SoC01 Magonjwa ya Afya ya akili yanatibika, vunja ukimya

SoC01 Magonjwa ya Afya ya akili yanatibika, vunja ukimya

Stories of Change - 2021 Competition

Baba Swalehe

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2017
Posts
20,178
Reaction score
39,641
" Daktari huwezi kuelewa ntakachokuambia bora nife nacho " yalikua ni maneno ya mgonjwa wangu niliyekua namhudumia kwa muda mrefu , niligundua ana matatizo zaidi yanayopelekea afya yake kudhorota siku baada ya siku

Afya ya akili kwa kimombo (mental health) ni swala ambalo limekua likichukuliwa kwa mzaha katika jamii zetu za kiafrika , ukisikia kuhusu afya ya akili ndugu msomaji akili yako lazima itakupeleka moja kwa moja kuwaza " UKICHAA " .

Afya ya akili sio ukichaa , afya ya akili ni uwezo wa akili mtu kufanya vitu kwa usahihi , kufikiri kwa usahihi , kutenda kwa usahihi , Ni uwezo wa ubongo kuchanganua mambo na kuyafanya kwa usahihi, mtu unaweza usiwe kichaa lakini hutendi kwa usahihi au hufikiri kwa usahihi . Unawaza kufa tu kila saa unawaza dunia yote imekutenga hayo yanaweza kuwa ni mawazo yako lakini sio sahihi

Ubongo wa binadamu umetengenezwa kwa namna ya tofauti sana tatizo lolote linaloweza kutokea kwenye ubongo linaweza kupelekea matatizo mengine mengi kwenye viungo vingine vya mwili unachukua asilimia mbili tu ya uzito wa mwili mzima lakini asilimia ishirini ya nishati nzima ya mwili inapelekwa kwenye ubongo, wanasayansi bado tunajaribu kuchunguza uhusiano wa matatizo ya akili na reaction mbali mbali zinazotokea kwenye ubongo lakini kwa uchache (nitatumia lugha rahisi ili kila mtu hata asiyesoma sayansi afahamu) naweza kusema matatizo mengi ya afya ya akili yanatokana na kukosekana kwa uwiano katika kemikali mbalimbali za saketi kwenye ubongo (neurones) mfano wa kemikali hizo ni serotonini na neuroepinephrine (nimekosa neno lake la kiswahili ).

Hizi nyuroni huwasiliana zenyewe kwa zenyewe na katika kuwasiliana hutumia kemikali nilizozitaja hapo juu na zingine nyingi inapotokea hakuna uwiano wa kemikali ndipo hapo mtu tunasema ubongo wake umepata shida na hafanyi mambo kwa usahihi mfano kunapokua na utengenezwaji mwingi wa kemikali ya dopimine katika saketi za ubongo hapo ndipo tunasema mtu ana ukichaa uliopitiliza( psychosis) , ndo hawa tunawaona wanaokota makopo kwenye mabarabara.

Kwa mtu mwenye msongo mkubwa wa mawazo inamaanisha kemikali za serotonini zinatengenezwa kwa kiwango kichache sana katika nyuroni zake za ubongo , serotonini sisi wataalamu wa afya hupenda kuiita " kemikali ya furaha" sababu ikipungua furaha ya mtu hupungua na hata hamu ya kula hupungua.

Kwa hiyo ubongo ni kama kiungo chochote kila kwenye mwili kwamba na chenyewe kinaweza kuumwa na kinaweza pata ajali hata maneno tu yanaweza kufanya ubongo upate ajali mfano unatukanwa au unadhalilishwa na mtu unayempenda kila siku na shida kubwa inakuja kwamba ubongo ndo unaongoza ogani zingine za mwili hivyo unapopata shida ogani zingine zitadhurika pia na hilo ndilo lilikua linatokea kwa mgonjwa wangu nliyemtaja mwanzo wa hili andiko

kwa hiyo kama tulivyoona hapo juu kwa uchache afya ya akili ni jambo linalohusu kukosekana kwa uhusiano wa kemikali mbali mbali za ubongo ,Hivyo jamii inapaswa itambue kwamba ukiwa na tatizo la akili sio kwamba wewe ni kichaa ni kwamba umeumwa kama unavyoweza kuumwa meno au mguu ndio ukichaa ni ugonjwa wa akili lakini sio kila ugonjwa wa akili ni ukichaa , sisi kama jamii inapaswa tuwe na uelewa wa kuweza kuwsaidia watu mbali mbali wanaopitia matatizo ya afya ya akili wakiwemo vichaa bila kuwabagua.

