Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Ukiwafuatilia watu humu na maandiko yao hasa ya kumkosoa Magufuli ni sawa na maneno ya khanga.

Hivi unamwaminishaje Mwana kijijini wa kawaida tu eti Magufuli hajafanya chochote huko kijijini kwake ilhali anashudia majengo na miundombinu bora kabisa ya Vituo bora vya Afya!?

Hivi unamwaminishaje Mwananchi aliyezoea kwenda ofisi ya Serikali ya Kijiji kueleza shidaze na kuishia kuzungushwa na kutoonwa wa thamani ilhali leo wakati wa Magufuli huyo huyo aliyepata kutokuwa na thamani anasikilizwa na kuthaminiwa!?

Unamwaminishaje Mwananchi aliyezoea kutokukuta dawa katika Zahanati za Vijiji huku akishuhudia Mtumishi wa Afya akineemeka nazo kwa kuwauzia wenye maduka ya dawa ilhali kila uchwao wakati huu wa Magufuli dawa zi lukuki katika Zahanati!?

Mwananchi aliyefunzwa kujitegemea na Utawala huu atakueleweje wewe unayetaka ayarejelee maisha ya kugawiwa mahindi ya msaada!?

Mwananchi aliyefunzwa kufanya kazi kwa bidii na si kukaa kulewa na kupiga soga mtaani atakueleweje wewe unayetaka akae na apige soga mtaani akingojea msaada wa Serikali bure yeye kujishughulisha!?

Yapo mengi ya kusema!

Ndugu zangu Magufuli huyo si wakushindwa kwa maneno ya khanga na vijembe.

Magufuli huyo si wa kushindwa kwa eti watu waaminishwe kwamba mtu aliyepigwa risasi na wenziye kwamba aonewe huruma kwa dhanio la Yeye atakuwa kiongozi mzuri.


Magufuli huyo si wakushindwa kwa Wapinzaniye kuzunguka mitaa ya wazungu.


Jipangeni!Vinginevyo,hata Kitongoji hamtaambulia!
 
Tuma jina lako ,na teuzi unayopenda kufanya kazi box number 11 magogoni


Afu umesahau ambatanisha na number ya simu
 
Ngoja uanze kuogeshwa kwa matusi hapa ndio akili itakukaa sawa!
 
Maneno ya khanga.

Amekuwa mbunge zaidi ya miaka 20, lakini mara karibia zote alishinda uchaguzi kwa ghiliba. Kama aliweza kushinda kwa ghiliba mara zote hizo akiwa waziri, atashindwaje kushinda kwa ghiliba leo akiwa na madaraka yote ya kuamrisha tume ya uchaguzi na vyombo vya dola?
 
Kwa mfumo wa TZ ni ngumu kwa Rais anaegombea kipindi cha pili kushindwa! Inawezekana kushindwa kwenye uchaguzi kipindi cha kwanza lkn si anapotaka kurudi kwa mara ya Pili na hii sio kwa Magu yeyote atakaekuwa madarakani mpk mfumo utakapobadilishwa.
 
wakulima wa korosho kutoka huko vijijini wameshalipwa fedha zao zote?
 
Kama hana hofu ya kushindwa mbona mna weka mazingira magumu ya uchaguzi ?!. Weka tume huru uone kama hawezi kushindwa .

Atarudi madarakani si kwa sababu za kupendwa au kazi zake. Bali kwa kubebwa na vyombo vya dola na vya maamuzi
 
Boya kweli we nyumbu wa kijani plus kamongo mchanga.
 
MBUNGE wa Same Magharibi amewaeleza wapiga kura wake mambo makubwa ambayo Rais Magufuli anayafanya kwa watanzania ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi CCM.

 
Daaah ni mbunge wangu hapo kaenda vijijini kabisa maana mjini aliita mkutano watu wakagoma kuja akasusa jumla
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…