EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,325
Asilimia 50 ya wagonjwa wanaotibiwa Muhimbili, kitengo cha Fiziotherapia, wanaumwa magonjwa yasiyoambukiza. Hayo yalielezwa jana na Katibu Mkuu wa Chama cha Madaktari Wazoeza Viungo Tanzania, Dk. Denis Mbezi, wakati akifafanua jambo kwa waandishi wa habari juu ya maandalizi ya Kongamano la Wataalamu wa Fiziotherapia katika nchi za Afrika, litakalofanyika jijini Arusha, Oktoba 14.
Dk. Mbezi alisema magonjwa hayo kwa sasa yameshika kasi na yanapoteza uhai wa watu wengi kutokana na kushindwa kutambua njia za kuzuia magonjwa hayo yasiwatokee. Aliyataja magonjwa hayo kuwa ni pamoja na shinikizo la damu, kisukari, kuwa na mafuta mengi mwilini, kuongezeka uzito na kuna kundi kubwa la wagonjwa wa kiharusi, uchakavu wa viungo na watoto wenye mtindio wa ubongo. Kiharusi kinasababishwa na shinikizo la juu la damu, usukari, chakula chenye mafuta mengi au uvutaji wa sigara.
Alisema watu wengi wameshindwa kupata elimu ya kuzuia magonjwa hayo yanayosababishwa na maisha yasiyozingatia misingi ya afya bora huku akitolea mfano shinikizo la damu linalosababishwa na kutofanya mazoezi. Kutokana na hali hiyo chama hicho kimeandaa kliniki ya wazi itakayotoa huduma bure kama ishara ya kumuenzi Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Oktoba 14 hadi 18 Arusha.
Dk. Mbezi ambaye pia anahusika na kitengo cha Fizioterapia Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), alisema kazi za chama hicho ni pamoja na matibabu hasa kwenye magonjwa yasiyoambukiza, kinga na kutoa elimu jinsi ya kuepuka magonjwa hayo.
Chanzo: Magonjwa yasiyoambukiza yaongezeka
Dk. Mbezi alisema magonjwa hayo kwa sasa yameshika kasi na yanapoteza uhai wa watu wengi kutokana na kushindwa kutambua njia za kuzuia magonjwa hayo yasiwatokee. Aliyataja magonjwa hayo kuwa ni pamoja na shinikizo la damu, kisukari, kuwa na mafuta mengi mwilini, kuongezeka uzito na kuna kundi kubwa la wagonjwa wa kiharusi, uchakavu wa viungo na watoto wenye mtindio wa ubongo. Kiharusi kinasababishwa na shinikizo la juu la damu, usukari, chakula chenye mafuta mengi au uvutaji wa sigara.
Alisema watu wengi wameshindwa kupata elimu ya kuzuia magonjwa hayo yanayosababishwa na maisha yasiyozingatia misingi ya afya bora huku akitolea mfano shinikizo la damu linalosababishwa na kutofanya mazoezi. Kutokana na hali hiyo chama hicho kimeandaa kliniki ya wazi itakayotoa huduma bure kama ishara ya kumuenzi Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Oktoba 14 hadi 18 Arusha.
Dk. Mbezi ambaye pia anahusika na kitengo cha Fizioterapia Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), alisema kazi za chama hicho ni pamoja na matibabu hasa kwenye magonjwa yasiyoambukiza, kinga na kutoa elimu jinsi ya kuepuka magonjwa hayo.
Chanzo: Magonjwa yasiyoambukiza yaongezeka