blogger
JF-Expert Member
- Mar 13, 2012
- 12,112
- 15,060
Hivi mmelipwa mje mumsafishe eeh!!?Habarini!
Nampenda huyu Mama ana moyo mwema sana ni mkarimu, anamoyo wa kujali vile vile ni mchangamfu hata kwa mtu asiye mfahamu.
Katika sanaa ya Tanzania kainua vipaji vingi sana sote tunajua hilo ni mchapakazi mzuri, mpenda amani asiye na makuu na yeyote.
Wabaya wachache wanajaribu kumchafua lakini wapi, wameishia kujipakaza mavi yao wenyewe .Sifa zake na uaminifu wake unambeba ,unatengeneza njia hata kwenye visiki
Isingekuwa kwa Msaada wako Madam Ritta Kala Jeremiah na msechu tungewajulia wapi?
Kayumba, Jumanne Iddi Menina na Walter wangejikwamuaje? Hamisi na Meshack wangetoboaje?
Wakati wengine wanafanya matusi ,wewe endelea kufanya kazi mwisho wa siku sifa zako njema zinaenezwa kila pembe ya nchi.
Kila la heri Madam wetu mpendwa Ritta Paulsen.
Alipe hela za watu.