Mtu anapokufuatwa na kukuelekeza shida yake jaribu kumsikiliza kama vile tulivyoona kwamba maneno yanaeza kuuletea ubongo ajali tafiti zinaonyesha maneno ya kufariji na kutia moyo yanaweza kupelekea mtu akapata ahueni katika mambo yanamkabili . Mtu akikwambia ana msongo wa mawazo tusimuone kama mtu weak mtu anayejiendekeza hii ipo kwetu sana wanaume na ndio wahanga wakubwa wa magonjwa ya akili.

Usikimbilie katika kufanya hitimisho la nini anaumwa msikilize kwa umakini , tafuta sehemu iliyotulia ongea nae sio lazima ukubaliane na anachoongea lakini kwa kuonyesha unajali hisia zake utakua umemsaidia pakubwa sana , muulize maswali machache yanayoweza kumfanya aongee zaidi lakini sio maswali yanayoweza kumfanya ajihukumu zaidi

Tunakutegemea wewe unayesoma hapa kuwa nyenzo ya kutuletea mtu mwenye magonjwa ya akili ili sisi tushughulike nae kitaalamu zaidi , jaribu kumshauri kwamba inapaswa awaone pia wataalamu wa afya hapo ni baada ya kumshauri maneno kadhaa ya kutia moyo na kubwa katika yote angalia na umsome huyo mtu kama ana mawazo ya kujidhuru na u deal na hilo jambo haraka kadri unavyoweza

katika makala zingine zinazofuata tutaongelea nini mtu anapaswa kufanya anapohisi ana tatizo la afya ya akili , hatua za kuchukua na pia tutaongelea nini serikali inapaswa ifanye kutatua matatizo haya leo tumeongelea jamii inapaswa ifanye nini na ielewe nini kuhusu afya ya akili usisahau ku vote kwenye alama ya ^ hapo chini

NIMALIZIE KWA KUSEMA " MAGONJWA YA AKILI YANATIBIKA VUNJA UKIMYA"
Asanteni sana
 
Upvote 98
Okay nimekupata.....

Ingawa pia unaweza kukuta mtu yupo sawa (unique) ila kwa mtizamo wa jamii na kutaka kumbadilisha kama jamii inavyotaka mkajikuta kwamba mnampoteza...

Yaani kuondoa ile confidence yake katika utofauti wake... (mfano mtu anaweza akawa mchangamfu sana kama chizi, yaani a happy go lucky guy) ila jamii kumuona kwamba hafai au inabidi ku-behave in such a different way ukajikuta kwamba unambadilisha chui anakuwa paka....

My point is we are all different tusije tukafanya kosa la kutaka kuwaondoa watu wenye behaviour tofauti na sisi kwa kuwa-label mafyatu (There is nothing worse than questioning yourself, kweli ukifikia hapo utakuwa hauona tofauti na robot inayokuwa programmed kufanya kila watu wanataka) And that's not being a Human...
Kuna vitu kama ADHD, na AUSTISM ambavyo kwa nchi kama Tanzania bado havijaangaliwa kitaalamu
Hivi viwili vinawafanya watu kuwa extremely challenging na vile vile very unique kama moja ya aina ya Autism inayojulikana kama asperger's syndrome huwafanya watu kuwa very smart and intelligent kwenye elimu lakini kuwa anaonekana hayuko sawa ukija kwenye masuala ya jamii
Mleta mada ni Mtaalamu wa haya mambo atatufafanulia zaidi...
 
Kuna vitu kama ADHD, na AUSTISM ambavyo kwa nchi kama Tanzania bado havijaangaliwa kitaalamu
Hivi viwili vinawafanya watu kuwa extremely challenging na vile vile very unique kama moja ya aina ya Autism inayojulikana kama asperger's syndrome huwafanya watu kuwa very smart and intelligent kwenye elimu lakini kuwa anaonekana hayuko sawa ukija kwenye masuala ya jamii
Mleta mada ni Mtaalamu wa haya mambo atatufafanulia zaidi...
Ntakuja kuongea about this
 
" Daktari huwezi kuelewa ntakachokuambia bora nife nacho " yalikua ni maneno ya mgonjwa wangu niliyekua namhudumia kwa muda mrefu , niligundua ana matatizo zaidi yanayopelekea afya yake kudhorota siku baada ya siku

Afya ya akili kwa kimombo (mental health) ni swala ambalo limekua likichukuliwa kwa mzaha katika jamii zetu za kiafrika , ukisikia kuhusu afya ya akili ndugu msomaji akili yako lazima itakupeleka moja kwa moja kuwaza " UKICHAA " .

