Madereva tuache tabia hizi

Madereva tuache tabia hizi

Wewe siyo dereva makini. Dereva makini anaendesha gari 5 akiwa barabarani. Ya kwake, ya mbele, nyuma, na kulia na kushoto.

Ni jukumu lako kumlinda wa mbele yako, tena hili halina mjadala. Yaani hata kama wa mbele anacheza zigzag, ni sharti umlinde usimgonge, kama unabisha gonga halafu traffic aje. Tena utoe sababu eti jamaa alikuwa anayumba? Traffic atakuambia hukuweka umbali unaotakiwa wa mita 3. Yaani, unatakiwa uone matairi ya gari ya mbele yanazunguka. Ukisogelea sana na usipoyaona matairi ya mwenzako ujue muda wowote unamgonga. Sijui udereva mnasomea wapi?

Huwa ninasikitika sana, lakini hakuna namna.

Kingine, hapa mtoa mada analalamikia mwendo wa 30KM. Kimsingi, huu mwendo haukatazwi na sheria. Sanasana, kama speed limit inasoma 50km/hr, ukitembea 30km siyo kosa. Kosa, ambalo utapewa karipio iwapo ukibainika, ni kutembea speed 20 wakati limit ni 50. Ila Kama hamna limit ukiwa 50 hakuna kosa.

Lakini pia Kuna speed limit za 20 na 30. Mfano, barabara ya kutoka Marangu Mtoni kwenda Rombo ina kona nyingi na miteremko. Speed limit sehemu kubwa ni 20 na 30. Sasa kuna madereva wengine wanataka ukiwa njia hii basi ukanyage 50 na 60 Jambo ambalo ni hatari. Nimeshuhudia huu usumbufu na mwingine anaovertake sehemu hatari.

Udereva siyo kujua kuendesha chombo Bali ni nidhamu, kujua na kutii sheria. Na hapa ndipo kuna wasumbua wengi. Hata Jana Singida ile ni ajali inatokana na wrong over taking.

Tujifunze utii
Mzee double lane kuna mambo ya ku keep distance??
We upo kulia mwenzio kushoto unaakaa mbali ili iweje?
 
Mzee double lane kuna mambo ya ku keep distance??
We upo kulia mwenzio kushoto unaakaa mbali ili iweje?

Kwani gari huwa inatembea kiubavu?


Hata kama sawa, lazima uweke distance kati ya gari yako na ya pembeni. Unawajibika kumlinda wa pembeni. Usivuke mstari.
Kama wewe huwa unaendesha gari, dah!
 
Kwani gari huwa inatembea kiubavu?

Distance keeping ni kati ya gari yako na ya mbele yako.

Kama wewe huwa unaendesha gari, dah!
Sasa mie ninezungumzia double lane za uelekeo mmoja we upo kulia mwenzio kushoto ghafla anahama kutoka huko alipo anakuja kwako bila kuangalia side mirror ili aweze kujua gari ya upande mwingine ipo umbali gani na spidi gani....

Sawa hapo unamteteaje chizi ka huyo..
 
Sasa mie ninezungumzia double lane za uelekeo mmoja we upo kulia mwenzio kushoto ghafla anahama kutoka huko alipo anakuja kwako bila kuangalia side mirror ili aweze kujua gari ya upande mwingine ipo umbali gani na spidi gani....

Sawa hapo unamteteaje chizi ka huyo..

Kwa vyovyote iwavyo ikotokea umemgonga nyuma wewe una makosa. Labda mpigane pasi ndipo kidogo itaweza kuleta ugumu kuamua. Ila kama kaingia ghafla halafu umegonga taa ya nyuma, bampa, nk ikiwezekana mlipe tu hapohapo kwa sababu traffic akija anaanza: kosa la kwanza: umeshindwa ku keep distance, kosa la pili: umeharibu gari ya mwezako: kosa la tatu: umehatarisha maisha: kosa la nne umeharibu gari yako. Hayo ndiyo makosa common kwenye kadhia hii. Hapo bado makosa kama kuharibu miundombinu, kujeruhi, kuua, nk.

Likikutokea hili ndipo utajua vyema
 
Kwa vyovyote iwavyo ikotokea umemgonga nyuma wewe una makosa. Labda mpigane pasi ndipo kidogo itaweza kuleta ugumu kuamua. Ila kama kaingia ghafla halafu umegonga taa ya nyuma, bampa, nk ikiwezekana mlipe tu hapohapo kwa sababu traffic akija anaanza: kosa la kwanza: umeshindwa ku keep distance, kosa la pili: umeharibu gari ya mwezako: kosa la tatu: umehatarisha maisha: kosa la nne umeharibu gari yako. Hayo ndiyo makosa common kwenye kadhia hii. Hapo bado makosa kama kuharibu miundombinu, kujeruhi, kuua, nk.

