Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo kupitia idara ya Maelezo leo inatarajiwa kutoa tamko kuhusu mwelekeo wa uandishi wa vyombo vya habari kufuatia malumbano na migongano ya maneno yenye kuashiria kuvunjika kwa maadili ya kiundishi hususan kuingilia habari za kibinafsi za maisha ya watu jambo ambalo linaonekana kuanza kuwakera viongozi mbalimbali. Pamoja na serikali baraza la vyombo vya habari nchini (MCT) nalo linatarajiwa kutoa tamko katika kile kinachoonekana kuitikia wito wa mmiliki wa vyombo vya IPP aliotoa juzi kwenye taarifa yake kwa vyombo vya habari kuhusu madai ya kuzushiwa habari mbalimbali za uongo.
Matamshi hayo ambayo yanatarajiwa kutolewa muda si mrefu ujao yanatarajiwa kutoa maangalizo kuhusu haja ya vyombo vya habari kuheshimu uhuru wa watu na maadili ya jamii yetu.
Msimamo wa KLHN ni kuwa uamuzi huo wa kutoa matamko umechelewa na inaonekana unakuja baada ya moto wa malumbano hayo kuanza kuunguza pabaya. Siku za hivi karibuni magazeti mbalimbali ambayo yanadaiwa kuwa na watu wakubwa nyuma yake yamekuwa yakitumika kurushiana madongo, kashfa, uzushi na madai ambayo kwa mtu yeyote mwenye akili timamu ataona kuwa yana walakini.
Kwa muda mrefu tumeandika na kupiga kelele kuhusu suala hili na hata katika kijarida chetu cha Cheche tumelitolea maoni jambo hili tena. Tunasikitishwa kuwa kwa muda mrefu serikali imekaa kimya ikiangalia na kukodolewa uchafuzi wa hewa ya habari nchini ambapo watu wachache wenye nguvu za kisiasa na kiuchumi wamewageuza watanzania kuwa vikaragosi vyao kwa kuwatupia kila aina ya habari huko wao wenyewe wakitengeneza mamilioni ya fedha. Tunasikitika kuwa kwa muda mrefu baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika kinyume na kundi moja huku vikiamini kuwa vina kinga na baraka ya watawala.
Licha ya kutambua mabadiliko yaliyotokea siku chache zilizopita ambapo vyombo vingine vimeibuka kuanza kujibu mapigo, tunasikitika kuwa kuna watu wameona kuwa jambo hilo ni la lazima baada ya serikali kukaa kimya kwa muda mrefu bila ya kuchukua hatua. Wakati serikali haikuweza kuvumilia mara tatu suala la MwanaHalisi na habari ya kumng'oa Rais Kikwete, kwenye masuala haya ya vitandani mwa watu na kwenye vyumba vya watu yamevumiliwa kwa muda mrefu kana kwamba hakuna utawala wa sheria nchini.
Wito wetu leo siyo tu kwenye masuala haya ya watu binafsi wanaogombana kupitia vyombo vya habari bali pia vyombo vile ambavyo vinatumika kutangaza habari za kingono na mambo ya ufuska kama kwa kuyatukuza huku vikiweka picha mbalimbali ambazo ni wazi zinavunja kanuni za Adhabu na sheria mbalimbal zinazohusiana na masuala ya uchapishaji, utangazaji n.k
Haitoshi kwa serikali leo kutoa matamko ya kumuonya mtu au kukemea, tunachotarajia ni kuona serikali ikichukua hatua madhubuti ya kufungia vyombo vyote vya habari ambavyo vimevuka mpaka wa maoni huru na kuwa katika eneo la kukashfiana na kuharibu maadili ya watoto (deliquency of minors). Tunatumaini kama serikali inaona kuwa mambo yanayofanywa ni sehemu ya uhuru wa maoni au habari, basi wakati umefika kwa serikali kuanzisha sera na hatimaye sera itakayoratibu habari za kingono, filamu, na vitu kama hivyo kwa watu wazima ili vipatikane katika mazingira yanayotakiwa, vikiratibiwa na kusimaiwa kisheria kuliko ilivyo sasa ambapo badala ya kuita kuwa ni mambo ya kingono (pornography) tumeamua kuvipatia jina la "udaku".
Hata katika nchi ambazo wengi wetu tunaonekana kuziiga mambo ya kingono yanaongozwa na sheria sawia na majarida au magazeti yenye habari za namna hiyo hayapatikana kiurahisi au waziwazi kama ilivyo nchini. Tunarajia serikali itahakikisha kuwa watu wazima wanapata uhuru wa kuona na kusoma kile wanachotaka kwa mujibu wa sheria na ya kuwa watoto wetu na public square or airwaves haviharibiwi kwa kuacha kundi la watu wachache kutawala hadi kwenye macho na masikio yetu.
