kipindupindu
JF-Expert Member
- Dec 16, 2010
- 1,053
- 170
Wakuu habari za usiku.kwa mara ya kwanza leo hii nimeamua kuongozana na mwenzi wangu na mke wangu mpendwa ili nikajionee sehemu anayonunulia vi-top,skin jeans,mapande manane na vimin skirts vya mtumba. Si mnajua vimwana wa kisasa wanajipendezesha kutoka kwenye viduka vidogo vya mitumba al-maarufu 'madocs'
Kwenye kiduka nilichoingia nimekutana na pazia linalogawa kachumba haka kadogo ktk sehemu mbili. Sehemu ya ndani kuna kioo kikubwa cha kujitazama, hapa ndipo wenzi wetu wa kike husaula na kubaki na nguo ya ndani (chupi na sidiria) ili kujaribisha nguo wanazotaka kununua.
Cha kushangaza na kushtusha utakuta mteja anabadilisha nguo kadhaa huku jamaa la kiume au kijana rijali(muuzaji) akimtazama miguu na kilichowatenganisha ni pazia ambalo upepo wa kaskazi ukivuma laweza kupepea na kuondoa usiri uliopo.
Yaani leo nimefikiria mengi kwa sababu mke wangu hakuonyesha kuwa na wasiwasi au uwoga wowote kwa kaka muuzaji ambaye ni brazaman ile mbaya. Yaani anamuamini kama mgonjwa wa kike anavyomuheshimu daktari wa kiume.
Nimejionea mengi ya kutilia shaka lakini kwa leo niishie hapa ili niwaachie wadada na wakaka wa jamvi hili tujadili jambo hili.
hivi ni kweli kinadada mnatoka salama kwenye haya madocs bila kunanihii?
Kwenye kiduka nilichoingia nimekutana na pazia linalogawa kachumba haka kadogo ktk sehemu mbili. Sehemu ya ndani kuna kioo kikubwa cha kujitazama, hapa ndipo wenzi wetu wa kike husaula na kubaki na nguo ya ndani (chupi na sidiria) ili kujaribisha nguo wanazotaka kununua.
Cha kushangaza na kushtusha utakuta mteja anabadilisha nguo kadhaa huku jamaa la kiume au kijana rijali(muuzaji) akimtazama miguu na kilichowatenganisha ni pazia ambalo upepo wa kaskazi ukivuma laweza kupepea na kuondoa usiri uliopo.
Yaani leo nimefikiria mengi kwa sababu mke wangu hakuonyesha kuwa na wasiwasi au uwoga wowote kwa kaka muuzaji ambaye ni brazaman ile mbaya. Yaani anamuamini kama mgonjwa wa kike anavyomuheshimu daktari wa kiume.
Nimejionea mengi ya kutilia shaka lakini kwa leo niishie hapa ili niwaachie wadada na wakaka wa jamvi hili tujadili jambo hili.
hivi ni kweli kinadada mnatoka salama kwenye haya madocs bila kunanihii?