Magufuli aagiza madaktari waliokimbilia hospitali binafsi kusakwa

Magufuli aagiza madaktari waliokimbilia hospitali binafsi kusakwa

Don YF

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2014
Posts
10,494
Reaction score
9,854
By Aurea Simtowe

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, John Magufuli ameagiza madaktari waliokimbia hospitali ya rufaa ya Kitete kwa madai ya maslahi madogo kufuatiliwa ili kuzilipa fedha za Serikali.

Madaktari hao wamekimbilia hospitali binafsi kwa madai kuwa huko wanalipwa fedha nyingi.

Magufuli ametoa agizo hilo leo Jumamosi Januari 30, 2021 baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la wagonjwa wa dharura katika hospitali ya rufaa Kitete lililogharimu zaidi ya Sh600 milioni.

Mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa Mkoa wa Tabora, Dk Marko Waziri amesema madaktari wanaoondoka katika hospitali hiyo wengi walikuwa wakisema maslahi ni madogo.

Amesema waliondoka na kumueleza kuwa mtu akiwa na shahada ya kwanza akajiendeleza na kupata shahada ya uzamili, tofauti ya mshahara wake na mtu mwenye shahada ya kwanza ni kati ya Sh200,000 hadi Sh300,000.

“Kuna mmoja nasikia ameajiriwa sehemu analipwa Sh5 milioni hivyo nadhani wanatoka huku serikali kwenda hospitali binafsi kutafuta hela,” amesema Dk Waziri

Magufuli amesema kama maslahi ni madogo kwa nini madaktari hao waliomba kuajiriwa serikalini na kuziba nafasi za madaktari wengine.

“Kazi ya udaktari ni kujitolea kama sadaka hata manesi hakuna mtu anayeridhika na mshahara lakini kama alipewa kazi yake akaajiriwa kwa nini asiifanye."

“Mwaka jana niliajiri madaktari 1000, kumbe daktari huyohuyo alipofika hapa akanusa tu akaondoka pamoja na mshahara wetu kwa nini asishtakiwe kwa wizi,” amesema Magufuli

Kwa mujibu wa Dk Waziri hospitali hiyo ina madaktari bingwa watano lakini watatu wameondoka.

“Na walisomeshwa na serikali, kwa gharama ya serikali na hawajarudisha hizo fedha, watafute hao madaktari ili tuje tujue hela zetu zipo wapi.”

“Kwa sababu hakuna mtu anayeridhika na mshahara hata mimi siridhiki nao, hata manesi hawa hawaridhiki lakini wanajituma, tunataka sisi wote matatizo yetu tuyatatue kwa pamoja kwa sababu hatuwezi kuyatatua kwa siku moja halafu mtu akaingia kwa ubinafsi,” amesema Magufuli.

Amesema hiyo ni kwa sababu hatua mbalimbali zinachukuliwa ili kuimarisha huduma za afya na miongoni mwa hatua hizo ni kuajiri watumishi zaidi ya 14,000 katika kipindi cha miaka mitano, kujenga hospitali na vituo vya afya, hospitali za rufaa, mikoa na zahanati

“Tumeanza na hivi baqdaye tunaingia katika maslahi ya watumishi wa afya, tunajua wanafanya kazi kubwa sana ya kujitolea na nawapongeza sana, kinachohitajika ni uzalendo pia.”

“Ukikimbia kinamama hapa wanaumwa wengine wanataka kufanyiwa upasuaji wewe unaenda huko Kamanga (hospitali). Mfuatilie huyo daktari aliyekimbia hapa mfuatilie huyo daktari ikiwezekana tunamfungia daktari tunafungia na hospitali aliyoenda kutibia,” amesema Magufuli

Amesema hilo litawafanya watu kutambua kuwa Wizara ya Afya si ya kuchezea kwa sababu watu wanasomeshwa kwa fedha za watanzania maskini na kupewa mikopo asilimia 100 lakini baada ya kumaliza wanakimbia kwa kudai maslahi madogo.

