Maelfu watii amri ya kuondoka Gaza huku Israel ikiandaa wanajeshi 300,000 kuanza fagia fagia

Vita sio game km la Man U vs Man City....

Unachopanga sio ndio kitakachotokea, ....

Naona wachambuzi uchwara wengi wakihemka na tabiri zao za kimhemko...

Only the dead saw the end of the war.

Tuandae popcorn za kutosha, kwani hili ni movie ni ndefu , ambapo jasho na damu nyingi itamwagika, only the battle hardened might prevail.
 
Vita kati ya Israel na majirani zake ngumu kuimaliza sababu anapigana na watu wasio na jezi wala alama
 
Katika ujinga wa karne uliofanyika ni HAMAS kuivamia Israel na kuwaua raia namna ile na kuwateka. Sijui ni nani aliwaaminisha ama aliwahamasisha kufanya such terror attack.

Ninajua kabisa, si rahisi kuubeba uchungu ama hisia za mtu aliyeumizwa kumoyo, Israel ni kweli wanalaumiwa sana sana na kulaaniwa kwa mashambulizi haya wwnayoyafanya.

Lakini ninasoma na kusikiliza kwa tahadhari sana wale wanaoipigia kelele Israel, sijasikia popote wakilaani kilichofanywa na HAMAS. Hata kama Israel anaikalia kwa mabavu ardhi ya wapalestina, lakini jibu la hayo ndo kuwavamia raia hususan kuchinja watoto, kuua wazee, kuwabaka na kuwaua wanawake? Israel ina haki ya kujilinda na kuwadhoofisha magaidi wa namna hiyo.

Kiukweli sipendi vita lakini kama opponet anachagua vita kama suluhisho basi apewe haki yake aridhike.

Bado naisihi Israel iwajali watoto na majeruhi wa vita
 
SEMA Hamas walijuwa kabisa matokeo ya Wanacho kifanya
 
Kwa hiyo ulitaka akili kitu ambacho hajafanya? hata Marekani alisema ya kuwa hakuna ushahidi wowote unao ihusisha Iran na ambush hiyo na wala ilikuwa haijui chochote kuhusu ambush hiyo hata wao iliwashutua.

Shambulizi hilo limesababishwa na udhaifu wa vitengo vya usalama na integensia ya Israel msilete visingizio.

Hata kama angekuwa amehusika wange mfanya nn? Yakwamba Israel ingeishambulia Iran[emoji2][emoji2][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] ww nakuona unaleta mizaa na utani aisee.

Hii Israel ambayo ina pambana na Hamas ndani ya wiki moja tu imesha anza kuomba misaada ya silaha kutoka Marekani na sasa hivi nasikia Marekani imetuma kikosi cha delta kuja kuisaidia kwenye mashambulizi ya ardhini.

Israel hii ambayo imekusanya wanajeshi laki 3 na nusu kwenda kupambana na wanamgambo wasio zidi 20,000 wasio miliki silaha yeyote zaidi ya bunduki na viroketi vya kutengeneza kienyeji ndo aje kupambana na jeshi la Iran lenye kila aina ya silaha za kimamboleo?

Kama ni kushiriki vita sio razima apeleke wanajeshi anaweza kuwa anatoa silaha kwa hamas kama anavyo fanya Marekani nchi Ukraine ,na hata asipo saidia hiyo ni juu yake kwa sababu sio razima ashiriki katika kila mzozo hali ya kuwa hana maslahi nao.
 
Kwahiyo siku za ibada wanajeshi wanaacha kilinda nchi badala yake wanaenda kwenye ibada, kweli hilo ni jeshi la kushangaza [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji2][emoji2].

Kumbe hata Tz siku za pasaka na Iddi unaweza vamia nchi na kufanya unavyo taka kwasababu vitengo vya usalama vitakuwa kwenye ibada?
 
Nadhani mwisho wa Hamas umefika, wamechekewa muda mrefu wakaota mapembe.
Mkuu vita sio kucheza ngoma ww subiri Israel haanze uvamizi wa ardhini ndo utanielewa sasa hivi huwezi nielewa kwa sababu ya mihemko.
 
Hii vita ukisoma kwenye mitandao unaweza kushangilia na kushabikia Ila ukikaa ukaanza kufatilia kipitia al Jazeera utatokwa na machozi tu
Kimsingi ni kosa kubwa sana kushangilia vita sehemu yoyote. Binafsi katika maombi yangu kwa Mungu kila nikipiga magoti ni kuombea amani ya nchi yetu. Hali ni mbaya sana huko hata hapo Kongo tu.

