Mafanikio ya awamu ya 5 sasa yanaanza kuonekana

Socratic

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2014
Posts
568
Reaction score
308
1. Kuna ongezeko kubwa la waumini makanisani japo sadaka haiongezeki (watu wanatafuta pa kuzugia kusukuma weekend)
2. Ndoa zimeendelea kuimarika na upendo wa familia unarejea kwa kasi (wababa wanarudi nyumbani kwa wakati)
3. Kuna kila dalili ya anguko la viccoba (watu wanakimbia na marejesho)
4. Kuna upungufu mkubwa wa paka maeneo ya bar na restaurants (watu wanalamba mpaka sahani na hakuna mabaki)
5. Kuongezeka kwa vibanda vya utumbo mitaani (nyama, maini na kuku vinaliwa kwa maelekezo ya daktari)
6. Kuongezeka kwa uhasama kati ya binadamu na mbuzi (binadamu kuingilia malisho ya mbuzi kwa kuongeza milo ya mboga za majani)
7. Kumbi za sherehe kugeuka maghala (harusi na sendoff kufanyika majumbani)
8. Kupungua kwa vitambi na nyama uzembe bila mazoezi (maji kwa sana badala ya bia ndo mpango mzima).
Na bado
 
Kuongezeka Kwa Wahuni wa siasa kufanya utapeli wa kisiasa kwa malengo yao

Uchungaji kuingiliwa na siasa
ili mt aendelee Kuwapiga watu Mpunga

Bila kutafuta kik walau kujiteka
mambo hayaendi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…