Mafanikio ya Wanaijeria kwenye muziki

Mafanikio ya Wanaijeria kwenye muziki

Jr Xavi Hernandez

Senior Member
Joined
Feb 25, 2022
Posts
182
Reaction score
261
Mwaka jana kwao ulikuwa mwaka wa mafanikio makubwa kwa wasanii wao. Walikuwa wamefanya makubwa kimataifa kupitia Album zao ambazo zilikuwa na mauzo makubwa(mfano Made in Lagos ya Wizkid) Single zao zilienda mbali sana(Essence ya Wizkid imeuza Double Platinum. sio masihara tena ndani ya Marekani.

Hakuna single ya Afrika yoyote iliyowahi kufanya hivyo siku za nyuma. Baadae Kina Burna Boy wakafanya kazi na kina Sia,Justin Biber,John Legend. Ndio kwanza mwezi wa 3 mwaka huu mpya tayari Muziki wa Nigeria unaendelea ulipoishia tena umeongeza kasi zaidi. Tayari Peru ya Fireboy ft Ed Sheeran imefanya vizuri mno,kwenye mauzo kwenye Chats mbali mbali za Uingereza moja kati ya hit kali mno.

Vipi kuhusu lile goma la Ckay? Tayari Mkongwe Maddona amethibitisha Remix ya ngoma yake akiwa amefanya na Fireboy. Wiz Khalifa kupitia Instagram ametuambia ameshamaliza kuandaa kete moja nzito akiwa na Star Boy Wizkid. Omah Lay ft Justin Biber tayari na Biber amethibitisha kupitia Instagram yake(ijumaa hii mzigo unaachiwa) Doh...Huyu Skibii ft Tory Lanz nayo collabo hiyo ikiwa imekamilika.

Burna Boy yupo kwenye maandalizi ya Album yake mpya. Davido anakwenda O2 Arena kwaajiri ya show. Bado hajaanza kazi kimataifa(hajawahi kukosea kimataifa huyu huwa anaachia hit pia) Hawa wanaigeria[emoji119][emoji119]

#Forgive Me
 
Upuuzi kusifia wa nje bila kujenga hoja jinsi wetu wanavyoweza nao hata kuwazidi
 
Miaka mitatu nyuma diamond alikua kwenye level moja na wakina Wizkid, davido na burnaboy ila mpaka sasa hawa jamaa wamemuacha mbali sana ,sasahiv anakazi ya kupambana na wakina ruger ,rema,joeboy, fireboy, ckay, jaywizzy n.k
kikubwa amenunua rolls royce ya 1.5bln.
 
Back
Top Bottom