Afya ya akili sio ukichaa , afya ya akili ni uwezo wa akili mtu kufanya vitu kwa usahihi , kufikiri kwa usahihi , kutenda kwa usahihi , Ni uwezo wa ubongo kuchanganua mambo na kuyafanya kwa usahihi, mtu unaweza usiwe kichaa lakini hutendi kwa usahihi au hufikiri kwa usahihi . Unawaza kufa tu kila saa unawaza dunia yote imekutenga hayo yanaweza kuwa ni mawazo yako lakini sio sahihi

Ubongo wa binadamu umetengenezwa kwa namna ya tofauti sana tatizo lolote linaloweza kutokea kwenye ubongo linaweza kupelekea matatizo mengine mengi kwenye viungo vingine vya mwili unachukua asilimia mbili tu ya uzito wa mwili mzima lakini asilimia ishirini ya nishati nzima ya mwili inapelekwa kwenye ubongo, wanasayansi bado tunajaribu kuchunguza uhusiano wa matatizo ya akili na reaction mbali mbali zinazotokea kwenye ubongo lakini kwa uchache (nitatumia lugha rahisi ili kila mtu hata asiyesoma sayansi afahamu) naweza kusema matatizo mengi ya afya ya akili yanatokana na kukosekana kwa uwiano katika kemikali mbalimbali za saketi kwenye ubongo (neurones) mfano wa kemikali hizo ni serotonini na neuroepinephrine (nimekosa neno lake la kiswahili ).

Hizi nyuroni huwasiliana zenyewe kwa zenyewe na katika kuwasiliana hutumia kemikali nilizozitaja hapo juu na zingine nyingi inapotokea hakuna uwiano wa kemikali ndipo hapo mtu tunasema ubongo wake umepata shida na hafanyi mambo kwa usahihi mfano kunapokua na utengenezwaji mwingi wa kemikali ya dopimine katika saketi za ubongo hapo ndipo tunasema mtu ana ukichaa uliopitiliza( psychosis) , ndo hawa tunawaona wanaokota makopo kwenye mabarabara.

Kwa mtu mwenye msongo mkubwa wa mawazo inamaanisha kemikali za serotonini zinatengenezwa kwa kiwango kichache sana katika nyuroni zake za ubongo , serotonini sisi wataalamu wa afya hupenda kuiita " kemikali ya furaha" sababu ikipungua furaha ya mtu hupungua na hata hamu ya kula hupungua.

Kwa hiyo ubongo ni kama kiungo chochote kila kwenye mwili kwamba na chenyewe kinaweza kuumwa na kinaweza pata ajali hata maneno tu yanaweza kufanya ubongo upate ajali mfano unatukanwa au unadhalilishwa na mtu unayempenda kila siku na shida kubwa inakuja kwamba ubongo ndo unaongoza ogani zingine za mwili hivyo unapopata shida ogani zingine zitadhurika pia na hilo ndilo lilikua linatokea kwa mgonjwa wangu nliyemtaja mwanzo wa hili andiko

kwa hiyo kama tulivyoona hapo juu kwa uchache afya ya akili ni jambo linalohusu kukosekana kwa uhusiano wa kemikali mbali mbali za ubongo ,Hivyo jamii inapaswa itambue kwamba ukiwa na tatizo la akili sio kwamba wewe ni kichaa ni kwamba umeumwa kama unavyoweza kuumwa meno au mguu ndio ukichaa ni ugonjwa wa akili lakini sio kila ugonjwa wa akili ni ukichaa , sisi kama jamii inapaswa tuwe na uelewa wa kuweza kuwsaidia watu mbali mbali wanaopitia matatizo ya afya ya akili wakiwemo vichaa bila kuwabagua.

Mtu anapokufuatwa na kukuelekeza shida yake jaribu kumsikiliza kama vile tulivyoona kwamba maneno yanaeza kuuletea ubongo ajali tafiti zinaonyesha maneno ya kufariji na kutia moyo yanaweza kupelekea mtu akapata ahueni katika mambo yanamkabili . Mtu akikwambia ana msongo wa mawazo tusimuone kama mtu weak mtu anayejiendekeza hii ipo kwetu sana wanaume na ndio wahanga wakubwa wa magonjwa ya akili.

