Maelfu wapona corona kwa siku moja Italia

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Habari njema kutoka Italia zinaarifu kuwa nchi hiyo kwa mara ya kwanza imerekodi idadi kubwa ya watu waliopona virusi vya corona katika kipindi cha masaa ishirini na nne.

Kulingana na mkuu wa idara ya kukabiliana na majanga Angelo Borelli, watu 2,563 wamethibitishwa kupona virusi vya corona katika kipindi cha siku moja. Idadi ya walioambukizwa virusi hivyo pia imepungua pakubwa.

Kati ya Alhamis na Ijumaa ni visa 3,786 vya maambukizi vilivyoripotiwa. Kulingana na Taasisi ya Kitaifa ya Afya mjini Roma, karibu wahudumu wa afya 17,000 wameambukizwa virusi hivyo sasa huku idadi kubwa wakiambukizwa wanapokuwa kazini.

DW Swahili
 
wapone fasta waje kututibu sisi huku africa.sisi tupo tupo tu tumekaa kaa tu.tunawangoja wao wapone kwanza kisha waje na huku kutuponesha.
Hata kama watachota dhahabu ama rasilimali zozote sisi tupo tyr.
Akili zetu africa zinafanya kazi kwa ufasaha kwenye chuki na roho mbaya na ulafi wa madaraka ila kwenye majanga akili azifanyi kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
 
"Wagonjwa wote waliyobaki (131) hali zao ni nzuri isipokuwa Wagonjwa 4 wanapatiwa matibabu ya Wagonjwa mahututi kutokana na kusumbuliwa na matatizo mengine ya kiafya."
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…