Madogo mnatudharua Mabroo zenu kisa tumeshindwa karibu Kila kitu

Madogo mnatudharua Mabroo zenu kisa tumeshindwa karibu Kila kitu

Umri umekwenda mkuu.
Ni vyema ukaachia ngazi ili vijana wako tuifanye kazi vyema.
Hili ni ombi tu mkuu

Tatizo MNATUDHARUA.
Kununua tuu kiwanja dharau elfu, kisa kaka zenu miaka nenda rudi hatumiliki hata kiwanja ukubwa wa eneo la choo
 
Tatizo MNATUDHARUA.
Kununua tuu kiwanja dharau elfu, kisa kaka zenu miaka nenda rudi hatumiliki hata kiwanja ukubwa wa eneo la choo
Ulikuwa wapi kununua kiwanja enzi za ujana wako.
Eti leo unakuja kunionea gere mimi kununua kiwanja katika umri ambao wewe hukuweza.

Waige wazee wenzako waliokubali kwamba wakati wao umekwisha.

Hizi ni zama za wanao na si wewe.
Waandae wanao vizuri ili wawe washindani wetu bora zaidi.
Hiyo ndio option iliyobakia upande wako ambayo ni salama
 
Ulikuwa wapi kununua kiwanja enzi za ujana wako.
Eti leo unakuja kunionea gere mimi kununua kiwanja katika umri ambao wewe hukuweza.

Waige wazee wenzako waliokubali kwamba wakati wao umekwisha.

Hizi ni zama za wanao na si wewe.
Waandae wanao vizuri ili wawe washindani wetu bora zaidi.
Hiyo ndio option iliyobakia upande wako ambayo ni salama

Dharau hizi.
Kwa hiyo mmegeuka washauri wa kaka zenu
 
Dharau hizi.
Kwa hiyo mmegeuka washauri wa kaka zenu
Hapo ndipo mnapokosea wazee.
Kuamini kwamba kijana hana nafasi ya kukushauri na kama akikushauri anakuwa amekudharau.

Wazee walioutumia ujana wao vizuri, Wanatambua mchango wetu kwao sisi vijana na wanatutumia kama washauri wao.

Kipindi wenzako kina bakhresa wanafanya maendeleo nyinyi mlikuwa mnawaza ngono tu mkiamini ni ujanja.
 
Mpo Pouwa.

Haya bhana! Yote Kheri. Mungu ndio anajua. Dharau mlizonionyeshea hakika kama kungekuwa na uchawi ningewaloga wote Mbuzi nyie, watoto niliowaona mkizaliwa, tukawakuza wenyewe, leo ninyi ndio wakuturushia mavi usoni? Kweli! kweli?

Kisa mmeshaanza kuzivua Sketi za Wadada sio? Au nini? Au niaje? Ni kwa vile vipesa vyenu mshenzi vya Udalali na kubeti ndio vinawapa kiburi? Afu dogo Mcheza amapiano unajua maneno yako bado hayajapotea akilini mwangu. Ni hiko kisabufa cha laki unusu ndio kilikufanya uropoke kwa jeuri kama tajiri anayedhamini wapiganaji wa Alshabab.

Kujua kuoga na kuvaa ndio sababu ya kutudharau siye kaka zenu tunaovaa marapurapu. Majukumu yetu ni makubwa madogo na mengi ajabu. Fikiri na fikiria familia zetu zatutegemea, waza na wazua jinsi ambavyo tunatakiwa tuwajengee ninyi ramani ili ninyi mpite kirahisi. Lakini kwa vile macho yenu machoni hayaoni mnatuona kama majinga na mbumbumbu!

Imefikia hatua mpaka mnatongoza Shemeji zenu ambao ni Wake Wetu. Hivi mnaakili ninyi watoto? Nitaua mtu Walahi! Nitapasua mtu mimi!
Kosa letu ni kuwakaribisha kwenye makazi yetu? Kosa letu ni lipi?

Vipafyumu vyenu vya elfu tano ndio vinawatia uchakaramu haramu kujitongozesha na kuwarubuni Wake zetu? Acheni dharau madogo. Jiheshiimuni tuwaheshimu.

Ni kweli kaka zenu maisha bado yanawezakuwa yanatusumbua. Huenda hata makazi kwetu ni shida. Huenda hata kula yetu bado niyakurushiana manati. Huenda bado tunapiga Wangwasuma kama Suma Jeikeitii mbele tembea nyuma geuka. Maisha yanatupeleka mperampera kama Gwaride la Hamas.

Lakini eleweni, Yote Mungu ndiye Muweza yote, na jitihada haizidi Kudura. Kufanikiwa kwenu msituone sisi mazombi na wazembe.

Nami nawaambia lililozama Magharibi ndilo hilohilo lilichomozea Mashariki. Na kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho. Kuweni na akiba ya maneno. Msitudharau sisi wala kumdharau yeyote kwa hali aliyonayo.

Jana mmenitukana mno. Labda mlisema mlikuwa mnanichana Ukweli. Kwa ukweli upi? Ninyi mnaujua ukweli ninyi? Si ninawauliza! Kama mngeujua ukweli basi msingenidharau.

Kisa mmefika Chuo kikuu? Au kisa nini? Au niaje?
Hamkuujua ukweli ndio maana mnatuona tuliowatangulia Wapuuzi na Watu tuliofeli. Hamtaki kutusalimia. Na tukiwasalimia mnasema tunataka kuwapiga kibomu, kuwakwara Pesa. Mnatuona kaka zenu washidashida.

Maneno yangu ni yaleyale, kuweni wapole na wanyenyekevu kabla maisha hayajawafundisha kwa njia ngumu.

Haya ngoja tuone mwisho wa mambo haya ni upi. Kama mlidhani tutashindwa kama mtuonavyo subirini mtaona. Siku zote mshindi hutokea mwishoni. Na mshindi ndiye atakayeandika historian.
Na mshindi ni yule atakayekuwa mkweli, muadilifu na mwenye haki na upendo.

Hasa wewe dogo mvaa vipensi na uliyepaka Bleach, kuwa Makini.

Alafu na wewe dogo mlokole, sijui msabato, sijui dini yako gani. Kuniona nimefeli maisha kwa sababu labda unadhani nilikuwa mhuni, au mjinga, au kuona kama nilimuasi Mungu basi nakuambia unakosea sana dogo.
Kutuona Kaka zenu tulioshindwa maisha kama waasi mbele za Mungu ni kutudharau. Mtajionea wenyewe, subirini Mkue mtayaona wenyewe.

Mimi acha nipumzike, kaugali kameshaiva.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Bado hujasema..!! Na utasema tu..!! yaani hapo bado..!! yaani mpaka usemeee...!!

Yaani siyo madogo tu, hata wenye rika sawa na wewe au waliokuzidi, kama wamekuzidi kila kitu utapitia hicho hicho kwao..!!

Kwenye familia tu kama umezidiwa hela na mdogo wako wa saba, maamuzi ya kifamilia atafanya yeye. Na kama kwenye kikao cha familia hayupo mtamsubiri..!! This is nature..!!
 
Bado hujasema..!! Na utasema tu..!! yaani hapo bado..!! yaani mpaka usemeee...!!

Yaani siyo madogo tu, hata wenye rika sawa na wewe au waliokuzidi, kama wamekuzidi kila kitu utapitia hicho hicho kwao..!!

Kwenye familia tu kama umezidiwa hela na mdogo wako wa saba, maamuzi ya kifamilia atafanya yeye. Na kama kwenye kikao cha familia hayupo mtamsubiri..!! This is nature..!!

Nitapiga mtu hapa
 
Back
Top Bottom