Maelezo ya kina kuhusu Uber. Usafiri salama na wa bei ya chini kwa mtanzania

Maelezo ya kina kuhusu Uber. Usafiri salama na wa bei ya chini kwa mtanzania

Nimeona watu wengi sana wakiiendea biashara hii ya UBER, magar haya yameongezeka sana hapa Dar es Salaam japo sio biashara inayohitaji mtaji mdogo...Naomba tujadili biashara hii pamoja na faida na changamoto zake
 
Achana na Uber fungua banda la chips utauza kuliko hao Uber
 
Achana na Uber fungua banda la chips utauza kuliko hao Uber
Unaongea kwakua una uhakikaa ama nin?ushawai fanya biashara ya chips?mim nishawai fanya hyo biashara,tena sio chips ni glocery kabsaa,so hunambii kitu kuhusu hyo ishu,ni pasua kichwa..management yake ni ishu.na ku master management labda umweke mama ako auze ndo utapiga hela au ukae mwenyew..uber ni nafuu sana ila pia ili upige hela lazma gar iwe yako na usimame mwenyew au umweke nduguyo...biashara za daslam management tu ndo ishu,ukipatia hapo bas umetusua
 
Kwanini mkuu
Uber japo utapata senti lakin si endelevu fikiria unamtoa mtu mf. Makumbusho unampeleka Kerege (Bagamoyo) unapata 12,000/= (hapo unakuta mteja ana ofa toka Uber ya 7,000/= so unalipwa cash na abiria 5,000/=) bado 25% ya Uber, Airtime, bundle, mafuta ya gari. Funny enough ukishamshusha Kerege unarudi tupu. Uber ni pasua maini
 
Kwenu wana jukwaa,poleni kwa uchovu wa siku ya leo.
Nimekaa nikafikiria biashara ya kfanya kwa ajili ya kujikwamua Guu ugumu nimeoa ninunue gari mbili aina ya IST nizifanye uber, faida itakayo patikana niongeze hadi zifikie tano au nne kama mungu akipenda,tafadhali waungwana naomba mchango wa kiushauri je biashara hii ni sahihi na italipa kweli kwao kuwekeza kwa gari hizo mbili?shukrni kwenu kwao michango yenu.
 
Ni biashara nzuri kwa sasa maana watu wanaizoea haraka kutokana na kua nafuu. Kumbuka tu kununua gari nzima ili kuepuka gharama za matengenezo ya mara kwa mara.
 
Ni biashara nzuri kwa sasa maana watu wanaizoea haraka kutokana na kua nafuu. Kumbuka tu kununua gari nzima ili kuepuka gharama za matengenezo ya mara kwa mara.
Ndio lengo langu,mungu bariki nipate ist mbili kwa mtaji nilio nao
 
Je gharama ya safari inawezakutegemea umbali dereva wa UBER alipo anapokufuata?
Ahsante


Uber ni nini?
Uber ni application inayokuwezesha kupata usafiri wa bei ya chini na salama katika sehemu nyingi za mkoa wa Dar-es-Salaam, kwa kupitia simu yako ya mkononi. Usafiri huu ni wa kutumia magari madogo yanayoweza kubeba kuanzia mtu mmoja hadi watu wanne.

Kujisajili na Uber
Nenda playstore, search 'Uber' utaiona ina icon nyeusi, download kisha ifungue.
Fanya usajili kwa kutumia namba yako ya simu, email na pia utachagua neno la siri.

Kupata punguzo la Tsh6200 katika trip yako ya kwanza
  • Nenda Menu kwa kubonyeza mistari mitatu iliyoko juu kushoto,Kisha bonyezaPayments,kisha bonyeza Add promo code , andika ubertz5
  • Utaona maandishi ya kijani yakionyesha kwamba utapata punguzo la tsh6200 katika trip yako ya kwanza.
  • Nitatoa mfano, safari yako ya kwanza ni kutoka posta hadi magomeni,na gharama yake ni shilingi 7200,basi utalipa sh1000 tu kutokana na hilo punguzo,lakini katika safari ya pili utalipa nauli kamili.

