Mafanikio kimaisha

Happiness kwa mimi na wale walionizunguka....
Kutumia kile nilichonacho / takachokipata, kuleta mabadiliko chanya from A to B (no matter how high or low that B is so long as its higher than A)
 
Reactions: Mbu

G hili lipo sana kuna watu wana ngekewa zao everything they touch turns to gold.


BAK siamini kama vinageuka tu dhahabu bila ya kuweka juhudi na maarifa. Mgeuza dhahabu nae anapata tabu kwa kiasi chake, japo kwua wewe ulioko pembeni unaona otherwise
 
Reactions: Mbu
Dunia uwanja wa fujo...

Hakuna happiness..(umeme, bad news, oppression, work hard less pay, fraud, etc..)

I am thinking to quit and look for a Garden (a promised garden heaven)

How to have a garden is my happiness
 
Reactions: Mbu
huko bhutan nao wana kitu inaitwa gross national happiness.
wameamua kutumia furaha kama kigezo cha kipimo cha maendeleo
katika nchi yao. jamaa wameunda na wizara kabisa ya kufuatilia hili.

 
Reactions: Mbu

...phheeewwww, sijakusoma siku nyingi sana...upo wewe?
raha kukuona hapa...umesema mafanikio yako ni kuridhika na majaaliwa yako?


msafi, aksante sana kwa angalizo hilo. Kusudio la kuishi........................ hivi ni wangapi wanjua makusudio yao?! Mie kusema ukweli nakiri kuwa weak wenye hii angle. Nadhani ndio maana mambo hayako sawa, I need a therapy.

....lol,...mwj1 you never fail to amaze me...
hapana bana, you are not in this world hususan jioni hii kwenye jf by accident...
you are here for a reason!...hebu jichungue na ujikubalishe thamani yako bana!


Happiness kwa mimi na wale walionizunguka....
Kutumia kile nilichonacho / takachokipata, kuleta mabadiliko chanya from A to B (no matter how high or low that B is so long as its higher than A)

...what if?....ukishindwa ku fulfil hizo 'multitasks' unajihesabu hujapata mafanikio maishani?
au nawe ni katika wale wanao accept their fates?


Dunia uwanja wa fujo...

Hakuna happiness..(umeme, bad news, oppression, work hard less pay, fraud, etc..)

I am thinking to quit and look for a Garden (a promised garden heaven)

How to have a garden is my happiness

...khaaa? hapana bana,....huko sasa ni kukaribisha depression wakati
sredi hii ni maksusi kusaidiana ni kwa jinsi gani tunayaangalia maisha, tulikotoka,
hapa tulipo na tunakoelekea...hakuna kukata tamaa!

...heaven ni promised land?...wanasema ili ukayafaidi matunda ya huko ni lazima vigezo na masharti
yazingatiwe ikiwemo kwenda huko na daftari lako linalojielezea umetumia vipi haya ;


- ujana wako kabla ya utu uzima wako

- afya yako kabla ya ugonjwa wako
- utajiri wako kabla ya umasikini wako
- uhai wako kabla ya kifo chako...




 

...what if?....ukishindwa ku fulfil hizo 'multitasks' unajihesabu hujapata mafanikio maishani?
au nawe ni katika wale wanao accept their fates?


Mkuu unajua issue inategemea na talent ya mtu.., mfano ningekuwa na kipaji (potential) kama ya Messi alafu nikacheza ligi daraja la nne, au ningekuwa naweza kuimba kama Michael Jackson alafu nisitoe Single.., au Kuandika Vitabu kama Sydney Sheldon alafu nisiandike kitabu....!! Then siwezi kusema nimefanikiwa...

Its all about potential ya mtu.., na nikiweza kufanikisha hio potential isiwe kwa faida yangu tu wala isilete karaha kwa watu...

Lakini in really life most of us are average.., kwahiyo having a normal average life, bila kuwa mzigo kwa wanaokuzunguka na ku-play your part kwenye jamii (even if ni kusafisha vyoo au kuchimba makaburi) ni mafanikio katika maisha...

Sababu mafanikio hayawezi yakawa equated na monetary au status value.., bali ni ku-accomplish what you started in life.. (be it kuchimba vyoo, basi chimba vyoo vizuri na penda shughuli yako na kuleta furaha kwa wanao kuzunguka)
 

...lol...hahahahahaahah!....

aisee wewe umenichekesha sana hiyo mifano yako ya 'mafanikio' kutokana na majaaliwa yako...
nadhani nitakuomba tuongozane niendapo kuangalia mafundi mbalimbali ninaowatumia...
hawana discipline ya kazi hata kidogo!

maendeleo na mafanikio ni kitu kimoja?
 

True Pretty...Definition of "Success in life" differs from one person to another.... Msalimie sana baby.
 
...lol...hahahahahaahah!....

maendeleo na mafanikio ni kitu kimoja?

Defenetely mkuu kuna quote moja inasema....

