Madhara ya dhambi ya uzinzi

Madhara ya dhambi ya uzinzi

magumbugu

Senior Member
Joined
Sep 27, 2017
Posts
143
Reaction score
266
1. Huangamiza nafsi.
"Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa;Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake." (Mithali 6:32)

Mtu hufa kiroho, kama ilivyo dhambi yoyote ile humuondoa mtu katika uwepo wa Mungu, na pia huondoa uwepo wa Mungu
kwa mtu na hicho ndicho kifo cha kiroho.

2. Huondoa ufahamu wa mwanadamu.
"Uzinzi na divai na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu." (Hosea 4:11)
Mtu anakuwa hana uwezo wa kuwa na ufahamu wa mambo mema ya kumpendeza Mungu, maana anakuwa hawezi kulitafakari Neno la Mungu, kila
wakati anakuwa anatafakari uzinzi tu.

3. Huchafua hekalu la Roho Mtakatifu.
"Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe." (1Wakorintho 6:18)
a) Uzinzi unahusisha viungo vya mwili, hivyo dhambi ya uzinzi inahusisha mwili moja kwa moja na ambalo ni hekalu la Roho Mtakatifu, (1Wakorintho 6:19)
Na Mungu anasema atamuharibu anayeliharibu au kulichafua hekalu la Roho Mtakatifu, (1Wakorintho 3:17)
b) Pia mwili ni kiungo cha Kristo,
"Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!" (1Wakorintho 6:15)
Swali la kujiuliza ni hili, Kama miili yetu ni viungo vya Kristo, Je, Yesu Kristo atakubali kuuwa na kiungo kichafu? Jibu ni hapana bali atakiondoa na kukitupilia mbali hadi kitakaposafishwa, mtu asipoomba toba ni lazima ataangamia kabisa maana anasema
tawi lisilozaa atalikata na kulitupa katika moto, (Yohana 15:6)

4. Humuunganisha mtu na madhabahu, miungu na ibada za mtu aliyezini naye, ukoo, kabila, nk.
"Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.”
(1Wakorintho 6:16)

Inawezekana kwa macho ya kawaida mtu asione, bali kiroho anakuwa ameshahama katika uwepo wa Mungu na kuungamanishwa na miungu ya yule mtu aliyezini naye, maana tayari wanakuwa mwili mmoja.

Anakuwa hana uwezo wa kumwabudu Mungu wa kweli, hata akiwepo
ibadani anakuwa hawezi kuunganishwa na Mungu kiroho, maana anakuwa tayari ana ibada za kishetani.

Kwa ujumla dhambi ya uzinzi kama zilivyo dhambi nyingine zote humuondoa mtu katika uwepo wa Mungu.
Hivyo tunapaswa kuepuka sana dhambi hii pamoja na dhambi zote ili Mungu asituache, maana Mungu akituacha shetani anachukua nafasi na kuanza kutuendesha.

Omba toba, tubia dhambi zote pamoja na uovu wote, naye Mungu atakusamehe maana anasema atazisafisha dhambi zetu zote,
(Isaya 1:18)Mungu akubariki sana! Mungu atusaidie tukae kwenye kusudi lake🤝🙏
 
Dhambi ya uzinzi inahesabika pale mtu alipolala na mke wa mtu na sio vinginevyo. Ikimaanisha kuwa adhabu ilitolewa kwa mke aliyechepuka na kama angekamatwa na mwanamume huyo wangeuwawa wote wawili. Ila kwa mwanamume kutembea na binti hata kama ameoa sheria haiwi uzinzi hivyo ni kusema aliyefungwa ni mke aliyeolewa huyu hapaswi kuingiliwa kamwe na ukimwingilia ndipo Methali inakuita wewe ( mwanamume) mjinga usiye na akili kwa ni ni? Maana umekosa wanawake mpaka ukaenda kujitia unajisi kwenye shahawa za mwanamume mwenzako?. Inaendelea kusema.....
Mithali 6
33. Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; <br>Wala fedheha yake haitafutika.
34. Maana wivu ni ghadhabu ya mtu; <br>Wala hatahurumia siku ya kujilipiza kisasi.
35. Hatakubali ukombozi uwao wote; <br>Wala hatakuwa radhi, ujapomlipa vitu vingi.
Yaani hata kufirwa inakuwa haki yako ukiingilia mke wa mtu.

