mkiluvya
JF-Expert Member
- May 23, 2019
- 809
- 729
Watu 25 zaidi wamepatikana vna virusi vya corona, na kulifanya taifa la Kenya kuwa na jumla ya visa vya maambukizi 912, Kulingana na taarifa iliyotolewa na Katibu tawala wa waziri wa Afya Rashid Aman Jumatatu.
23 kati yao ni wanaume, huku waili wakiwa ni wanawake. Umri wao ni kati ya miaka 22 na miaka 50
23 kati ya visa vipya vya maambukizi ya Covid-19 ni raia wa Kenya, huku 2 wakiwa ni raia wa Wasomali.
kaunti za Taita Taveta, Garissa na Meru ni maeneo ya hivi karibuni kurekodi visa vyake vya kwanza vya virusi vya corona. Taveta ina wagonjwa 2, Garissa 2 na Meru 1.
Dkt Aman amesema kuwa sampuni 44,851 ndizo zilizokwishapimwa hadi sasa.
Mpango unaolengwa kwa sasa ni kuwapima watu wengi.''Tumepokea vifaa vya kupima ndio maana tumeongeza shughuli ya upimaji'', amesema.