Mafundi wa Kitanzania badilikeni

Mafundi wa Kitanzania badilikeni

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Hapa nitaongea kwa ufupi sana na hii mada inawahusu mafundi wa aina zote hasa wale wanaokuja majumbani au maofisini kufanya matengenezo fulani kuanzia mafundi ujenzi, wapakaji rangi, fundi umeme hadi fundi wa maji.

Kuna mambo mawili ambayo yanakera sana ambayo wanafanya mafundi wa Kitanzania.

Kwanza, ni ishu ya kutofanya usafi baada ya kumaliza kazi. Mafundi wetu hawa hawadhani kuwa ni wajibu wao kuacha pasafi mazingira waliyofanyia kazi. Hili nimeliona hata kwa wale ninaodhani watakuwa wamepitia mafunzo. Nashauri vyuo vya ufundi vifundishe na kusisitiza utaratibu sahihi wa fundi kufanya kazi iliwemo kuacha mazingira safi baada ya kazi.

Pili, ni suala la kuondoka na vifaa vya mteja. Anaweza kuja kubadili au kufix kitu fulani, akimaliza kazi wengi wana tabia ya kuchukua kifaa alichobadilisha. Usipokuwa makini, kama siyo kifaa chote basi kuna kitu alichobadili atabeba bila kuomba au kutoa taarifa.

Kwa leo nitagusia hayo tu.
 
Pili, ni suala la kuondoka na vifaa vya mteja. Anaweza kuja kubadili au kufix kitu fulani, akimaliza kazi wengi wana tabia ya kuchukua kifaa alichobadilisha. Usipokuwa makini, kama siyo kifaa chote basi kuna kitu alichobadili atabeba bila kuomba au kutoa taarifa.
hili swala linakera kweli
mafundi ni wezi
 
Kingine tabia za mafundi ukipeleka kitu jitahidi uwepo la sivyo atatoa vitu vizuri vizuri ataweka vibovu kingine mafundi ujenzi ndio shida sana bila usimamizi utapigwa mifuko ya simenti mpaka unyooshe maelezo kiufupi mafundi wa kibongo ni shida tu
 
Hapa nitaongea kwa ufupi sana na hii mada inawahusu mafundi wa aina zote hasa wale wanaokuja majumbani au maofisini kufanya matengenezo fulani kuanzia mafundi ujenzi, wapakaji rangi, fundi umeme hadi fundi wa maji.

Kuna mambo mawili ambayo yanakera sana ambayo wanafanya mafundi wa Kitanzania.

Kwanza, ni ishu ya kutofanya usafi baada ya kumaliza kazi. Mafundi wetu hawa hawadhani kuwa ni wajibu wao kuacha pasafi mazingira waliyofanyia kazi. Hili nimeliona hata kwa wale ninaodhani watakuwa wamepitia mafunzo. Nashauri vyuo vya ufundi vifundishe na kusisitiza utaratibu sahihi wa fundi kufanya kazi iliwemo kuacha mazingira safi baada ya kazi.

Pili, ni suala la kuondoka na vifaa vya mteja. Anaweza kuja kubadili au kufix kitu fulani, akimaliza kazi wengi wana tabia ya kuchukua kifaa alichobadilisha. Usipokuwa makini, kama siyo kifaa chote basi kuna kitu alichobadili atabeba bila kuomba au kutoa taarifa.

Kwa leo nitagusia hayo tu.
Kanuni ni ileile kila mtu anakula kwa urefu wa kamba yake..
Watanzania wote ni wezi tunapishana uwezo tu.
 
Hapa nitaongea kwa ufupi sana na hii mada inawahusu mafundi wa aina zote hasa wale wanaokuja majumbani au maofisini kufanya matengenezo fulani kuanzia mafundi ujenzi, wapakaji rangi, fundi umeme hadi fundi wa maji.

Kuna mambo mawili ambayo yanakera sana ambayo wanafanya mafundi wa Kitanzania.

Kwanza, ni ishu ya kutofanya usafi baada ya kumaliza kazi. Mafundi wetu hawa hawadhani kuwa ni wajibu wao kuacha pasafi mazingira waliyofanyia kazi. Hili nimeliona hata kwa wale ninaodhani watakuwa wamepitia mafunzo. Nashauri vyuo vya ufundi vifundishe na kusisitiza utaratibu sahihi wa fundi kufanya kazi iliwemo kuacha mazingira safi baada ya kazi.

Pili, ni suala la kuondoka na vifaa vya mteja. Anaweza kuja kubadili au kufix kitu fulani, akimaliza kazi wengi wana tabia ya kuchukua kifaa alichobadilisha. Usipokuwa makini, kama siyo kifaa chote basi kuna kitu alichobadili atabeba bila kuomba au kutoa taarifa.

Kwa leo nitagusia hayo tu.
Vyuo vyote vya ufundi somo la kwanza kabisa ni usalama sehemu ya kazi, usalama wako wewe fundi usalama wa vifaa vyako na usalama wa kazi unayo fanya.
Sambamba na hilo ni usafi, kwanza usafi wako wewe na vifaa vyako usafi wa kazi yako na usafi wa eneo la kazi.
Kuanza usafi kabla ya kazi na baada ya kazi ni kanuni namba moja ya fundi.
 
siwezi kupiga deki sehemu smbayo nmefnya kaz kama kuna uchafu mwmgi ntatpa tu sio kusafsha hyo n kaz yako
 
Umetumia lugha stahiki bila kupepesa maçho...
Ni wezi full stop...
Juzi hapa wamenipiga kokoto kile Kiloli kidogo kokoto nyeusi, jamaa wamekuja wakamwaga chap, bila kunipa nafasi kukagua!, kikijaa inakuwa laki 2, lakini mafundi wezi wanawaambia niwekee za laki na sabini, wanalamba 30, na wakifika site wanamwaga haraka ili usistuke.
 
Shida ya Tanzania watu wengi wamejikuta kwenye hizo kazi sababu ya njaa.

Elimu tunayoitoa kwenye taaluma mbalimbali haiko sawa matokeo yake tunazalisha wataalam wenye vyeti na ufaulu mzuri lakini sio watu competent wenye uelewa wa walichosomea

Hatuna mifumo ya kusajili watu kwenye hizi taaluma na kuwapa certifications na kuwa registered kwenye bodi mbalimbali.
 
Mi pia hiyo tabia siipendi, fundi anakuja kubadili kitambaa cha kochi anabeba alivyotoa kama vile mali yake.

Kuna mmoja alikuja kuweka wall paper gundi yangu, kamaliza kazi akabeba yote iliyobaki kama vile robo tatu li wall paper lenyewe wiki tu likabanduka....aliniudhi sana. Mxyuuuu
 
Back
Top Bottom