Likikutokea hili ndipo utajua vyema
Iwe kosa isiwe kosa haihalalishi uzembe wa kuhama lane bila kuangalia side mirrors unaeza gongwa na gari ambalo sio saizi yako ukafa vile vile usiwatetee hao wanofanya huo ujinga
 
Iwe kosa isiwe kosa haihalalishi uzembe wa kuhama lane bila kuangalia side mirrors unaeza gongwa na gari ambalo sio saizi yako ukafa vile vile usiwatetee hao wanofanya huo ujinga

Kufa ni sehemu ya maisha ya barabara. Ila sasa unadhani kati ya aliyekufa na wewe uliyegonga na kubaki hai ni nani ana tabu?

Kama wewe ni dereva, kuwa makini aisee. Kama unaandika vitu vya namna hii, ninahisi udereva wako hauko sawa kidogo.

Nilitaka kushare tu na wewe maana huwezi jua, tunaweza kukutana road bila kujuana yalafu yakatokea mazabe.

Udereva ni undugu ndiyo maana hata ukimpisha mwenzako sehemu korofi, mfanao ana mzigo anapanda mlima, ukipaki kumpisha anakushukuru.

Kwa hiyo ukiwa barabarani unakuwa na hisia za kuendesha gari tano kwa wakati mmoja. Huo ndiyo udereva.

Wakati wewe unajifunza, mwenzako kafuzu nk.

Ni hayo tu. Sina nia ya kubishana
 
Hapo namba mbili (2) naomba ufafanuzi kidogo:-

Mpo double road na wote wawili mpo kwenye speed moja, mmoja kulia na mwingine kushoto ni upande upi mnatakiwa mkae ili kuruhusu anaekuja ku overtake? Left or Right?

Kuna rule sijui kama ipo applied TZ inasema "keep left unless overtaking"
 
Kwa vyovyote iwavyo ikotokea umemgonga nyuma wewe una makosa. Labda mpigane pasi ndipo kidogo itaweza kuleta ugumu kuamua. Ila kama kaingia ghafla halafu umegonga taa ya nyuma, bampa, nk ikiwezekana mlipe tu hapohapo kwa sababu traffic akija anaanza: kosa la kwanza: umeshindwa ku keep distance, kosa la pili: umeharibu gari ya mwezako: kosa la tatu: umehatarisha maisha: kosa la nne umeharibu gari yako. Hayo ndiyo makosa common kwenye kadhia hii. Hapo bado makosa kama kuharibu miundombinu, kujeruhi, kuua, nk.

Likikutokea hili ndipo utajua vyema

Iwe kosa isiwe kosa haihalalishi uzembe wa kuhama lane bila kuangalia side mirrors unaeza gongwa na gari ambalo sio saizi yako ukafa vile vile usiwatetee hao wanofanya huo ujinga

Wakuu mimi navyoona wote mpo sahihi,
Nitasahihishwa kama nipo sahihi.
Katika traffic cases ya magari kugogwa au kugonga mara nyingi huwa wanaangalia ni gari gani limeumizwa mbele, ambalo linakua lina majeraha mbele ndilo linalokua limegonga lenzake bila kujalisha kosa kalifanya nani.
Ila hata hivyo hii tabia ya kujipachika kama vile mtu anaendesha bodaboda sio tabia nzuri, unaweza ukafanya hivyo kumbe mwenzako break zake za kupump alafu ila upande wako.
Pia nimeangalia udereva wa Dar kusema ukweli kukeep distance ni changamoto maana kidogo tu ukiacha ka safety distance atashangaa kabajaji kapo tayari mbele
 
Hapo namba mbili (2) naomba ufafanuzi kidogo:-

Mpo double road na wote wawili mpo kwenye speed moja, mmoja kulia na mwingine kushoto ni upande upi mnatakiwa mkae ili kuruhusu anaekuja ku overtake? Left or Right?