Tunachotarajia leo siyo maneno matupu, bali hatua kali na za mfano, ili hatimaye kwa kutumia sheria kulazimisha kina cha uandishi, habari za kuvutia, na maadili yanazingatiwa katika fani hii. Vinginevyo, kama wanachotaka ni kukemea "tabia iliyojitokeza" tumeona kuwa sisi tutanguliwe kuwakemea kwa uzembe na kufumbia macho uposhaji mkubwa wa maadili.
Matamshi hayo ambayo yanatarajiwa kutolewa muda si mrefu ujao yanatarajiwa kutoa maangalizo kuhusu haja ya vyombo vya habari kuheshimu uhuru wa watu na maadili ya jamii yetu.
Msimamo wa KLHN ni kuwa uamuzi huo wa kutoa matamko umechelewa na inaonekana unakuja baada ya moto wa malumbano hayo kuanza kuunguza pabaya. Siku za hivi karibuni magazeti mbalimbali ambayo yanadaiwa kuwa na watu wakubwa nyuma yake yamekuwa yakitumika kurushiana madongo, kashfa, uzushi na madai ambayo kwa mtu yeyote mwenye akili timamu ataona kuwa yana walakini.
Kwa muda mrefu tumeandika na kupiga kelele kuhusu suala hili na hata katika kijarida chetu cha Cheche tumelitolea maoni jambo hili tena. Tunasikitishwa kuwa kwa muda mrefu serikali imekaa kimya ikiangalia na kukodolewa uchafuzi wa hewa ya habari nchini ambapo watu wachache wenye nguvu za kisiasa na kiuchumi wamewageuza watanzania kuwa vikaragosi vyao kwa kuwatupia kila aina ya habari huko wao wenyewe wakitengeneza mamilioni ya fedha. Tunasikitika kuwa kwa muda mrefu baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika kinyume na kundi moja huku vikiamini kuwa vina kinga na baraka ya watawala.
Licha ya kutambua mabadiliko yaliyotokea siku chache zilizopita ambapo vyombo vingine vimeibuka kuanza kujibu mapigo, tunasikitika kuwa kuna watu wameona kuwa jambo hilo ni la lazima baada ya serikali kukaa kimya kwa muda mrefu bila ya kuchukua hatua. Wakati serikali haikuweza kuvumilia mara tatu suala la MwanaHalisi na habari ya kumng'oa Rais Kikwete, kwenye masuala haya ya vitandani mwa watu na kwenye vyumba vya watu yamevumiliwa kwa muda mrefu kana kwamba hakuna utawala wa sheria nchini.
Wito wetu leo siyo tu kwenye masuala haya ya watu binafsi wanaogombana kupitia vyombo vya habari bali pia vyombo vile ambavyo vinatumika kutangaza habari za kingono na mambo ya ufuska kama kwa kuyatukuza huku vikiweka picha mbalimbali ambazo ni wazi zinavunja kanuni za Adhabu na sheria mbalimbal zinazohusiana na masuala ya uchapishaji, utangazaji n.k
Haitoshi kwa serikali leo kutoa matamko ya kumuonya mtu au kukemea, tunachotarajia ni kuona serikali ikichukua hatua madhubuti ya kufungia vyombo vyote vya habari ambavyo vimevuka mpaka wa maoni huru na kuwa katika eneo la kukashfiana na kuharibu maadili ya watoto (deliquency of minors). Tunatumaini kama serikali inaona kuwa mambo yanayofanywa ni sehemu ya uhuru wa maoni au habari, basi wakati umefika kwa serikali kuanzisha sera na hatimaye sera itakayoratibu habari za kingono, filamu, na vitu kama hivyo kwa watu wazima ili vipatikane katika mazingira yanayotakiwa, vikiratibiwa na kusimaiwa kisheria kuliko ilivyo sasa ambapo badala ya kuita kuwa ni mambo ya kingono (pornography) tumeamua kuvipatia jina la "udaku".
Hata katika nchi ambazo wengi wetu tunaonekana kuziiga mambo ya kingono yanaongozwa na sheria sawia na majarida au magazeti yenye habari za namna hiyo hayapatikana kiurahisi au waziwazi kama ilivyo nchini. Tunarajia serikali itahakikisha kuwa watu wazima wanapata uhuru wa kuona na kusoma kile wanachotaka kwa mujibu wa sheria na ya kuwa watoto wetu na public square or airwaves haviharibiwi kwa kuacha kundi la watu wachache kutawala hadi kwenye macho na masikio yetu.
Tunachotarajia leo siyo maneno matupu, bali hatua kali na za mfano, ili hatimaye kwa kutumia sheria kulazimisha kina cha uandishi, habari za kuvutia, na maadili yanazingatiwa katika fani hii. Vinginevyo, kama wanachotaka ni kukemea "tabia iliyojitokeza" tumeona kuwa sisi tutanguliwe kuwakemea kwa uzembe na kufumbia macho uposhaji mkubwa wa maadili.
Last edited by a moderator: