jebs2002
JF-Expert Member
- Sep 3, 2008
- 9,604
- 8,812
Kudos mkuu, sidhani kama tumelala, nadhani tuko kwenye "coma"! Kuzinduka kwetu hakujulikani, kila Idara, Taasisi na Wizara ya Utalii na Mawasilianp iko hovyo kabisa, kuanzia Dinosaur wao Prof wa jina Maghembe mpaka mfagiaji, wao kujigamba gamba tu wamesoma na kuona mengi nje, kuyafanya hapa hakuna lolote, zaidi sana watawapa tenda matapeli wa kibongo ulaya, na ilishatokea UK, hela za ukweli zilitafunwa kwa kisingizio cha kuitangaza TZ, huyu jamaa aliyefanya haya yupo mjini, ndio kwanza anaonekana kama mwekezaji kumbe fisadi tu wa hela za mlalahoi, huu uozo sijuwi kaka utaisha lini...Bodi ya Utaliii imelala usingizi.