Maghorofa 64 hatarini kuanguka Kariakoo

Maghorofa 64 hatarini kuanguka Kariakoo

Maghorofa 64 yaliyopo eneo la Kariakoo, Manispaa ya Ilala yamejengwa kinyume na sheria na kwamba baadhi yanaweza kuporomoka kutokana na ujenzi wake kuwa chini ya kiwango.

Kampuni iliyopewa zabuni ya kufanya ukaguzi wa majengo Manispaa ya Ilala, inayoitwa Design Plus Architects (DPA) imebaini kati ya majengo ya ghorofa 90 yaliyokaguliwa, 67 yamejengwa kinyume na sheria.

Uamuzi wa kuipa kampuni binafsi kazi ya kukagua majengo, ulikuja baada ya jengo la ghorofa 16 kuanguka na kuua watu 36 Machi 26, mwaka huu.

Meneja Uendeshaji wa DPA, Mustafa Maulid alisema jana kwamba ukaguzi wa majengo hayo ulianza Julai mwaka huu baada ya kupata zabuni hiyo.

“Hali ni mbaya katika majengo tuliyoyakagua, kuna majengo ya ghorofa yenye nyufa nyingi, pia yapo majengo yanayogusana ambayo ni hatari kwa watumiaji,” alisema.

Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa alipoulizwa hatua za kuchukua, alisema vikao vya madiwani vitaamua hatua za kuchukua baada ya kuipitia ripoti ya ukaguzi huo.

“Ukipita Kariakoo hata kama siyo mtaalamu wa ujenzi utagundua kwamba majengo mengi yamejengwa bila kufuata sheria za ujenzi, baada ya kuanguka kwa jengo katikati ya jiji, tukaamua kuipa kampuni binafsi kazi ya ukaguzi ili kuona ni majengo gani yapo kinyume na sheria,” alisema Silaa.

Akifafanua zaidi, Maulid alisema makosa waliyoyabaini ni watu kuendesha ujenzi bila kuwa na vibali.

Alisema makosa mengine ni ujenzi bila kufuata michoro iliyoidhinishwa na Manispaa ya Ilala.

“Hii ina maana kwamba watu wanajenga majengo tofauti na michoro inayotoka kwa wataalamu wa manispaa. Kwa mfano majengo yote Kariakoo yanatakiwa kuwa na maegesho ya magari lakini wao wanaweka flemu za maduka,” alisema Maulid.

Pia, alisema watu wanahamia kwenye maghorofa kabla hayajaisha kitendo ambacho ni kinyume na sheria.

Kuhusu changamoto walizokutana nazo, Maulid alisema baadhi ya wamiliki wa nyumba walikuwa wakiwazuia kuingia kufanya ukaguzi, huku wengine wakikimbilia kushtaki kwa wanasiasa.

Alisema wengine wamekuwa wakiwatishia kwa lengo la kuwazuia kufanya kazi hiyo na kwamba, wataendelea na kazi hiyo hadi wamalize.

CHANZO:Mwananchi.

MY TAKE:
Tusubiri janga lingine litokee alafu tume iundwe kuchunguza.

Hii ni moja ya matumizi bora kabisa ya kodi zetu!

Commercial set up zote, zilindwe kisheria na ujenzi wake usiwe tu wa class kubwa zenye janja janja.
Lazima team ziwe na competent people who will deliver.
Pengine hii report ilifanyiwa kazi, ila ngoja tuone tunaposimama leo baada ya kupita miaka 10.
 
Maghorofa 64 yaliyopo eneo la Kariakoo, Manispaa ya Ilala yamejengwa kinyume na sheria na kwamba baadhi yanaweza kuporomoka kutokana na ujenzi wake kuwa chini ya kiwango.

Kampuni iliyopewa zabuni ya kufanya ukaguzi wa majengo Manispaa ya Ilala, inayoitwa Design Plus Architects (DPA) imebaini kati ya majengo ya ghorofa 90 yaliyokaguliwa, 67 yamejengwa kinyume na sheria.

Uamuzi wa kuipa kampuni binafsi kazi ya kukagua majengo, ulikuja baada ya jengo la ghorofa 16 kuanguka na kuua watu 36 Machi 26, mwaka huu.

Meneja Uendeshaji wa DPA, Mustafa Maulid alisema jana kwamba ukaguzi wa majengo hayo ulianza Julai mwaka huu baada ya kupata zabuni hiyo.

