Maghorofa 64 hatarini kuanguka Kariakoo

Maghorofa 64 hatarini kuanguka Kariakoo

Maghorofa 64 yaliyopo eneo la Kariakoo, Manispaa ya Ilala yamejengwa kinyume na sheria na kwamba baadhi yanaweza kuporomoka kutokana na ujenzi wake kuwa chini ya kiwango.

Kampuni iliyopewa zabuni ya kufanya ukaguzi wa majengo Manispaa ya Ilala, inayoitwa Design Plus Architects (DPA) imebaini kati ya majengo ya ghorofa 90 yaliyokaguliwa, 67 yamejengwa kinyume na sheria.

Uamuzi wa kuipa kampuni binafsi kazi ya kukagua majengo, ulikuja baada ya jengo la ghorofa 16 kuanguka na kuua watu 36 Machi 26, mwaka huu.

Meneja Uendeshaji wa DPA, Mustafa Maulid alisema jana kwamba ukaguzi wa majengo hayo ulianza Julai mwaka huu baada ya kupata zabuni hiyo.

“Hali ni mbaya katika majengo tuliyoyakagua, kuna majengo ya ghorofa yenye nyufa nyingi, pia yapo majengo yanayogusana ambayo ni hatari kwa watumiaji,” alisema.

Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa alipoulizwa hatua za kuchukua, alisema vikao vya madiwani vitaamua hatua za kuchukua baada ya kuipitia ripoti ya ukaguzi huo.

“Ukipita Kariakoo hata kama siyo mtaalamu wa ujenzi utagundua kwamba majengo mengi yamejengwa bila kufuata sheria za ujenzi, baada ya kuanguka kwa jengo katikati ya jiji, tukaamua kuipa kampuni binafsi kazi ya ukaguzi ili kuona ni majengo gani yapo kinyume na sheria,” alisema Silaa.

Akifafanua zaidi, Maulid alisema makosa waliyoyabaini ni watu kuendesha ujenzi bila kuwa na vibali.

Alisema makosa mengine ni ujenzi bila kufuata michoro iliyoidhinishwa na Manispaa ya Ilala.

“Hii ina maana kwamba watu wanajenga majengo tofauti na michoro inayotoka kwa wataalamu wa manispaa. Kwa mfano majengo yote Kariakoo yanatakiwa kuwa na maegesho ya magari lakini wao wanaweka flemu za maduka,” alisema Maulid.

Pia, alisema watu wanahamia kwenye maghorofa kabla hayajaisha kitendo ambacho ni kinyume na sheria.

Kuhusu changamoto walizokutana nazo, Maulid alisema baadhi ya wamiliki wa nyumba walikuwa wakiwazuia kuingia kufanya ukaguzi, huku wengine wakikimbilia kushtaki kwa wanasiasa.

Alisema wengine wamekuwa wakiwatishia kwa lengo la kuwazuia kufanya kazi hiyo na kwamba, wataendelea na kazi hiyo hadi wamalize.

CHANZO:Mwananchi.

MY TAKE:
Tusubiri janga lingine litokee alafu tume iundwe kuchunguza.

Hii ni moja ya matumizi bora kabisa ya kodi zetu!
Hayo majengo waliyoyabaini yana mapungufu yawekwe alama kabisa,tupite mbali nayo
 
Wataalamu wamesema, serikali ichukuwe hatua, tatizo kuna majengo ya wale watu "unanijua mimi ni nani?".
 
Na Mm nitaanzisha mada nikisema kiongozi fulani atakufa, halafu baada ya miaka 10 akifa watu waje waniite nabii kwa kutabiri hicho kifo.

Au

Nitabiri kuwa ipo siku simba itashinda kombe la ligi kuu halafu baada ya misimu miwili ashinde halafu mje mniite nabii
Are you dumb, stupid or dumb?
 
na mwaka mwingine litaanguka jingine kama hivi. toka 2013 kosa lilelile tena 2024.
 
Maghorofa 64 yaliyopo eneo la Kariakoo, Manispaa ya Ilala yamejengwa kinyume na sheria na kwamba baadhi yanaweza kuporomoka kutokana na ujenzi wake kuwa chini ya kiwango.

Kampuni iliyopewa zabuni ya kufanya ukaguzi wa majengo Manispaa ya Ilala, inayoitwa Design Plus Architects (DPA) imebaini kati ya majengo ya ghorofa 90 yaliyokaguliwa, 67 yamejengwa kinyume na sheria.

Uamuzi wa kuipa kampuni binafsi kazi ya kukagua majengo, ulikuja baada ya jengo la ghorofa 16 kuanguka na kuua watu 36 Machi 26, mwaka huu.

Meneja Uendeshaji wa DPA, Mustafa Maulid alisema jana kwamba ukaguzi wa majengo hayo ulianza Julai mwaka huu baada ya kupata zabuni hiyo.

“Hali ni mbaya katika majengo tuliyoyakagua, kuna majengo ya ghorofa yenye nyufa nyingi, pia yapo majengo yanayogusana ambayo ni hatari kwa watumiaji,” alisema.

Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa alipoulizwa hatua za kuchukua, alisema vikao vya madiwani vitaamua hatua za kuchukua baada ya kuipitia ripoti ya ukaguzi huo.

