jacklinekahu
Member
- Jun 15, 2015
- 7
- 1
Habari,
Mie ni mdaiwa wa bodi ya mkopo nilikua naomba kupata maelekezo kuhusu upigaji upya wa mahesabu wa tunaodaiwa na Loan Board, kiukweli nilipata shida sana ambapo siku ya alhamis nilifika katika ofisi za Bodi ya Mkopo nia ni kulipa deni langu ambalo lilikua limebakia kiasi cha sh milioni moja cha ajabu niliambiwa inabidi nipigiwe mahesabu upya na kujikuta nadaiwa kiasi cha sh milioni sita kiukweli niliishiwa nguvu na nilivyouliza nikaambiwa ni waraka umetoka na wao wanautekeleza.
Hoja yangu ni kwamba kwanini wasitujulishe kupitia vyombo vya habari ama kupitia waajiri wetu maana mwajiri wangu anajua nadaiwa kiasi cha sh milioni moja ndo outstanding balance, pili je hili deni kwa wataalam wa sharia si inabidi iwaguse wale ambao hawajaanza kukatwa sio sie ambao tumeshakatwa kwa miaka minne mpaka sasa?
Na tatu je ambao walishamaliza kulipa je nao watapigiwa mahesabu upya?
Mie ni mdaiwa wa bodi ya mkopo nilikua naomba kupata maelekezo kuhusu upigaji upya wa mahesabu wa tunaodaiwa na Loan Board, kiukweli nilipata shida sana ambapo siku ya alhamis nilifika katika ofisi za Bodi ya Mkopo nia ni kulipa deni langu ambalo lilikua limebakia kiasi cha sh milioni moja cha ajabu niliambiwa inabidi nipigiwe mahesabu upya na kujikuta nadaiwa kiasi cha sh milioni sita kiukweli niliishiwa nguvu na nilivyouliza nikaambiwa ni waraka umetoka na wao wanautekeleza.
Hoja yangu ni kwamba kwanini wasitujulishe kupitia vyombo vya habari ama kupitia waajiri wetu maana mwajiri wangu anajua nadaiwa kiasi cha sh milioni moja ndo outstanding balance, pili je hili deni kwa wataalam wa sharia si inabidi iwaguse wale ambao hawajaanza kukatwa sio sie ambao tumeshakatwa kwa miaka minne mpaka sasa?
Na tatu je ambao walishamaliza kulipa je nao watapigiwa mahesabu upya?