Ila kuhusiana na mwanamwali ukimuingilia ukadakwa waweza toa mahari akawa mkeo au ikiwa baba mzazi haridhii umuoe itatoa mahari kisha ataenda zake. Hii ni kibiblia kabisa
 
Kabla ya yote ningependa kujua uzinzi maana yake nini mtumishi? Maana naskia kuna uasherati na uzinzi
uzinzi ni pale unapofanya mapenzi kabla ya ndoa, uasherati ni pale unapofanya mapenzi nje ya ndoa yaani umeoa ndoa ya kanisani lakini unafanya mapenzi na mtu ambaye sio mkeo au mmeo
 
Dhambi ya uzinzi inahesabika pale mtu alipolala na mke wa mtu na sio vinginevyo. Ikimaanisha kuwa adhabu ilitolewa kwa mke aliyechepuka na kama angekamatwa na mwanamume huyo wangeuwawa wote wawili. Ila kwa mwanamume kutembea na binti hata kama ameoa sheria haiwi uzinzi hivyo ni kusema aliyefungwa ni mke aliyeolewa huyu hapaswi kuingiliwa kamwe na ukimwingilia ndipo Methali inakuita wewe ( mwanamume) mjinga usiye na akili kwa ni ni? Maana umekosa wanawake mpaka ukaenda kujitia unajisi kwenye shahawa za mwanamume mwenzako?. Inaendelea kusema.....
Mithali 6
33. Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; <br>Wala fedheha yake haitafutika.
34. Maana wivu ni ghadhabu ya mtu; <br>Wala hatahurumia siku ya kujilipiza kisasi.
35. Hatakubali ukombozi uwao wote; <br>Wala hatakuwa radhi, ujapomlipa vitu vingi.
Yaani hata kufirwa inakuwa haki yako ukiingilia mke wa mtu.

Ila kuhusiana na mwanamwali ukimuingilia ukadakwa waweza toa mahari akawa mkeo au ikiwa baba mzazi haridhii umuoe itatoa mahari kisha ataenda zake. Hii ni kibiblia kabisa
mtu wa Mungu acha kuupinga ukweli ili uhalalishe dhambi, tendo la ndoa ni kwa ajili ya wanandoa,
 
Dhambi ya uzinzi inahesabika pale mtu alipolala na mke wa mtu na sio vinginevyo. Ikimaanisha kuwa adhabu ilitolewa kwa mke aliyechepuka na kama angekamatwa na mwanamume huyo wangeuwawa wote wawili. Ila kwa mwanamume kutembea na binti hata kama ameoa sheria haiwi uzinzi hivyo ni kusema aliyefungwa ni mke aliyeolewa huyu hapaswi kuingiliwa kamwe na ukimwingilia ndipo Methali inakuita wewe ( mwanamume) mjinga usiye na akili kwa ni ni? Maana umekosa wanawake mpaka ukaenda kujitia unajisi kwenye shahawa za mwanamume mwenzako?. Inaendelea kusema.....
Mithali 6
33. Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; <br>Wala fedheha yake haitafutika.
34. Maana wivu ni ghadhabu ya mtu; <br>Wala hatahurumia siku ya kujilipiza kisasi.
35. Hatakubali ukombozi uwao wote; <br>Wala hatakuwa radhi, ujapomlipa vitu vingi.
Yaani hata kufirwa inakuwa haki yako ukiingilia mke wa mtu.

