Magoli ya Simba kwa Stand Utd ni mepesi sana, nini kipo nyuma ya pazia?

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Mtanange wa leo wa ligi kuu bara, uliopigwa katika dimba la Kambarage pale Shinyanga, Simba ameibuka na ushindi wa goli 2-0. Hongereni kwa hilo.

Ila kuna kitu kinanipa mashaka, magoli waliyofunga ni marahisi sana, yaani wamerahisishiwa namna ya kupata magoli hayo, kwa kifupi ni kama kupigana na mlevi aliyepo chakari.

Goli la kwanza ni la penati. Mpira umemgusa mchezaji wa Stand begani, refarii akakimbilia kutenga tuta, na John Bocco akafunga.

Goli la pili, offside ya wazi kabisaaaaa, John Bocco alibaki pekee yake na kipa halafu yule kipa sikuelewa ni kwa namna gani mpira uliompitia karibu ashindwe walau hata kuugusa. INASHANGAZA!

Inaonekana Simba kwa sasa wanapeleka miamala pande mbili, kwa wasimamizi wa mchezo bila kusahau kwa mabeki na magolikipa wa timu pinzani. Hebu kumbuka walau goli la faulo alilofungwa kipa wa Lipuli juzi, ni AIBU.

Mpira wetu bado una safari ndefu sana.

Nawasilisha...
 
Goli ni goli tu mzee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
stand walipwe stahiki zao,,, full stop.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vitendo vya rushwa ni vingi ila watendaji wa TAKUKURU no mpaka Mamlaka iseme shida tupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…