"Success is to be measured not so much by the position that one has reached in life as by the obstacles that one has overcome"

Kwahiyo mkuu hata kama ni safari wewe badala ya kwenda mbele unarudi nyuma (wazazi wako wamekuachia mtaji wewe unafilisi au wamekuachia Bilioni nne wewe unaongeza laki moja tu..., au unakuwa baba wa familia unauza nyumba na kulaza watoto njaa..) huwezi kusema umefanikiwa kwenye maisha..

Wakati yule alianza na familia akiwa labda mtoto wa shule..., akaweza kutunza mtoto wake mpaka akawa mtu mzima na yeye akaweza kujiangalia na angalau kupata mlo mmoja kila siku (tasema huyu amefanikiwa kutokana na njia alizopitia)..,

Alafu hapa siongelei mafanikio tu bali hata kushindwa kutumia opportunities ambazo zipo available for your detriment and others detriment..

Pia mkuu tusisahau personal satisfaction.., nadhani kama mtu ungependa uwe mchoraji alafu sababu ya pressure ya watu ukawa daktari bingwa it is debatable kama umefanikiwa katika maisha iwapo kila siku utakuwa hupendi kazi yako na kuna kitu kina-miss
 
VOR

utajijuaje kama wwe ni average tu? unapimaje kipawa chako?
 
VOR

utajijuaje kama wwe ni average tu? unapimaje kipawa chako?

Potential huwa inaonekana wakati watu tunakuwa tangia wadogo.., kuna vitu huwa ni vyepesi sana kwetu kuliko wengine ila tu katika kukua unakuta mtu unaloose the way.

Au mtu sababu ya ulevi, au mambo ya kidunia kuanguka au kuacha kile alichokuwa anakifanya vizuri na kupotea njia.

Ingawa ukweli ni kwamba persistent kwa kila mtu akifanya anafanikiwa ila wengi huwa tunakata tamaa (lakini kukata kwetu tamaa kusifanye tuishi au kuwa mzigo kwa wengine) na tukifanya hayo tutakuwa tumefanikiwa in the eyes of an average community.

Na kuhusu kipawa chako bila kujaribu huwezi kujua kwahiyo kama unapenda kuimba, imba watu wakipenda nyimbo zako then una kipaji.., lakini ukiimba single kama moja alafu ukaanza kubwia unga na kunywa pombe hadi ukaharibu kazi zako nadhani utakuwa hujafanikiwa kwenye maisha..

nadhani unakubaliana na mimi kwamba "There is Nothing Worse than Wasted Talent.."
 
Mbu, mimi naweza kusema niko upande wa Gaijini maana kwa jinsi alivyotoa maelezo yake it's the same thing which was on my mind at the same time umenikumbusha ule wimbo wa jana ambao aliuweka MTM kwenye thread ya MwanajamiiOne, kila mtu binafsi ana jinsi ya kutasfiri mafanikio kwake kuna mwingine alitamani awe na gari kuna mwingine alitamani apate nyumba kuna baadhi ya watu wakiishapata baadhi ya vitu wanaona wameridhika na kufanikiwa.

Lakini mimi binafsi naona ukiwa na amani moyo ni mwako ni kila kitu, ukiwa na watu wanaokupenda, kukuthamini na kukujali hivi vitu vingine kwa kweli havitakupa shida na pia hapa nitagusia mahusiano kidogo unaweza kukubaliana na mimi mahusiano yaliyo bora ni moja ya mafanikio ya kimaisha kuna watu watauliza kwanini? Lakini i tell you ukiwa na mtu anayekuthamini, kukupenda na kukujali it's more than artificial things ambavyo utakuwa unavifikiria kuwa ukivipata utakuwa umefanikiwa because to me i believe they come and go I've been there already. Kwahiyo naomba niunge mkono mawazo ya Gaijin
 
Rocky are you saying kua mpaka hapo ulipo bado kabisa hujapata hata kijihisia kua kitu fulani ama mahala fulani ndo utaona umefanikiwa??

AshaDii sikatai na wala sijilaumu kwa hali niliyo nacho na nilicho nacho. Kwanza kwa upande wangu ni above what I expect at my age.
Kuna hali ile ya kusema nikimaliza shule nitafanya kazi na kujenga nyumba na kuwa na gari na then niwe na familia
Then baada ya hapo inakuwaje unafanya nini ni kula na kufurahi tuu au kuna la zaidi hapo
Hapo ndio sasa unatakiwa uwe na malengo ambayo kwa sometime inakuwa ngumu kuyapata kwa wakati mmoja ila bado tunapambana
Mafanikio yapo na namshukuru Mungu sana kwa hatua ya maisha nilipo na bado napambana sio kwamba nimerelax as if nimefika mwisho wa njia na kwa sasa naona kama ndio kwanza hatua naanza
Kama ni mtoto ndo kwanza anatambaa bado hajaanza hata kunyanyuka
Maana tunachoangalia ni mafanikio binafsi na the mustakabali wa watoto wako utakaokuwa nao wasije kupitia hatua au type ya maisha uliyopitia wewe wakati wa kukua kwako
 
Hii topic nimejikuta nakumbuka maneno kwenye wimbo wa BRYAN WHITE

I guess I must be wishing on
Someone else's star
It seems like someone else keeps getting
What I'm wishing for
Why can't I be as lucky
As those other people are
I guess I must be wishing
On someone else's star
 

Nakubali potential inaonekana tokea wadogo na saa nyengine unakuja kugundua kuwa wewe ni hodari wa kitu fulani lakini hili la kutojaribu ndilo linalosababisha wasichana wengi wakatae kusoma masomo ya sayansi wakisema wao hawawezi japo hawajaweka effort

General speaking, kwa bidii ndogo tu majority ya watu wanaweza kufanya vitu vikubwa, lakini wengi hatufanyi kwa vile ama hatujiamini au tunaridhika kirahisi na tulichonacho.