Usikimbilie katika kufanya hitimisho la nini anaumwa msikilize kwa umakini , tafuta sehemu iliyotulia ongea nae sio lazima ukubaliane na anachoongea lakini kwa kuonyesha unajali hisia zake utakua umemsaidia pakubwa sana , muulize maswali machache yanayoweza kumfanya aongee zaidi lakini sio maswali yanayoweza kumfanya ajihukumu zaidi

Tunakutegemea wewe unayesoma hapa kuwa nyenzo ya kutuletea mtu mwenye magonjwa ya akili ili sisi tushughulike nae kitaalamu zaidi , jaribu kumshauri kwamba inapaswa awaone pia wataalamu wa afya hapo ni baada ya kumshauri maneno kadhaa ya kutia moyo na kubwa katika yote angalia na umsome huyo mtu kama ana mawazo ya kujidhuru na u deal na hilo jambo haraka kadri unavyoweza

katika makala zingine zinazofuata tutaongelea nini mtu anapaswa kufanya anapohisi ana tatizo la afya ya akili , hatua za kuchukua na pia tutaongelea nini serikali inapaswa ifanye kutatua matatizo haya leo tumeongelea jamii inapaswa ifanye nini na ielewe nini kuhusu afya ya akili usisahau ku vote kwenye alama ya ^ hapo chini

NIMALIZIE KWA KUSEMA " MAGONJWA YA AKILI YANATIBIKA VUNJA UKIMYA"
Asanteni sana
Hii ni moja ya mada bora sana katika story nilizozisoma kwenye hili jukwaa, unajua jamii yetu kwa asilimia kubwa inaona aibu kuzungumzia hili suala, halafu familia zenye wagonjwa wa akili huwa zinatengwa au kunyanyapaliwa kutokana na imani potofu ambazo tumejengewa na mababu zetu, wengine hata wakitaka kuoa hawaoi kwenye familia zenye wagonjwa wa akili

Inabidi nguvu kubwa itumike kueli.isha jamii kwamba hawa wenzetu wanatibika na wanaweza kurudi kwenye hali zao za kawaida

Hongera sana kwa andiko zuri lenye kutoa elimu na kutia moyo
 
Hii ni moja ya mada bora sana katika story nilizozisoma kwenye hili jukwaa, unajua jamii yetu kwa asilimia kubwa inaona aibu kuzungumzia hili suala, halafu familia zenye wagonjwa wa akili huwa zinatengwa au kunyanyapaliwa kutokana na imani potofu ambazo tumejengewa na mababu zetu, wengine hata wakitaka kuoa hawaoi kwenye familia zenye wagonjwa wa akili

Inabidi nguvu kubwa itumike kueli.isha jamii kwamba hawa wenzetu wanatibika na wanaweza kurudi kwenye hali zao za kawaida

Hongera sana kwa andiko zuri lenye kutoa elimu na kutia moyo
Asante sana jamani 😍😍😍
 
Hii ni moja ya mada bora sana katika story nilizozisoma kwenye hili jukwaa, unajua jamii yetu kwa asilimia kubwa inaona aibu kuzungumzia hili suala, halafu familia zenye wagonjwa wa akili huwa zinatengwa au kunyanyapaliwa kutokana na imani potofu ambazo tumejengewa na mababu zetu, wengine hata wakitaka kuoa hawaoi kwenye familia zenye wagonjwa wa akili

Inabidi nguvu kubwa itumike kueli.isha jamii kwamba hawa wenzetu wanatibika na wanaweza kurudi kwenye hali zao za kawaida

Hongera sana kwa andiko zuri lenye kutoa elimu na kutia moyo
Si ushavote lakini
 
Just Learn to cut out the noise around you. Calm down and see things in perspective. Reset your faith! Everything that is going on in your life will soon make sense. Don’t let Satan mess with your mind and tell you otherwise. Have beautiful patience things will work out for you
 
You think there’s no solution; no way out of your problems. You feel almost certain that it’s a dead end. You forget you have the Lord of the Worlds, the Owner of Miracles. Remember, don’t consider your circumstances, consider what the Almighty can do. Nothing is impossible.
 
Whatever you do, don’t hurt others. When you try to hurt those who hurt you, you’re only hurting yourself. Because it’s not in your character to act in an ugly manner. What you need to do is forgive and move on. Easier said than done for most. But only good can overcome evil.
 
Taking at least 20 minutes out of your day to stroll or sit in a place that makes you feel in contact with nature will significantly lower your stress hormone levels. That's the finding of a study that has established for the first time the most effective dose of an urban nature experience. Healthcare practitioners can use this discovery to prescribe 'nature-pills' in the knowledge that they have a real measurable effect.
 
The hardest thing in life is pulling yourself out of a dark place. You are emotionally, mentally, and physically drained and feel lost no matter what. Anyone in a dark place, dont give up on yourself. Bad times dont last. You are stronger than you think.
 
Back
Top Bottom