Madhara ya ongezeko la tozo la miamala katika jamii

Madhara ya ongezeko la tozo la miamala katika jamii

Jamii zetu zinaishi kwa kutegemeana, familia ndiyo safety net ukipata matatizo. Hatuna desturi ya kutemea ustawi wa jamii tukipata matatizo. Mama mdogo akiwa mgonjwa, familia itatoa msaada wa hali na mali.

Simu zimerahisisha mawasiliano. Leo hii uko Bukoba utatuma pesa ya MRI scan kwa ndugu aliye Dar , utatuma ada ya shule Arusha na hata mama akilalamika amechoka kula tembele atapata 10,000 ya kubadilisha kitoewo wewe ukiwa bado Bukoba.

Sasa kwa kila hela tutakayo tuma katika kusaidiana machungu ya maisha Mwigulu anakata kipande. Yale matumaini kidogo tuliyobaki nayo ya maisha nayo pia yanapigwa panga. Afadhali ya jana kuliko leo.
Tuliaa ww adui wa jpm..hapo n mwanzo tuu..kuna mengi yajayoo..najua moyoni mwako unamkumbuka jpm kwa uthabiti aliokuwa nao..ila huku jf unabwabwajaa tuu..pyu pyu pyuu kuhusu jpm..uzur hata ww utatuma helaa...kazi iendeleee..
 
Kitu cha ajabu wananchi hao hao wanapolalamikia ugumu wa kitu serikali inakua haina solution ila linapokuja swala la kukandamiza wananchi serikali fasta inareact,miaka sasa tunalalamikia makampuni ya simu kuibia watu,serikali ipo kimya ila kwenye hii kodi sababu anayeumia ni maskini hata mwezi haijapita tayari ishaanza kuumiza watu!
 
Kodi gani unayolipa wewe? Ukienda dukani hudai risiti na ukiuza hutoi risiti ndio maana unalia Lia hovyo humu..lipa kodi Nyerere alitumia hadi bakora kwa watu kama nyie Ili mlipe kodi

Nyerere alipunguza hadi mshahara wake.

Sisi wanapeana magari ya mamilioni, majumba ya mabilioni, wao, wabunge, mawaziri, na vigogo wengine kodi hawa lipi. Wanapanga kujenga masanamu.

CAG kuripoti wizi wao kila leo na hakuna hatua zinazochukuliwa.

Hiki kimeumana.

Kama wewe ni wao au mufaika muda wako wa kulipa kodi stahiki au kuwajibishwa umewadia.
 
MAENDELEO binafsi hayapatikani bila ya kuufunga mkanda.....

MAENDELEO ya nchi hayapatikani bila ya KUIFUNGA MIKANDA.....

*****************

Mkuu wangu leo unasema AFADHALI YA JANA ?!! 😲😲

Daaah binadamu sisi....Kutwa ulikuwa unasema tuko "jehanamu" na KUMSHAMBULIA hayati JPM....leo hii JANA ni bora ?!!! Ha ha ha ha

#KaziIendelee
 
Back
Top Bottom