“Ukipita Kariakoo hata kama siyo mtaalamu wa ujenzi utagundua kwamba majengo mengi yamejengwa bila kufuata sheria za ujenzi, baada ya kuanguka kwa jengo katikati ya jiji, tukaamua kuipa kampuni binafsi kazi ya ukaguzi ili kuona ni majengo gani yapo kinyume na sheria,” alisema Silaa.

Akifafanua zaidi, Maulid alisema makosa waliyoyabaini ni watu kuendesha ujenzi bila kuwa na vibali.

Alisema makosa mengine ni ujenzi bila kufuata michoro iliyoidhinishwa na Manispaa ya Ilala.

“Hii ina maana kwamba watu wanajenga majengo tofauti na michoro inayotoka kwa wataalamu wa manispaa. Kwa mfano majengo yote Kariakoo yanatakiwa kuwa na maegesho ya magari lakini wao wanaweka flemu za maduka,” alisema Maulid.

Pia, alisema watu wanahamia kwenye maghorofa kabla hayajaisha kitendo ambacho ni kinyume na sheria.

Kuhusu changamoto walizokutana nazo, Maulid alisema baadhi ya wamiliki wa nyumba walikuwa wakiwazuia kuingia kufanya ukaguzi, huku wengine wakikimbilia kushtaki kwa wanasiasa.

Alisema wengine wamekuwa wakiwatishia kwa lengo la kuwazuia kufanya kazi hiyo na kwamba, wataendelea na kazi hiyo hadi wamalize.

CHANZO:Mwananchi.

MY TAKE:
Tusubiri janga lingine litokee alafu tume iundwe kuchunguza.

Hii ni moja ya matumizi bora kabisa ya kodi zetu!
 
Maghorofa 64 yaliyopo eneo la Kariakoo, Manispaa ya Ilala yamejengwa kinyume na sheria na kwamba baadhi yanaweza kuporomoka kutokana na ujenzi wake kuwa chini ya kiwango.

Kampuni iliyopewa zabuni ya kufanya ukaguzi wa majengo Manispaa ya Ilala, inayoitwa Design Plus Architects (DPA) imebaini kati ya majengo ya ghorofa 90 yaliyokaguliwa, 67 yamejengwa kinyume na sheria.

Uamuzi wa kuipa kampuni binafsi kazi ya kukagua majengo, ulikuja baada ya jengo la ghorofa 16 kuanguka na kuua watu 36 Machi 26, mwaka huu.

Meneja Uendeshaji wa DPA, Mustafa Maulid alisema jana kwamba ukaguzi wa majengo hayo ulianza Julai mwaka huu baada ya kupata zabuni hiyo.

“Hali ni mbaya katika majengo tuliyoyakagua, kuna majengo ya ghorofa yenye nyufa nyingi, pia yapo majengo yanayogusana ambayo ni hatari kwa watumiaji,” alisema.

Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa alipoulizwa hatua za kuchukua, alisema vikao vya madiwani vitaamua hatua za kuchukua baada ya kuipitia ripoti ya ukaguzi huo.

“Ukipita Kariakoo hata kama siyo mtaalamu wa ujenzi utagundua kwamba majengo mengi yamejengwa bila kufuata sheria za ujenzi, baada ya kuanguka kwa jengo katikati ya jiji, tukaamua kuipa kampuni binafsi kazi ya ukaguzi ili kuona ni majengo gani yapo kinyume na sheria,” alisema Silaa.

Akifafanua zaidi, Maulid alisema makosa waliyoyabaini ni watu kuendesha ujenzi bila kuwa na vibali.

Alisema makosa mengine ni ujenzi bila kufuata michoro iliyoidhinishwa na Manispaa ya Ilala.

“Hii ina maana kwamba watu wanajenga majengo tofauti na michoro inayotoka kwa wataalamu wa manispaa. Kwa mfano majengo yote Kariakoo yanatakiwa kuwa na maegesho ya magari lakini wao wanaweka flemu za maduka,” alisema Maulid.

Pia, alisema watu wanahamia kwenye maghorofa kabla hayajaisha kitendo ambacho ni kinyume na sheria.

Kuhusu changamoto walizokutana nazo, Maulid alisema baadhi ya wamiliki wa nyumba walikuwa wakiwazuia kuingia kufanya ukaguzi, huku wengine wakikimbilia kushtaki kwa wanasiasa.

Alisema wengine wamekuwa wakiwatishia kwa lengo la kuwazuia kufanya kazi hiyo na kwamba, wataendelea na kazi hiyo hadi wamalize.

CHANZO:Mwananchi.

MY TAKE:
Tusubiri janga lingine litokee alafu tume iundwe kuchunguza.

Hii ni moja ya matumizi bora kabisa ya kodi zetu!
Duh! Huu uzi ulipotezewa tangu 2013, ndiyo umekuja kufufuliwa mara tu baada ya matokeo kuanza kuonekana!!
 
Kama huu uzi una zaidi ya miaka 10 na haukupata wachangiaji,basi hata sisi tunastahili lawama coz tuliuignore pia,
Inawezekana hatukuona umuhimu wake kipindi hicho.

😀😀
Uzi wa mambo muhimu tofauti na siasa haupati wachangiaji wengi.
Ukiandika mambo ya ngono, ndoa na siasa utapata wachangiaji.
Zinafuata habari za Simba na Yanga.
Takwimu zinasema watatu kati ya wanne ni ......
 
Back
Top Bottom