Magari aina ya BMW na Mercedez Benz huwa na matatizo gani?

Magari aina ya BMW na Mercedez Benz huwa na matatizo gani?

Hata Benz C class Zipo na Tabia Kama hizi???
Ukweli c-class sijui zikoje, lakini all german cars wana complicate mambo, usishangae betrinya mercedez ukaikuta chini ya siti ya dereva. My bro alinunua merc nimesahau model ipi kama coupe flani ndogo ivi, nikamwambia asiilete kabisa, akanunua yeye, haikufika wiki ngoma ikaanza kumbumia, matatizo madogo tu lakini repair cost yake ilikuwa kama £300 ivi na icho ni kitu kidogo sana tu kilikuwa. Kuna c class hizi za 2007 kuendelea niliona jamaa ana repair one shock up kwa dola 1000, hio ni 1 shock up tu, afu ndo jamaa yupo USA bara ziko bomba, merc,bmw,audi, sio kwa ajili ya daily driving uku kwetu, utumie weekend tu kula bata. Newest model wameimprove engine reliability, lakini still complications ndo zile zile. Hawa jamaa gari zao zina shida kwa sababu ya izi complications tu, lakini kama wamgekuwa wanafuata wajapan, gari zao usingeweza kucompare na yoyote ile, mana wanajua kukufurahisha
 
Kuna jirani yangu ana 745li kila nikimuona anapita nywele zina nisimama japo mara zote nanyoa kipara.
Yuko vizuri huyo, muhimu kwenye gari yoyote ni maintaincance lakini kuna common issues na hasa 745 za 2002, kesi nyingi water leak, idrive, na gearbox kugoma kubadili gear, na hii yote ni kwa sababu haya magari kutwa yapo under electronic input, sensor moja tu ikigoma mara gari inachanganyikiwa, na gari zao ukiidharau taa ya check engine utakuja kujuta. Mana utasema izi gari makusudi wamezipanga ziharibike na kusumbua zikifika km fulani. Ukiingia beforward 7 series unazikuta cheap mpaka unashangaa kweli hii BMW? Lakini value yake imeshuka kwa sababu repair costs doesnt make sense at all. Mi nshapanga ipo siku nitanunua japo hio ya 2002-3-4 engine ikisumbua, unashusha unaweka V8 ya toyota tu lakini unabakisha control box ya bimmer kwa ajili ya features za bmw na control box ya toyota kushughulikia engine tu.
 
Yuko vizuri huyo, muhimu kwenye gari yoyote ni maintaincance lakini kuna common issues na hasa 745 za 2002, kesi nyingi water leak, idrive, na gearbox kugoma kubadili gear, na hii yote ni kwa sababu haya magari kutwa yapo under electronic input, sensor moja tu ikigoma mara gari inachanganyikiwa, na gari zao ukiidharau taa ya check engine utakuja kujuta. Mana utasema izi gari makusudi wamezipanga ziharibike na kusumbua zikifika km fulani. Ukiingia beforward 7 series unazikuta cheap mpaka unashangaa kweli hii BMW? Lakini value yake imeshuka kwa sababu repair costs doesnt make sense at all. Mi nshapanga ipo siku nitanunua japo hio ya 2002-3-4 engine ikisumbua, unashusha unaweka V8 ya toyota tu lakini unabakisha control box ya bimmer kwa ajili ya features za bmw na control box ya toyota kushughulikia engine tu.
Ukweli mtupu, nilikua na vw touran ilikuja taa ya check engine inawaka toka Japan ilinitesa Ile gari siwezi sahau. Gearbox, mara sensor, shock ups nk,, ilikua inakaa garage kuliko home. Nikachukia kila kitu kuhusu gari za mjerumani isipokua bima 7 series.
 
Jamani kuna Audi A4 nataka chukua lakini sina ujuzi sana na hizi gari. Specifications ni hizi;
Chassis# WAUZZZ8E44A275112
model Code: GH-8EALT
version: 2.0
Engine Code: ALT

Nahitaji kufahamu kuhusu hayo hapo juu.
Pita Google mkuu check review za hiyo gari kutoka mwaka iliyotengenezwa. Pia check YouTube nk
 
Hivi vipi kuhusu bmw x3? Au SUV similar? Naitamani sana ila ndio woga wa usilolijua....tumpumzishe mjapan na rav4/suzuki zake.
 
Hivi vipi kuhusu bmw x3? Au SUV similar? Naitamani sana ila ndio woga wa usilolijua....tumpumzishe mjapan na rav4/suzuki zake.
X3 iko poa mkuu, hizi kama una hela ya kuweza kununua spare parts, service unafanya on time na una peleka kwa fundi anaezijua kuzitengeneza hazina shida.
 
Unaongea lak350 mi nina Nissan hardbody double cab shock ya monoroe mkuu juzi nimeweka 4set 2.2m moja laki5 nusu
Benz maintenance take ipo juu mkuu. Shocks peke ake ya bei ya chini ni 400-600 laki hii naongelea C class.
Ukija Benz kama S class shock take unapata kwa 2.5 mil each.
Hii ni moja ya sababu watu wanakimbia hizi gari ila in nzuri sana kwa upande mwingine maana ukifunga spare unasahau.
Nakaribisha maswali zaid nitajitolea kuyajibu kuhusu gari hizi.
 
Nina BMW SUV hapa. Sijaona gharama zake. Labda kwa sababu lipo kwenye warranty na maisha yangu kiaina fulani ni ya gharama (kwa mtizamo wa Mtanzania "wa kawaida", this is a relative matter) kwa hiyo naona kawaida.Majuzi nimebadili matairi mawili (run-flat) nimelipa $620, including tax.

Unaweza kupata matairi kwa nusu ya bei hiyo kama huna run flat, kwa hiyo hiyo bei ya juu isikutishe sana.

Sasa kama hujawa na uwezo kama huo, na unataka kununua tu BMW au Benz uonekane, lazima uone kizunguzungu.

Tena kwa sasa nimelichoka nasubiri lichoke kidogo tu nichukue Porsche Macan S au Range Rover Sport.

Maisha mafupi, make money, spend money.

cc Nyani Ngabu johnmlay
 
Range rover sport hadi kufika dar port ina cost tshs ngapi?
 
Back
Top Bottom