Hakuna anayepinga juhudi za rais wetu, japo wapo wanaohoji ili kupata ukweli, ndo hilo tu!
Jambo la kujiuliza ...
Waliomtangulia walikuwa ni wa kutoka chama gani?
Kama wote walitoka chama hichohicho ina maana ndani ya chama hicho kuna wachache sana wenye kuwa waadirifu kiutendaji.
Akimaliza mda wake si watarudi walewale waharibu tena ili tuanze na moja?
Kinachotakiwa ni kufumua mfumo mzima ... wachache wajiunge na upinzani ili chama cha wapiga deal kiwekwe pembeni.
Nimeyaandika haya leo lakini baada ya miaka 10 mbele mtayaona haya!
Walioharibu raiway,
Waliotuuzia nguzo za umeme toka misitu yetu,
Waliosaini mikataba pasipo kuisoma
Waliouza maliasiri za taifa
Waliouza hadi wanyama na kuwasafirisha nje wakiwa hai
Hawa wote bado wapo na wanasubiri mda wa mpambanaji wetu uishe warudi tena kuendeleza ufisadi wao!