“Hali ni mbaya katika majengo tuliyoyakagua, kuna majengo ya ghorofa yenye nyufa nyingi, pia yapo majengo yanayogusana ambayo ni hatari kwa watumiaji,” alisema.

Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa alipoulizwa hatua za kuchukua, alisema vikao vya madiwani vitaamua hatua za kuchukua baada ya kuipitia ripoti ya ukaguzi huo.

“Ukipita Kariakoo hata kama siyo mtaalamu wa ujenzi utagundua kwamba majengo mengi yamejengwa bila kufuata sheria za ujenzi, baada ya kuanguka kwa jengo katikati ya jiji, tukaamua kuipa kampuni binafsi kazi ya ukaguzi ili kuona ni majengo gani yapo kinyume na sheria,” alisema Silaa.

Akifafanua zaidi, Maulid alisema makosa waliyoyabaini ni watu kuendesha ujenzi bila kuwa na vibali.

Alisema makosa mengine ni ujenzi bila kufuata michoro iliyoidhinishwa na Manispaa ya Ilala.

“Hii ina maana kwamba watu wanajenga majengo tofauti na michoro inayotoka kwa wataalamu wa manispaa. Kwa mfano majengo yote Kariakoo yanatakiwa kuwa na maegesho ya magari lakini wao wanaweka flemu za maduka,” alisema Maulid.

Pia, alisema watu wanahamia kwenye maghorofa kabla hayajaisha kitendo ambacho ni kinyume na sheria.

Kuhusu changamoto walizokutana nazo, Maulid alisema baadhi ya wamiliki wa nyumba walikuwa wakiwazuia kuingia kufanya ukaguzi, huku wengine wakikimbilia kushtaki kwa wanasiasa.

Alisema wengine wamekuwa wakiwatishia kwa lengo la kuwazuia kufanya kazi hiyo na kwamba, wataendelea na kazi hiyo hadi wamalize.

CHANZO:Mwananchi.

MY TAKE:
Tusubiri janga lingine litokee alafu tume iundwe kuchunguza.

Hii ni moja ya matumizi bora kabisa ya kodi zetu!
Muda huu hapa kariaakoo mh rais kagusia ripoti hii..
Ahsante mama ifanyiwe kazi sasa.
 
Tuseme ukiingia ghorofa lolote kariakoo, utakapotoka ndio ujue upo salama. Hakikisha simu yako imejaa charge.
 
Muda huu hapa kariaakoo mh rais kagusia ripoti hii..
Ahsante mama ifanyiwe kazi sasa.
Wengi hamkumuelewa alipoigusia hiyo ripoti.
Hapo alikuwa anawakumbusha wafanyabiashara na wamiliki kukichangia Chama kama ilivyo kwenye makubaliano ya kutoyabomoa maghorofa hayo.
Inaaonekana wengi walijisahau au waliamua kuwa wakaidi, hivyo alichokifanya mheshimiwa rais ni kuwakumbusha kwamba ile list bado ipo na imeongezeka zaidi sababu wanawajua wote waliojenga chini ya viwango.
Hivyo ilikuwa ni kuwakumbusha wajibu wao kwa Chama kuhakikisha kina hela na kinashinda hasa kipindi hiki mnapoelekea kwenye uchaguzi mkuu.

System inapokupendelea kuwa makini, wakati wewe unajiona umeiweka mfukoni, wao lengo lao ni kukutia ubovu, kukupaka madoa, kukudhoofisha ili baadaye waje kuku blackmail.
 
November 2013 ikapita.

November 2024 ikapita.

Ikatolewa order ripoti ya 2024 iandikwe hatujui hadi sasa iko wapi.

Nayo itapita tena hadi jengo lingine lidondoke na kuleta maafa ndio wataibuka kujidai wameumizwa.

Watajidai kutoa michango kugharamia majeruhi na waliofariki na kutoa mahitaji ya kijamii.

Mwezi wa 3 sasa kimya kama halikutokea janga kubwa tu.

Halafu itapita tena.
 
Tatizo njaaa ndo zimekithiri kwa wabongo maaana kama n miezi mi3 imepita na bado wamiliki wa majengo hawana time ya kifanyia tathmini majengo yao tutakufa2 maaana Hawa wamiliki wapo na jambo moja2 kuchimba underground Ili waongeze frem kwo hili haliwezi Isha otherwise kiama kisimame
 
Ma engineer wakaguzi wa manispaa waliokua wanaidhinisha kila hatua ya ujenzi washitakiwe.
 
Back
Top Bottom