Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Tulia hapo hapo piga goti utubu Mungu hadhihakiwi !
 
Nasisitiza tena TUBU!!!!!Huu ni unabii.
 
Ndio tatizo la misukule ! Wewe kama mkristo uwezi mfananisha binadamu na Yesu
wanafanana na hata yesu angekuwa mtanzania angempa udc hta wa sumbawanga mana ili uteuliwe lazima uwe
1.Mkristo/muislam asojua uislam.
2. Kipaumbele kwa wtu wa ziwa magharibi zaid sana mangosha
3.uwe ccm mpiga makofi kwa mfalume
 
Soma tena umsome kwa u makini utamwelewa ana maana gani. Hata mimi ni meridian mara tatu ndo nikamwelewa
 
Hapa nafasi yangu ya Utumishi ni kubwa sana____hata unipe Uwaziri cwezi kubali.

Kwa wanaokumbuka ule unabii wataamini ninachosema.
ingekua una uteuzi ungekua unahara humu jf???
 
Wewe ni msengerema! Unanena makufuru yaliyotabiriwa katika kitabu cha Daniel I 7
 
Wagalatia mna utani mwingi sana ! .......sijui Yesu AS mnamchukuliaje !??
 
Huu "unabii" utatimia lini ili iwe rahisi kuulizana wakati utakapofika!!!?
 
Duuuh........mungu kaja kama mfalme ! .....nabii wewe umetabiriwa na Kitabu gani !?
 
hivi jaman mbona tunazidi kuvalishana uungu mtu namna hii kati karne hii si vema huyu ni mwanadamu na ana mapungufu so sioni haja ya kumuhesabia haki kiasi hicho kwa kumpa sifa zote hiz wakati kuna mapungufu mengi bado.Tuacheni kumdhihaki Mungu jamani wewe sema mengine muache Mungu.
 
Eti nasikia Uchumi wetu upo Unstable labda kweli. Wapo wasemao hali mbaya Mh Rais amebana sasa sijui amewabana wapi awasemi wanasingizia uchumi. Tatizo siyo uchumi hawajazoea kutumia pesa kwa nidhamu. Mh anawapeleka njia hiyo taratibu tutazoea tu. Basi na kwa wanaojua siasa wanateck advantage kulikuza wamesahau la maandamano. Ila napenda msimamo alionao Mh raisi Swala nidhamu na hofu ya mwenye Mungu lianzie kwenye familia zetu ili baadaye tusipate viongozi wapigaji. Ombi langu kwa mh Raisi tupia macho na huku kwenye kilimo maana tuna ardhi kubwa lakini haitunufaishi najua viwanda bado hatuna ila tusafirishe hata nje. Mh rais pia huu mitaani kuna vijana wengiwao wameishia la saba na form4 kazi zao nizakipato cha siku moja na pesa nyingi huishia kwenye kubet na kula haswa chipsi Nakuomba utupe maeneo, elimu ya ukulima na vifaa. [HASHTAG]#triyme[/HASHTAG]
 
Kijiji hakina zahanati miaka 50, wajawazito wajifungulia porini WANANCHI wa kijiji cha
Zepisa, kata ya Hombolo
Bwawani, Manispaa ya
Dodoma, hawana uhakika wa
kupata tiba pale wanapougua
kutokana na kutokuwa na zahanati tangu nchi ipate
uhuru, hali inayowafanya
baadhi ya wajawazito
kujifungulia porini.
Wakizungumza na Nipashe jana,
baadhi ya wananchi wa kijiji hicho
kilichopo umbali wa zaidi ya
kilomita 50 kutoka makao makuu
ya manispaa ya Dodoma, walisema
kumekuwa na matukio mengi ya wajawazito kujifungulia porini
wakiwa njiani kuelekea zahanati ya
kata iliyopo umbali wa kilomita 13
kutoka kijiji hapo. Mkunga wa jadi kijijini hapo,
Evelyna Lugolein (80), alisema
kutokana na kukosekana kwa kituo
cha afya au zahanati amesaidia
kuzalisha zaidi ya wajawazito 800.
Alisema kutokana na kujitolea
kuzalisha wajawazito wengi, hivi sasa jina lake lipo kwenye zahanati ya kata
Hombolo Bwawani kutokana na wengi
wanaojisikia uchungu kwenda nyumbani kwake
kujifungua kisha kuwasindikiza katika zahanati
hiyo. "Kuna siku nilimsindikiza mama mmoja, tukiwa
porini usiku wa saa 6:00 akajisikia uchungu,
dereva wa bodaboda aliyetupakia alikimbia na
kutuacha hapo, ghafla nikasikia sauti ya fisi ikilia
hali iliyotuogopesha sana,” alisema. Mwananchi mwingine, Amina Matonya, alisema
wanawake wengi wajawazito kijijini hapo
wamekuwa wakijifungulia porini kutokana na
kushikwa uchungu wakati wakiwa njiani
kuelekea zahanati ya kata. “Tupo ndani ya manispaa, lakini kwa muda
mrefu kijiji hiki hatupewi ushirikiano wa huduma
ya afya, basi kama hawakitaki watuambie ili
tujue tumetengwa na serikali yetu,” alisema
Matonya. Kwa upande wake, mama aliyepoteza watoto
wake wawili kwa kukosa huduma za haraka
wakati wa kujifungua, Adovic Joseph, alisema
kitendo hicho kitaendelea kuwaathiri wengi
iwapo hawatajengewa zahanati na kuwapo
huduma stahiki. “Nina mtoto mmoja ambaye baada ya ujauzito
kufikisha miezi saba ilinibidi niende Dodoma
mjini kwa ndugu zangu ili niweze kupata
huduma hospitalini na nisimpoteze kama
ilivyokuwa kwa wawili wa mwanzo," alisema
Joseph. Mwenyekiti wa kijiji hicho, Justin Chilingo,
alisema kijiji hicho ni kama kimetelekezwa na
serikali kutokana na kujenga msingi wa zahanati
na kutandaza jamvi kwa muda mrefu kisha
kuondoka. Naye Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ya Hombolo
Bwawani, Daudi Kamunya, alisema kijiji hicho
kina kaya 1,224 zenye wakazi zaidi ya 7,000,
lakini maisha ya wananchi wake yamekuwa ya
shida kutokana na kutopewa kipaumbele. Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma, Godwin
Kunambi, alipoulizwa kuhusiana na malalamiko
ya wananchi wa kijiji hicho kuhusu zahanati,
alisema suala hilo linashughulikiwa. Naye Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony
Mavunde, alisema atahakikisha suala hilo
linashughulikiwa haraka.
Source: IPP MEDIA
 
Sasa mkuu kama suala hilo limefika kwa viongozi wa wilaya mkoa na taifa esp mbunge na waziri kuna haja gani ya kumlaumu rais??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…