Kuna rule sijui kama ipo applied TZ inasema "keep left unless overtaking"
Mkuu kitaratibu kama unaenda slow unatakiwa utembee na line ya kushoto, utaona morogoro road kuna baadhi ya sehemu katikati ya chalinze- morogoro wameweka kabisa hiyo michepuo ili magari yanayoenda taratibu yasilazimishe yasiotaka kwenda taratibu kuenjoy maisha.
Lakini inapokuja kiuhalishia watu hawajali hili unakuta magari mawili side by side yanaenda slow kwenye double road, mwishoe hakuna gari nyuma yao linaloweza kuwavuka kwa njia ya kulia (kama utaratibu unavyosema) wala ya kushoto.
 
Wewe siyo dereva makini. Dereva makini anaendesha gari 5 akiwa barabarani. Ya kwake, ya mbele, nyuma, na kulia na kushoto.

Ni jukumu lako kumlinda wa mbele yako, tena hili halina mjadala. Yaani hata kama wa mbele anacheza zigzag, ni sharti umlinde usimgonge, kama unabisha gonga halafu traffic aje. Tena utoe sababu eti jamaa alikuwa anayumba? Traffic atakuambia hukuweka umbali unaotakiwa wa mita 3. Yaani, unatakiwa uone matairi ya gari ya mbele yanazunguka. Ukisogelea sana na usipoyaona matairi ya mwenzako ujue muda wowote unamgonga. Sijui udereva mnasomea wapi?

Huwa ninasikitika sana, lakini hakuna namna.

Kingine, hapa mtoa mada analalamikia mwendo wa 30KM. Kimsingi, huu mwendo haukatazwi na sheria. Sanasana, kama speed limit inasoma 50km/hr, ukitembea 30km siyo kosa. Kosa, ambalo utapewa karipio iwapo ukibainika, ni kutembea speed 20 wakati limit ni 50. Ila Kama hamna limit ukiwa 50 hakuna kosa.

Lakini pia Kuna speed limit za 20 na 30. Mfano, barabara ya kutoka Marangu Mtoni kwenda Rombo ina kona nyingi na miteremko. Speed limit sehemu kubwa ni 20 na 30. Sasa kuna madereva wengine wanataka ukiwa njia hii basi ukanyage 50 na 60 Jambo ambalo ni hatari. Nimeshuhudia huu usumbufu na mwingine anaovertake sehemu hatari.

Udereva siyo kujua kuendesha chombo Bali ni nidhamu, kujua na kutii sheria. Na hapa ndipo kuna wasumbua wengi. Hata Jana Singida ile ni ajali inatokana na wrong over taking.

Tujifunze utii
Ww nae ni mkuda
 
Kuna hawa wa bodaboda,

Huwa hawajui kusubiri.

Wanapenda kujichomeka katikati na kupita na side mirror zetu.

Hawa wako radhi chombo chake kitembee bila breki lakini honi iwepo.

Gari nyingi hasa Dar zina mikwaruzo ya kuchubuka rangi kisa ni hawa vijana.
Huwa natembea na mawe kwenye dashboard kwa ajili ya Hawa jamaa.
 
Kuna hawa wa bodaboda,

Huwa hawajui kusubiri.

Wanapenda kujichomeka katikati na kupita na side mirror zetu.

Hawa wako radhi chombo chake kitembee bila breki lakini honi iwepo.

Gari nyingi hasa Dar zina mikwaruzo ya kuchubuka rangi kisa ni hawa vijana.
washawahi pita na side mirror yako nini?
 
Kuna hawa wa bodaboda,

Huwa hawajui kusubiri.

Wanapenda kujichomeka katikati na kupita na side mirror zetu.

Hawa wako radhi chombo chake kitembee bila breki lakini honi iwepo.

Gari nyingi hasa Dar zina mikwaruzo ya kuchubuka rangi kisa ni hawa vijana.
Na nyie piteni katikati
 
Hizi tabia zingine tukubaliane tu ni ukudu;
  • kutanua kwenye foleni mpaka unakula barabara zote mpaka ya wale wanaoenda ulipotoka huu ni UKUDA na UBINAFSI, yani kwakua wewe uelekeo wako hauendi basi sote tusiende?
  • Kwenye makutano ya barabara unakuta mtu analazimisha kwenda mbele mpaka anazuia magari yanayotoka upande anapoelekea yasitoke kwa kukunja kulia na yanayotoka njia ya kushoto kwake yashinde kuingia barabarani na kwenda alipotoka.
Picha haioneshi vizuri, Ila hilo gari jekundu lilitumia zaidi ya dakika 10 kutoka barabarani. Yani kwa lugha rahisi halikufanikiwa kutoka mpaka pale sisi tuliporuhusiwa.
20201215_185258.jpg
 
Back
Top Bottom