Siwezi kusema ni mbaya kwa vile wasipofanya huwa wana furaha na wameridhika kwa hiyo kwa definition niliyoitoa (mmmh!!??) wanajiona kuwa weshafanikiwa though sisi tuliomzunguka tunaewza kuona kuwa ni wasted talent
 


hapo Mkuu umenipoteza, mimi mawazo ya aina hiyo sijawahi kuwa nayo. (My pasture is always green?? au ndio kuridhika tu)
 
Unalosema ni kweli sio tu kwa wasichana hata wavulana kuna kitu kinaitwa UTHUBUTU nakumbuka kuna kipindi niliona kazi wanahitaji Project Manager at first nilipoona vigezo kwanza nilichoka nikasema that's not for me maana niliona zile qualification ziko juu sana lakini baadae sijui kitu gani kiliniijia kichwani nika-apply nilishangaa nilipopigiwa simu kuitwa kwenye interview of 20 people tulioomba walikuwa wanahitaji mtu mmoja tu but nafikiri kule kujiamini kwangu ndiko kulinifanya nipate, kwahiyo nafikiri tukiwa na uthubutu kwenye jambo lolote i believe you'll succeed
 
hapo Mkuu umenipoteza, mimi mawazo ya aina hiyo sijawahi kuwa nayo. (My pasture is always green?? au ndio kuridhika tu)
Unajua Gaijin nilisoma lyrics za huu wimbo nikaanza kujiuliza what was in his mind alipokuwa anaandika na mawazo kama hayo yaki-dwell in your mind chochote utakachofanya utaona it's nothing at all
 
Mbu, Thanks for the post,

Binadamu tumeumbwa na roho dhaifu ambayo hata siku moja haiwezi kuthamini mafanikio yake. Hata Steve Jobs hakuamini kama amefanikiwa hadi alivyokufa na kuacha mamilion wana-lia.

Sometime, hata mimi binafsi najisahau na kuhisi bado nina mwendo mrefu kufikia mafanikio, ni udhaifu wangu kwani nasahau nimeruka vi-uzi vingi hadi kufikia hapa nilipo. Nasahau hata kuna watu wanasoma mazaga zaga nayoandika na kunipa Thanks hata pale nisipositahili, yaani hayo ni mafanikio tosha kuona una-heshimiwa na jamii hata kama jamii hiyo imebaki na mtu moja tu ambaye ni mke au mpenzi wako....

Ningeweza kua-andika mengi, lakini nashindwa kupata benchmark kwani kuna factor nyingi na zinabadilika badilika hasa kutokana na Muda..mfano binafsi nafikiri nimefanikiwa kuwa na ka-team nako-kaita familia ambacho najua nisipofanya kazi wamekufa njaa.. Namshukuru Munga bado wako hai nami bado sijainua mdomo au mkono wangu kumpiga mama yao...Kwa upande wa pili naona sijafanikiwa kwani sometime nakosa usingizi nikifikiri siku nikichemsha hii Team yangu itapigwa bao na maisha.. Where is the limit? Anyway, ni mfano mdogo..

All in all, tukiacha udhaifu wetu wa kutoona mafanikio yetu, tumefanikiwa kwa vitu vingi tu!!
 
...nawashukuru sana nyote kwa michango yenu jumapili ya leo...
kiukweli nimefaidika na mawazo yenu nyote na ningependa kutoa hitimisho hili
kwa jinsi nilivyowasoma na kuwaelewa na mtizamo wangu ulivyokuwa...;

mafanikio nm matokeo mazuri ya jambo, ustawi, fanaka
maisha nm muda wa uhai wa kiumbe

....nimejiridhisha hakuna binadamu ambaye atakuwaa na mafanikio kwa
asilimia 100%...lazima patatokea mapungufu sehemu mojawapo ya maisha yake.

...ndio kusema, kila mmoja wetu anawajibika kufurahia sehemu yoyote ya mafanikio yake maishani,
hata iwe ni ndogo kama mdudu chungu, mfano yule anayebahatisha hewa, mlo na maji...au yule aliyejaaliwa mali,
watoto, na upendo wa hali ya juu lakini moyoni mwake ameshindwa kuuondoa, wivu, chuki, na katika na hayo.

mwenyezi mungu atuongoze katika njia iliyo sahihi, na atuzidishie nuru ya kutambua neema zake alizotujaalia.
- amen -

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…