Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Madereva wa Magari yanayofanya safari za Nachingwea, Ruangwa, Liwale, Mtwara na Masasi kutokea Stendi kuu ya Mabasi Mkoani Lindi wamegoma hii leo januari 8, 2025 kwa kile walichokieleza kuchoshwa na utitiri wa faini barabarani na kufungiwa leseni zao na Jeshi la polisi kupitia kitengo cha usalama barabarani
Hali hiyo inatajwa kuathiri shughuli za usafiri na usafirishaji hususani kwa abiria wanaoelekea kwenye maeneo hayo kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali huku wengi wao wakiwa ni wafanyabiashara na wangonjwa wanaolekea hospitali kupata huduma
Wakizungumza mbele ya mkuu wa wilaya ya Lindi Victoria Mwanziva aliyefika kusikiliza kero zao madereva hao wamesema biashara kwao inakuwa ngumu na wanashindwa kufikisha hesabu kwa wamiliki wa vyombo kutokana na kupigwa faini Zaidi ya tatu kwa siku na wakati mwingine faini wanaandikiwa bila hata makossa
Akizungumzia kuhusu faini hizo mkuu wa usalama barabarani wilaya ya Lindi amesema hakuna dereva ambaye anaonewa katika kuandika faini isipokuwa wengi wanavunja sheria za barabarani huku akiwataka kuhakikisha wanapakia level seat na kutembea mwendo unaohitajika kisheria
Aidha mkuu wa wilaya ya Lindi Victoria mwanziva amewataka madereva hao kurudi barabarani na kwamba changamoto hizo watakaa na kuzijadili baadae katika kikao na wao huku akiwaasa askari wa usalama barabarani kutanguliza hekima kwanza
Hata hivyo madereva hao bado wamegoma wakisema hawataingia mpaka leseni zao zitaporudishwa na kutatuliwa kero zao .
Madereva wa Magari yanayofanya safari za Nachingwea, Ruangwa, Liwale, Mtwara na Masasi kutokea Stendi kuu ya Mabasi Mkoani Lindi wamegoma hii leo januari 8, 2025 kwa kile walichokieleza kuchoshwa na utitiri wa faini barabarani na kufungiwa leseni zao na Jeshi la polisi kupitia kitengo cha usalama barabarani
Hali hiyo inatajwa kuathiri shughuli za usafiri na usafirishaji hususani kwa abiria wanaoelekea kwenye maeneo hayo kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali huku wengi wao wakiwa ni wafanyabiashara na wangonjwa wanaolekea hospitali kupata huduma
Wakizungumza mbele ya mkuu wa wilaya ya Lindi Victoria Mwanziva aliyefika kusikiliza kero zao madereva hao wamesema biashara kwao inakuwa ngumu na wanashindwa kufikisha hesabu kwa wamiliki wa vyombo kutokana na kupigwa faini Zaidi ya tatu kwa siku na wakati mwingine faini wanaandikiwa bila hata makossa
Aidha mkuu wa wilaya ya Lindi Victoria mwanziva amewataka madereva hao kurudi barabarani na kwamba changamoto hizo watakaa na kuzijadili baadae katika kikao na wao huku akiwaasa askari wa usalama barabarani kutanguliza hekima kwanza
Hata hivyo madereva hao bado wamegoma wakisema hawataingia mpaka leseni zao zitaporudishwa na kutatuliwa kero zao .