platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,424
- 11,320
Nimestuka kidogo ndiyo maana nimeleta kama swali.
Inaeleweka kuwa umiliki wa KQ umegawanywa kwa GOK, KLM, KG lenders na public. Na inaeleweka kuwa si lazima shirika la ndege liwe na ndege zake lenyewe ili kujiendesha, linaweza ku-lease na biashara ikaendelea.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka baadhi ya Wabunge na vyombo vya habari wanasema ndege nyingi za shirika la Ndege Kenya zinamilikiwa kwa siri na Wanasiasa au vigogo Serikalini. Hii haihusiani na ndege ambazo huwa tunaambiwa kwamba zimekuwa leased, hizi ni zile miongoni mwa ndege zinazosemwa zinamilikiwa na KQ. Ina maana kuwa kuna 'wajanja' huwa wanachukua chao mapema ndiyo maana Shirika likiyumba linapewa bail out.
Link hapo chini ya gazeti la Daily post imemnukuu Mwenyekiti wa kamati ya uwekezaji akishangazwa kuwa kumbe katika ndege 28 zinazofanya kazi ni ndege tatu tu ndiyo za KQ nyingine za 'cartels', politicians etc.
http://www.kenyan-post.com/2019/02/shock-as-it-emerges-kq-own-3planes.html
NB: Habari nyingine ni kuwa Mwenyekiti wa bodi ya Kenya Aviation AUTHORITY pia ni Mwenyekiti wa bodi ya Commercial Bank of Kenya ambayo inamilikiwa na familia ya Kenyatta.
Kuna Watu wanakula mema ya Nchi duh!
Inaeleweka kuwa umiliki wa KQ umegawanywa kwa GOK, KLM, KG lenders na public. Na inaeleweka kuwa si lazima shirika la ndege liwe na ndege zake lenyewe ili kujiendesha, linaweza ku-lease na biashara ikaendelea.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka baadhi ya Wabunge na vyombo vya habari wanasema ndege nyingi za shirika la Ndege Kenya zinamilikiwa kwa siri na Wanasiasa au vigogo Serikalini. Hii haihusiani na ndege ambazo huwa tunaambiwa kwamba zimekuwa leased, hizi ni zile miongoni mwa ndege zinazosemwa zinamilikiwa na KQ. Ina maana kuwa kuna 'wajanja' huwa wanachukua chao mapema ndiyo maana Shirika likiyumba linapewa bail out.
Link hapo chini ya gazeti la Daily post imemnukuu Mwenyekiti wa kamati ya uwekezaji akishangazwa kuwa kumbe katika ndege 28 zinazofanya kazi ni ndege tatu tu ndiyo za KQ nyingine za 'cartels', politicians etc.
http://www.kenyan-post.com/2019/02/shock-as-it-emerges-kq-own-3planes.html
NB: Habari nyingine ni kuwa Mwenyekiti wa bodi ya Kenya Aviation AUTHORITY pia ni Mwenyekiti wa bodi ya Commercial Bank of Kenya ambayo inamilikiwa na familia ya Kenyatta.
Kuna Watu wanakula mema ya Nchi duh!