Sijui tumekuwa na kizazi cha namna gani nchi hii. Anzia ile vita ya Urusi na Ukraine, kulikuwa na mashabiki wengi sana aasa wamehamia hiyo ya Palestina na Israel mbaya hii imekaa kidini. Waislam na Wakristo kila.mmoja anavutia uoande wake. Eeehh Mungu saidia hiki kizazi chetu. Hali ni mbaya sana.
 
Haaaa watu wanadhani vita ni sawa nakucheza ngoma[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Vita sio lele mama na ndio maana mpaka sasa Israel haijaingia gaza bado inajipanga vizuri.
Tatizo watu akiona mavifaru,magari makubwa wanaogopa bila ya kujua kuwa mbele ya ant_tank ni sawa na kibox kinacho tembea.
 
Nimesoma hoja zako hakuna sehemu umesema walichokifanya Hamas kuua raia si sahihi ila umesema watu wa Israel waliuwawa sababu ya udhaifu wa jeshi lao. Inshort "You stand with HAMAS".

Dunia inahitaji tishio la uvamizi kutoka nje ili tuwe na common enemy wa kutuunganisha.

Pakitokea tishio la Allien kuchukua ardhi ya dunia haya maigizo ya "i stand with Israel", "I stand with hammas" sijui russia ukraine katika kushabikia kuuana wenyewe kwa wenyewe yatapungua.
 
Hamasi ana jeshi hawafiki watu 3000 Israel kashindwa kumpiga mpaa aje asaidiwe na majeshi ya marekani na uingereza yani mpaa Amerca kapeleka Nuclear 😂 anadhani Hamasi watamuogopa vita sio kuwa na vifaru vingi au ndege nyingi ni vipi unapigana.

Hakuna kitu duniani kama iman mwenyezi Mungu alisha sema ukiwa na Iman usiogope kitu.

Mimi na uhakika Israel hawezi shinda vita hi hata asaidiwe na Europe yote na America alidhani kuwakatia maji, umeme na chakula wananchi wa Gaza watawageukia Hamasi jamaa wa Gaza wala hawakujali.

Anawambia wengine tokeni majumbani kwenu afu sehemu ya usalama akisha ona wanaenda kule anakuja wauwa.

Je hili ndio taifa lenu teule kama mnavyo dai kwenye bibilia zenu 😂 hilo taifa linaonyesha action za ushetani kuwauwa watu ambao hawana silaha.
 
Humanitarian ndiyo Jambo muhimu MUNGU anataka sio hizi dini zetu...
Mauaji yanayotokea Gaza haifai kushabikia hata kidogo ingawa wabongo wengi naona wamefanya ushabiki kama wa Simba na yangq
 
Nadhani mwisho wa Hamas umefika, wamechekewa muda mrefu wakaota mapembe.
Shambulio lililofanywa na Hamas ni historical,

Wameuwa maelfu na kuchukuwa mateka waisrael wasiokuwa na idadi

Haijawahi tokea toka kuanzishwa kwa taifa la Israel. ...

Maswali::
1. Dunia nzima wanajiuliza (including waisrael wenyewe) Hamas wanajiamini nini kwa kufanya uchokozi mkubwa katika historia ya chokozi zote duniani (911 included) ..hasa ukizingatia huko nyuma vita baina yao ilisababishwa na kisa kidogo sana( kumteka mwanajeshi wa Israel mmoja)

2.Mossad ....ni shirika la kijasusi la Israel ambalo linasemekana ndio lenye uwezo na utaalamu wa mambo ya kijasusi kuliko mashirika yote duniani" limefelije kujua mpango wa uvamizi wa Hamas? ...na nini kingine hawakijui ...maana isijekawa trap iliyoratibiwa na kuandaliwa vizuri

3. Bombing Gaza ni kitu cha kawaida kwa waPalestina, kuingia vitani mtaa kwa mtaa Gaza ni mission ngumu sana kwa waisrael kwani hakuna Frontline maalumu ni vita vya kuoteana (urban gorilla warfare )....ila mwenyeji obviously will have upper hand kwa sababu ya familiarity with location &terrains. . ... je kuna appetite ya kutosha?

4. Wakisha ingia Gaza, what is the endgame, km vita ikienda ndivyo sivyo" what is the plan B

5. pamoja na Israel kuwa na silaha za kisasa sana za kivita.....are its soldiers are gorilla battle hardened? ...maana kuna tetesi zile njemba za Hizbu ambazo zimezoea shughuli pevu toka Syria zimeingia kitambo...

Haya maswali yanahitaji cooler& sober mind kuyajibu kwanza kwa ufasaha kabla ya kuingia kwenye huu mwaliko wa vita Gaza.

Nb. Naomba niwakumbushe wakristo wenzangu taifa la Mungu la israel sio hili linaloongozwa na Bibi...

Tuendelee kumuomba Mungu awanusuru wote kwenye kwenye hili janga ambalo hakuna anayejua mwisho wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…