Zingatia

Unaweza kujisajili mara moja tu kwa kutumia hiyo promotion code, ukirudia kujisajili kwa namba nyingine kama baadhi ya watu wanavyopotosha mitandaoni, akaunti yako ya uber itafungiwa na hutaweza tena kutumia huduma za uber

Jinsi ya kutumia Uber kuita usafiri.
  • Fungua app ya Uber, hakikisha umewasha GPS, itakuletea maandishi 'where to'.Hapo utajaza unapotaka kwenda,mfano 'Magomeni Mapipa'.
  • Itakuonyesha kiasi cha nauli inayokadiriwa, na utabonyeza 'Request uberX'
  • Hapo hapo,itakuonyesha jina na namba ya gari la dereva atakayekufata hapo hapo ulipo, na ndani ya dk5 atakuwa kashafika.
Malipo ya usafiri
  • Ukifika 'destination' yako dereva atabonyeza 'Stop trip' kwenye application iliyoko kwenye simu yake, na hapo hapo itaonyesha nauli kwenye simu yako na kwenye simu ya dereva
  • Unaweza kulipa kwa Cash(Taslimu) au kwa kutuma Kadi ya benki
Umuhimu wa kutumia Uber
  • Ni gharama nafuu zaidi ukilinganisha na taxi za kawaida, kwa sababu bei inahesabiwa na mashine yenyewe kulingana na umbali wa sehemu unayoenda, na sio derevaa kujipangia bei kubwa
  • Ni salama zaidi, hasahasa usiku, kwasababu dereva wa uber anakuwa amesajiliwa na endapo itatokea tatizo lolote mfano kusahau kitu kwenye gari, dereva anaweza kupatikana kwa haraka
  • Inakusaidia kuokoa muda; mfano upo sehemu ambapo hamna taxi,bajaji wala bodaboda, unaweza kuita usafiri na ukakufata hapohapo kwa kutumia app hii.
UPDATE 1:
Uber inakuletea usafiri wa bajaji pia, ambao ni bei rahisi zaidi, sasa unaweza kuchagua kati ya UberX(taxi) na UberPoa(bajaji) kutokana na uwezo wako. UberPOA inapatikana maeneo ya Mwenge, Sinza, Kijitonyama, Mikocheni A, Mwananyamala, Kinondoni, Namanga, Msasani, Oysterbay, Masaki & Kigamboni ingawa huduma hii inasambaa maeneo mengi katika siku za baadaye.

UPDATE 2:
Kwa wale waliokwisha kutumia ofa yao ya kwanza(first ride), usiache kutumia Uber, endelea na unaweza ukapata punguzo la 25% au 50% kwa safari zako 4 mara kwa mara
 
Je gharama ya safari inawezakutegemea umbali dereva wa UBER alipo anapokufuata?
Ahsante
Kwa uzoefu wangu huo umbali wa dereve kukufuata hauhusiki. Ila muda wa kukusbiri ukiwa mahali unaulipia.

Pia ogopa kupanda uber kwenye njia au muda ambao una foleni kubwa. Utajuta mpaka kufa. Kuna fee ya muda wa safari.

Rafiki yangu alijichanganya akalipa 98, 000/= toka mbagala mpaka kimara baruti.
 
OFA! SAFIRI BURE SASA. Download app ya uber, ingiza promotion code ya ubertz5 ili katika safari yako ya kwanza upate punguzo la tsh 6200
We jamaa promo code yako iko expired vipi ubarozi ushaupoteza mkuu.
 
OFA! SAFIRI BURE SASA. Download app ya uber, ingiza promotion code ya ubertz05 ili katika safari yako ya kwanza upate punguzo la tsh 6200
 
OFA! SAFIRI BURE SASA. Download app ya uber, ingiza promotion code ya ubertz05 ili katika safari yako ya kwanza upate punguzo la tsh 6200
Ila mbona account yangu kila mala inakuwa deactivated kwanii hili
 
Ila mbona account yangu kila mala inakuwa deactivated kwanii hili
Pole sana mkuu, tafadhari fika mlimani city kuna kituo cha huduma kwa wateja wa Uber, utapata suluhisho la tatizo lako
 
Pole sana mkuu, tafadhari fika mlimani city kuna kituo cha huduma kwa wateja wa Uber, utapata suluhisho la tatizo lako
Nimecheck na uber support wamenirekebishia wako fasta sana jamaa kitu ambacho hawataki ni kutumia account zaidi ya moja ya uber kwenye device moja ila nimewapa sababu wameifungua.
 
OFA! SAFIRI BURE SASA. Download app ya uber, ingiza promotion code ya ubertz05 ili katika safari yako ya kwanza upate punguzo la tsh 6200
 
Back
Top Bottom