Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Wewe umeleta mambo ya mgao wa umeme watu wanakwambia kwao kuna umeme unaleta mambo ya kunyongana!!
UKiangalia hapo juu utaona jana mida kama hii nilimwambia mleta mada kwamba hatuna umeme; na hapa ninapoandika kwa mara nyingine hatuna umeme tangia saa 11!

Wewe Masenu K Msuya, unazungumzia vipi suala la siku tatu mfululizo kutokuwa na umeme mida zile zile?! Acheni kutetea ujinga nyie watu ambao posts zenu huwa mnaweka namba za simu! Kama mnatete ujinga kwa kutegemea uteuzi ndio maana huwa mnaweka hadi namba za simu, then you guys are among the worst creatures in this nation!
 
Utaambiwa siyo mgawo ila kwenu hakuna tu umeme!!
Wanakera sana hawa jamaa! Yaani wangejua damage ambayo tunaipata wala wasingethubutu kuleta mada za kipumbavu kama hizi! Nakumbuka Jmosi iliyopita ilibidi nimdanganya ninayemfanyia kazi kwamba Tanzania kuna heavy rainfall na kwahiyo Internet ipo down sana wakati tatizo lilikuwa umeme! Sijui uongo wangu utadumu kwa muda gani manake hata nikiangalia schedule yangu ya kazi, hadi sasa nilitakiwa nimefanya masaa 12 unusu lakini nimefanya for only 9 hours, nikiwa nyuma kwa saa 3 na ushee and counting!
 
Amefanya makubwa yapi kuongeza ufukara na umaskini wa watanzania ,miaka mitatu maskini wameongezeka sana kwa vitendo vyake mwenyewe .
 
Umeme ulitulia kidogo hasa miaka miwili iliyopita ukilinganisha na enzi za awamu ya nne..ila mwaka huu hadi sasa tumerudi kule kule,umeme unakatika sana maeneo mengi ya jiji la Dar na Pwani.Wenyewe wanasema ni "matengenezo ya kawaida" ila nnachojua mimi mwananchi nakosa umeme,sioni tofauti ya matengenezo ya kawaida na mgao wa umeme kama tangu December hadi February hii bado umeme unakatika mara kwa mara.Ni hasara tu.Mwaka huu Tanesco wanazingua.Mkuu nenda kule uzi wa Tanesco ukaone malalamiko.
 
Wewe unasema nini?,huku kibamba na probably mbezi tuko gizani tangu saa 4 00 usiku halafu unakuja kusema nini hapa?,kamwambie aliyekutuma hali haiko vizuri huku
 
Habari wakuu kwa muda mchache tangu rais wetu magufuli aingie madarakani amefanya mambo mengi makubwa sana kunaonekana kabisa transformation ya wazi kutoka nchi ya uchumi wa chini kwenda kwenye nchi ya uchumi wa kati.Tumeshuhudia akipambana na rushwa,akipigania maslai mapana ya nchi licha ya kejeli anazopata na vikwazo anavyotengenezewa na mambeberu kupitia wanasias uchwara lakini bado anafany kazi yake ipasavyo.Hongera magufuli umekuwa rais bora kuwahi kutokea afrika mashariki
 
Hata ukilinganisha jamaa na sababu ya magadi utaona sabuni ya magadi ni bora kwakuwa ndiyo unayo mudu kununua.
 

Mkuu Mheshimiwa Raisi kua Bora Afrika mashariki Ni Jambo li inawezekana kwa 100%.

Cha msingi Inategemeana not viwango vya contestants anaopambanishw nao. Mfano sitegemei
Mtu kama dikteta museven ampite JPM.nk

JIFANYE UNAJIKUNA, udadavue hayo mazuri aliyofanya muheshimia wetu ili kuweka Sawa maoni yako ikae vyema. Na watu waweze kuelewa

.
 
Hivi nashindwa kuelewA mbona maraisi waliotangulia walifanya mengi mazuri na wananchi tukafurahia matunda mazuri lakini watu hawakusifia mbali na kuneemeka na matunda ya mmoja mmoja Leo hii wanafiki wanajifanya kusifia tuu .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mambo yapi yanayoifanya nchi yetu kuelekea uchumiwa kati?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Raisi wa hovyo kuwahi kutokea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…