Mafanikio Ya Diamond ni Dalili ya Kifo

KakaJambazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2009
Posts
18,804
Reaction score
12,227
Kitendo cha diamond kila anapokwenda nchi husika husimama, anapokelewa kama mfalme, mambo makubwa nanayoyafanya kimziki, kiulimwengu wa roho, ni dalili ya kifo kinamnyemelea (Eeh Mungu muepushie na jinamizi hili).

Daimond anachafanya sasa ivi, kiulimwengu wa roho ni kupata mashabiki ambao siku sio nyingi watakuja kuhuzunika sana, kwani kifo chake kitakua cha ghafla tu.
Fuatilia hii duniani huko na hapa tz, kwa watu wote na hata kwa wanasiasa eg Deo Filikunjombe na wengine, vifo vyao vinatokana na Ibilisi kutaka kuwaumiza wanaobaki.

Diamond ni kama vile anawaaga mashabiki zake.
Namshauri Diamond asali sana, kwani ibilisi mtoa roho anamnyemelea.
 
Watanzania bwana mna mambo ya ajabu, diamond anasimamisha watu kama justin beiber, kama drake, kama rihanna, kama beyonce?
Justin Beiber akipita mtaani mabinti wanavyomkimbilia hatari tupu.
Chris Brown mwaka juzi alipiga show ghana akalipwa ela yenye thaman ya pesa ya madafu bils 2.5, mpaka watu wakalalamika kwanini nchi masikini kama ghana inagawa mpunga mwingi hivyo?
Mbona hao hawajafa?
 
Mkuu una roho mbayaa aisee, hivi ungekuwa ni wewe........
 
Kila mwanadamu lazima atauonja umauti sio Mimi, wewe na yeye Ndio maana unatakiwa Kuish kama unakufa kesho.

Hakuna jipya hata yeye Akifa Atakuwa sio wa kwanza Wala wa Mwisho kufa.

Nawewe jipange Kwani hata nusu saa Yako ya baadaye huifahamu.

Njia za Mauti ni nyingi tu, Ila kufa ni kule kule.

Mwanadamu hutakiwi kukiogopa kifo abadani.

Hakika wewe ni kaka jambazi
 
Mafanikio hayo acha kumsema mwenzako vibaya kawaida ya wabongo kusema watu vibaya wala hainishangaz sana
 
Reactions: BAK
Sasa hata kama uliomba kazi ya kuwa mganga wake wa kienyeji ukanyimwa usitumie mitandao kumshawishi akufikirie tena. Hata Sheikh Y..ya naye alikuwa akitoa vitisho kama hivyo ambavyo ni upuuzi tu.
 
WEWE
WEWE NDIYE UTAKUWA UNATUAGA HIVYO.ISRAELI AMESHAKUINGIA HIVYO ANZA KUANDIKA WOSIA
 
Mkuu una roho mbayaa aisee, hivi ungekuwa ni wewe........
Mkuu mi si naelezea hali halisi, hata wewe hapo leo ghafla ukianza kuporomosha majumba, huwezi chukua miaka 7.

Mfano mzuri, yule marehemu Seki lusekelo,(mfanyabiashara wa madini-Tanzanite) mimi nimeishi nae, kwao walikua masikini, wakutupwa enzi hizo sekondari, alisoma kwa shida sana, akafaulu akaenda Chuo kikuu, alivyomaliza aliajiriwa mgodi wa Bulyanhulu, akafanya kazi miezi 6 tu, akaenda Mererani, akaanza kupata hela za ajabu, sasa ivi ni historia.

Mkuu imani huja kwa kusikia.
 
Nimakosa kumtabiria MTU kifo.
 
Mi namwomba asali na afunge sana. Aachane na uhuni kwani pia ibilisi ndo njia zake izo.
 
Duh, kumbe na Ali Kiba naye anawaaga watu huko Fiesta? Ni dalili kuwa atakufa hivi karibuni.
 

Kupata sifa na umaarufu mkubwa bila kumrudishia Mungu sifa na Utukufu hiyo ni hatari sana inayoweza kupelekea kifo cha mhusika!..
 
Kwa hiyo conclusion kutoka na huyo seki ni kila anayepata mafanikio basi kinachofuata ni kufa.
And by the way hakuna kinachoshangaza maana lazima mtu afe na hakuna muda sahihi wa kufa.
 
Mi namwomba asali na afunge sana. Aachane na uhuni kwani pia ibilisi ndo njia zake izo.
Kwa kifupi muziki ni kazi ya Shetani Mwanamuziki yoyote awe mkubwa au mdogo jua anafanya kaz ya Shetani. Shoo afanyie uwanjani mwingine sebuleni wote wanafanya kaz ya ibilis

Kifo Haijalishi wanaokufa Ndio watenda dhambi Hapana waovu na Wema wote watakufa.
 
Dah jaman hata kama hauependi mziki wake au sio fan wake lakin hatua hii ni hate iliyopitiliza aise kuhusisha na kifo duh
 
Yaani wewe kwanza akili huna,pili,umejifunza,au umefundishwa vibaya dini au imani yako,kwa ufupi,mambo unayoyaamini ni batili,tafuta msaada,nenda shule upate elimu
 
Kwa hiyo conclusion kutoka na huyo seki ni kila anayepata mafanikio basi kinachofuata ni kufa.
And by the way hakuna kinachoshangaza maana lazima mtu afe na hakuna muda sahihi wa kufa.
Mkuu hata hujanielewa.
 
Kupata sifa na umaarufu mkubwa bila kumrudishia Mungu sifa na Utukufu hiyo ni hatari sana inayoweza kupelekea kifo cha mhusika!..
Sedekia je utasemaje kuhusu yeye?
Au na yeye alikuwa hamrudishii Mungu sifa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…