Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Ameshalalamika mara nyingi tu kwamba Urais mgumu. Kama kazi inamshinda anangoja nini? AJIUZULU.
 
Hapa na paswa kumjibu yeye mwenye uwezo wa kutupa katiba mpya kukujibu wewe ni sawa na kukimbiza upepo
huna jipya maana unaonekana hata hujui katiba yenyewe inasemaje hujui hata kipengere gani cha katiba kibadirishwe nyie ndiyo mkiambiwaandamaneni mnafuata mkumbo ukikamatwa na kuuliwa unataka katiba ibadirike kipengele gani hujui sasa ni majanga mnayataka?
 
Amwache CAG afanye kazi zake bila bughudha, aondoe kifungu cha kuzuia CAG asikague madini.

Na aruhusu wananchi tuzipate ripoti za CAG bila bughudha kabisa.

Mzalendo wa kweli haogopi kukaguliwa.
 
Amwache CAG afanye kazi zake bila bughudha, aondoe kifungu cha kuzuia CAG asikague madini.

Na aruhusu wananchi tuzipate ripoti za CAG bila bughudha kabisa.

Mzalendo wa kweli haogopi kukaguliwa.
Madini ATCL na TANROADS
 
Unataka ligi maana najua ujui ila unataka kujifanya unajua pole endelea kukomaa ni bando lako tu.
siyo nataka ligi muangaliege na mambo ya kushabikia siyo unashabikia kitu ambachohukijui kisa watu wengi wanataka katiba mpya wewe hujui hata unataka badiliko gani kwenye katiba pole sana
 
Write your reply...Kukomesha mihazara ya kidini.Yaani sasa hivi kama awamu ya kwanza bado bongo flava na uvutaji bangi.
 
Acha porojo mbona hali ni mbaya zaidi kuliko enzi za upigaji,
 
kwa uwezo wa nchi wa BUDGET ya 40%?? Binafsi nitampima kama ataongeza pato la taifa kuwa zaidi ya 50% ya budget ya nchi.
Hivyo vingine ni too much ujamaa/ujima
 
Ningekuwa ninaruhusiwa kutoka tathim ningetoa kama ifuatavyo
1. Huduma Kwa wananchi wanyonge 99%
2. Miundo mbinu 89%
3. Maamuzi magumu 101%
4. Kupokea ushauri 100%
5. Michezo 40%
6. Kukubalika CCM 58%
7. Wanafiki wanaokufuata kama yuda Iskariote (wanafiki) alivyofanya 78%
8. Uhuru wa demokrasia nchini 15%
9. Siasa za kimataifa na kukubalika 90%
10. Wapinzani kujifanya hawakuelewi lakini wanakuelewa 79%
11. Huduma Kwa wananchi bomoa bomoa 50%
 
Mimi kitaaluma ni mhandisi naelewa uhandisi japo sijawahi kuzungumzia uhandisi humu hata kidogo

Kimsingi nchi maskini kama yetu inahitaji nishati nyingi na yakutosha

Kikwete ameimba sana ngonjera ya mchuchuma na liganga hatujaona kitu ngonjera zilizoanza tangu enzi za rais mstahafu benjamin willium mkapa jembe langu

Tukaja kwenye gesi ya mtwara hakuna mabadiliko halisi tunayoyaona kama watanzania

huu mpango wa stiglers gorge wa mh magufuli ukitengemaa na kusimama basi kumkosoa kwangu kutakoma hapo !!!

Hakika huu utakuwa ni ukombozi kwa watanzania hususani maskini!!

Viva jpm
Viva ccm

Ila kama hiyo peoject itasimama

Mambo ambayo sitayakubali kamwe kwa utawala huu ni haya

1.demokrasia
2.makundi maalum kuminywa stahiki zao halali
3.kutekana Tekana na kupigana pyu pyupyu
4.wanasiasa kuhama vyama kishamba shamba
5.kukusifusifu sehemu ambayo hata huitaji masifa kimsingi masifa yanashusha hadhi hayapandishi waambie wanaokuzunguka waache mtindo WA kukusifusifu halafu mbaya zaidi wanakusifu kishamba haustahili sifa zao za kinafiki bora cc tunaokukosoa kwa haki kuliko wanaokusifu kinafiki
Ila ukitoa hayo hapo juu mh rais John Joseph pombe magufuli I personally love you!!!!

Muda huu naamini umepumzika baada ya siku nzima ya kulijenga taifa!!


Be blessed na usiku mwema mh rais wangu!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…