Hakika kabisa uongozi ni mzigo mkubwa mnoo kwa mwenye nia thabiti ya kuwakomboa mamilioni waliopo kwenye lindi la umaskini.Viongozi wazalendo na wakweli hawawezi kukwepa kuchukiwa na kundi la wezi,makabaila,mabeberu,Wanyonyaji,Mafisadi na wanyang'anyi.
Viongozi wetu wakuu wanafanya kazi ngumu sana wawapo madarakani,Kazi yenye wingi wa lawama,Majukumu yenye kuhatarisha hata uhai wao toka kwa maadui wa haki,Kazi zenye kufurahisha kundi moja huku jingine likibubujikwa na majonzi..
Wananchi wenye kulipenda taifa/nchi twapaswa kuwaombea mbele za mwenyezi Mungu kwa dhati kabisa ili Mungu Mwenyezi aweze kuwatia nguvu/kuwapa hekima kubwa/kuwapa ujasiri mkuu/kuwapa mamlaka kuu na kuwawezesha kufanya mengi yalio makusudi ya Mungu kwa Taifa hili kimaendeleo.Kwa nguvu,hekima na fahamu zao pekee hawawezi bali katika Mungu muumba awatiae nguvu {roho,Nafsi na Mwili}...
Watawapiga vita sana-msivunjike moyo,watawateta-Msikate tamaa,Watawasusia-Simameni imara,Watapanga njama gizani-Mungu atawaumbua kweupe,Watafanya hila za kila namna-Watashindwa na kulegea,Watafanya ushirikina-Utawarudia wenyewe,Watalazimisha mapenzi yao-Yatakwama.....
Fanyeni kazi bila kuchoka nyinyi viongozi mnaopigana kila kukicha kutokomeza wizi,rushwa,ufisadi,ulaghai,uvivu,uhuni,Mazoea {Kisiasa,Kiuchumi,Kijamii}"Hakika Mtayaweza yote katika yeye {Mungu Muumba} awatiaye Nguvu"