Tangu aingie madarakani rais John Pombe Magufuli,amefanya mambo mengi mazito,mazuri na ya ajabu kwa kiwango chake.
Pamoja na mambo anayoifanyia nchi yetu kuwamekuwa na baadhi ya watanzania wenzetu ambao wao wameamua kuziba macho na kutokuona lolote jema alifanyalo.
Ukweli ni kuwa mh rais Fanya kazi ambayo kila mtanzania anaiona hata wale wanaojifanya hawaoni ipo siku kama si mioyoni mwao watatamka hadharani kwamba wewe ulikuwa rais makini,mzalendo,mchapa kazi na mwadilifu.
Sifa ya mwanadamu ni kukataa kilichopo,Ila siku kikitoka atakitamani tena kwa sifa kemu kemu.Asili ya watanzania tunaijua,ni wanafiki,wavivu,waongo,wafitini na wapenda vya dezo.
Pambana jemedari wetu siku ukiondoka madarakani tutayataja mazuri yako ya kununua ndege,kujenga madaraja,kutoa elimu bure,huduma za maji,afya na umeme,kuondoa uzembe kazini,uzalendo usio na shaka,uaminifu na uadilifu wako katika utumishi Wa umma.
Usiogope kusemwa,hata aliyewaumba wanadamu anasemwa,tena kwa kashifa,wewe ni zaidi maana ni mwanadanu tu unaishi Leo kesho haupo.Timiza wajibu wako kwa watanzania na Mungu atakubariki.
Viva Maguduli,daima mbele,nyuma ni mwiko.
Ukiwanacho haukithamini, kikiondoka ndo unalia kwa kukikumbuka. Atakumbukwa sana tu, kama wengine walivyokumbukwa