Mkurya romantic
Member
- Jul 21, 2022
- 41
- 61
Imekua tabia ya mda mrefu sasa kuwachukulia watu kutoka maeneo ya visiwa vya ziwa Victoria kua ni watu washamba wasio jua chochote sana sana kisiwa cha UKEREWE kinaonekana ni kisiwa cha watu washamba sana ila leo ningependa kutoa orodha ya watu muhimu nchini walio tokea ukerewe
Uzi bado unaendelea......
Ni eneo gani jingine watu wana lichukulia poa lakini lina watu muhimu na wenye mambo makubwa ?
Tiririka chini uzi huuu
- Piusi Msekwa Amewahi kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mabunge ya Nchi za Jumuiya ya Madola (CPA) kati ya mwaka 1999-2002, pia Mjumbe wa Kamati ya Kurekebisha Sekta ya Sheria kati ya mwaka 1993-1994 na Mjumbe wa Tume ya Rais ya Kuangalia Mfumo wa Vyama vya Siasa nchini kati ya mwaka 1991-1992. Nyadhifa nyingine ambazo amewahi kuzishikilia, ni Uenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi katika Mamlaka ya Maendeleo ya Mitaji kati ya mwaka 1985-2000 na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi katika Chuo cha Uongozi wa Wanyamapori barani Afrika kati ya mwaka 1985-2000. Vilevile aliwahi kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu kati ya mwaka 1984-1989, Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi katika Chuo cha Ushirika Moshi kati ya mwaka 1984, Mjumbe wa Tume ya Kurekebisha Sheria mwaka 1983 na Mjumbe wa Kamati ya Rais ya Kupunguza Matumizi ya Serikali kati ya mwaka 1982-1983.
- Mama Getruda Mongella = Gertrude Mongela ameshika nyadhifa mbalimbali za kitaifa na kimataifa. Miaka 1993-1995 alikuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Wanawake na kuhudhuria mkutano wake wa nne uliofanyika Beijing, China mwaka 1995. Amewahi kuwa balozi nchini India (1991-1993), Waziri Asiye na Wizara Maalum, Waziri wa Ardhi, Maliasili na Utalii, mshauri maalum wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi, na Utamaduni
Uzi bado unaendelea......
Ni eneo gani jingine watu wana lichukulia poa lakini lina watu muhimu na wenye mambo makubwa ?
Tiririka chini uzi huuu