Ila kuhusiana na mwanamwali ukimuingilia ukadakwa waweza toa mahari akawa mkeo au ikiwa baba mzazi haridhii umuoe itatoa mahari kisha ataenda zake. Hii ni kibiblia kabisa
😳😳
 
yaani wanapewa watu(mchungaji/mhubiri) afu wasema haichukuliwi na mtu
sadaka haimunufaishi Mchungaji inakunufaisha ww mtoaji, ndo maana hta mchungaji haitumiii bali inatumika kwa ajili ya kueneza injili ili iwafikie watu wengi zaidi, hata ww ukienda kwa mganga ukatoa kuku unadhan hyo kuku ni kwa ajili ya mganga, ni kwa ajili yako
 
1. Huangamiza nafsi.
"Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa;Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake." (Mithali 6:32)

Mtu hufa kiroho, kama ilivyo dhambi yoyote ile humuondoa mtu katika uwepo wa Mungu, na pia huondoa uwepo wa Mungu
kwa mtu na hicho ndicho kifo cha kiroho.

2. Huondoa ufahamu wa mwanadamu.
"Uzinzi na divai na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu." (Hosea 4:11)
Mtu anakuwa hana uwezo wa kuwa na ufahamu wa mambo mema ya kumpendeza Mungu, maana anakuwa hawezi kulitafakari Neno la Mungu, kila
wakati anakuwa anatafakari uzinzi tu.

3. Huchafua hekalu la Roho Mtakatifu.
"Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe." (1Wakorintho 6:18)
a) Uzinzi unahusisha viungo vya mwili, hivyo dhambi ya uzinzi inahusisha mwili moja kwa moja na ambalo ni hekalu la Roho Mtakatifu, (1Wakorintho 6:19)
Na Mungu anasema atamuharibu anayeliharibu au kulichafua hekalu la Roho Mtakatifu, (1Wakorintho 3:17)
b) Pia mwili ni kiungo cha Kristo,
"Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!" (1Wakorintho 6:15)
Swali la kujiuliza ni hili, Kama miili yetu ni viungo vya Kristo, Je, Yesu Kristo atakubali kuuwa na kiungo kichafu? Jibu ni hapana bali atakiondoa na kukitupilia mbali hadi kitakaposafishwa, mtu asipoomba toba ni lazima ataangamia kabisa maana anasema
tawi lisilozaa atalikata na kulitupa katika moto, (Yohana 15:6)

4. Humuunganisha mtu na madhabahu, miungu na ibada za mtu aliyezini naye, ukoo, kabila, nk.
"Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.”
(1Wakorintho 6:16)

Inawezekana kwa macho ya kawaida mtu asione, bali kiroho anakuwa ameshahama katika uwepo wa Mungu na kuungamanishwa na miungu ya yule mtu aliyezini naye, maana tayari wanakuwa mwili mmoja.

Anakuwa hana uwezo wa kumwabudu Mungu wa kweli, hata akiwepo
ibadani anakuwa hawezi kuunganishwa na Mungu kiroho, maana anakuwa tayari ana ibada za kishetani.

Kwa ujumla dhambi ya uzinzi kama zilivyo dhambi nyingine zote humuondoa mtu katika uwepo wa Mungu.
Hivyo tunapaswa kuepuka sana dhambi hii pamoja na dhambi zote ili Mungu asituache, maana Mungu akituacha shetani anachukua nafasi na kuanza kutuendesha.

Omba toba, tubia dhambi zote pamoja na uovu wote, naye Mungu atakusamehe maana anasema atazisafisha dhambi zetu zote,
(Isaya 1:18)Mungu akubariki sana! Mungu atusaidie tukae kwenye kusudi lake🤝🙏
Kwa maana wote mmetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.

Mishahara wa dhambi ni Maruti
 
uzinzi ni pale unapofanya mapenzi kabla ya ndoa, uasherati ni pale unapofanya mapenzi nje ya ndoa yaani umeoa ndoa ya kanisani lakini unafanya mapenzi na mtu ambaye sio mkeo au mmeo
kama maana ndio hio basi uzinzi upo sana sanaa utaendelea kuwepo sanaa tena watumishi makanisani ndio wanauchochea maana wengi wao(sio wote) ni wazinzi hatari
...
kingine hata wewe,mimi na yule tunazini sana moyo soma Mathayo 5:27
Mmesikia usizini lakini mimi nawaambieni yeye amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini nae moyoni mwake
...
Mwenyezi MUNGU atusamehe sana rehema yake ituponye na hukumu iliyo mbele yetu AMEN
 
Back
Top Bottom