuitetea taasisi iliyomwajiri na kumlipa mshahara. Kwangu huyu dada mwenye msimamo wa kukisimamia kile anachokimini na kukitete ndiocho kinachomtesa. Watesi wake wameamua kumtangazia vita na kuapa ama zake ama zao.
Wanatumia nguvu kubea mno kutaka kumdhoofisha ili tu watimize malengo yao na asiwepo wa kusema hili hapana.
Wapo tayari hata kushawishi wanachama na wapenzi wa Simba ili walaghaike na kuwa upande wao kwa nia ya malengo yao.
Kabla hujaja kunishawishi kutaka niungane na wewe itabidi kwanza uje na majibu ya maswali yafuatayo.
1. Kosa lake ni lipi?
2. Wapi amekiuka miiko ya kazi yake?
3. Kanuni ipi ya mbwa mwitu au ya Simba amevunja?
4. Kosa lake ni kusema ukweli na kufichua dhambi?
Kwa karne hii bado tunaeneza majungu na fitna ili tu kumfanya mtu ajione mnyonge kwa manufaa ya malengo ya giza?
Tumefika mahali mtu akiwa ni mtumishi anayefuata ueledi na kufuata taratibu za kazi basi huyo anakuwa adui?
Badala tuitumie elimu na utendaji mzuri wa kazi wa huyu dada kwa manufaa ya kulisogeza soka mbele tunamjengea majungu na kutaka aondeke ili tutimize majungu na janja janja.
Kwa mwenye mapenzi ya kweli na mpira wetu bila kujali itikadi ya klabu yake. Atasimama na Babra. Ila wenye kutaka njia za mkato na janja janja watapambana mpaka wahakikishe anaondoka ofisini.
Hatukatai kwamba kama binadamu na yeye ana mapungufu yake ila hayatoshi kuondoa yale mazuri anayolifanyia soka letu.
Babra anatakiwa kwa sasa kumtia moyo na kumuhakikishia wapenda soka wa ukweli na maendeleo ya kweli tuna macho na tunaona kila analofanya kwa klabu yake na soka kwa ujumla.
MIMI NIMEAMUA KUSIMAMA NA BABRA