“Si ungekimbia wakati unasoma, hela yetu umekula halafu unasema maslahi madogo, tunataka maslahi yaboreshwe na hiyo ndiyo nia ya serikali hii lakini unaanza kimoja huwezi kuboresha maslahi wakati hospitali huna, majengo na vifaa,”

Amesema lengo la Serikali ni kuweka majengo ya kutosha na vifaa ili madaktari wafanye kazi katika maeneo mazuri kabla ya kuhamia eneo lingine.

“Lakini nataka niwahakikishie suala la maslahi yenu tunaliangalia kikamilifu kulingana na bajeti itakavyokuwa inakuja, nataka hilo niwahidi lakini kukimbia ni dhambi,” amesema Magufuli.
 
Kuna Ph.D kwa reasoning seriously? Hakuna Uhuru kamwe! Kwani lazima mtu afanye kazi kwa public hospital?[emoji848][emoji848][emoji848][emoji15]
 
Ata kama wanafanya kazi private sector si TRA inaweza kuwakata pesa ya loan kwa mishahara juu kwa juu kama vile PAYE, the way Kenya wanafanya HELB, ata ukiajiriwa na private sector with your KRA Pin they can trace you and demand your employer to deduct some amount to repay the education loan, does Magufuli have a Ph.D for real? Hii reasoning inasikitisha sana!
 
Hehehehe! Jameni hata kitambo tulipokua gizani sidhani kama tulikua kwenye kiwango hiki, au labda itakua hizo hela sio mkopo, labda huwa wanasamehewa mikopo ya vyuoni, na kama husamehewa basi daktari arudi kwanza eneo lake la kazi.
 
Watz mnalo jameni.

Bado naomba mwenye ufahamu wa hizi taarifa kwa kiundani atudadavulie, maana mbona naona kama hatari kwa kweli, hamna kitu cha hovyoo kama kuwa na katiba mbovu kwenye nchi, hapa hata kosa halipo kwa Magufuli, ila katiba. Yaani mkiwa na katiba mbovu lazime mumkome rais, hata mimi niwe rais kwenye nchi yenye katiba mbovu lazima mtakaa. Kha nawakomoa hadi raha.

Haileti mantiki, kama hizo hela ni mkopo basi haipaswi daktari apangiwe wapi pakufanya kazi, maana lazima achakarike namna gani atazirejesha na pia kujiboresha kimaisha, halafu kingine sijakielewa, hivi hiyo hospitali alikokwenda kuajiriwa inafungiwa kwa kosa lipi, jameni hata hili MATAGA team mnasifia?
 
Hili boko unakosa hata ground ya kulitetea. Mkataba wa kazi ni hiari na mtu anaweza acha kazi within 24 hrs. Katika hali ya kawaida ingekuwa kuwa, baada ya kujua sababu za kuacha kazi, angeagiza bodi ya mishahara ili watoe mapendekezo ya kuboresha maslahi ya watumishi wa umma ili wasishawishike kuacha kazi kwani ni wengi tu wameacha. Cha ajabu zaidi ni kuwa, hata Waziri anayeelekezwa afanye ufuatiliaji naye alikuwa daktari akakimbilia kwenye siasa ambapo kuna mikupuo ya hela.
 
Watz mnalo jameni.

Bado naomba mwenye ufahamu wa hizi taarifa kwa kiundani atudadavulie, maana mbona naona kama hatari kwa kweli, hamna kitu cha hovyoo kama kuwa na katiba mbovu kwenye nchi, hapa hata kosa halipo kwa Magufuli, ila katiba. Yaani mkiwa na katiba mbovu lazime mumkome rais, hata mimi niwe rais kwenye nchi yenye katiba mbovu lazima mtakaa...kha nawakomoa hadi raha.

Haileti mantiki, kama hizo hela ni mkopo basi haipaswi daktari apangiwe wapi pakufanya kazi, maana lazima achakarike namna gani atazirejesha na pia kujiboresha kimaisha, halafu kingine sijakielewa, hivi hiyo hospitali alikokwenda kuajiriwa inafungiwa kwa kosa lipi, jameni hata hili MATAGA team mnasifia?
Na wewe ni mmbea sana, wewe hata dog akiingia kwa nyumba utapiga nduru mpaka Somalia wasikie.
 
Na wewe ni mmbea sana, wewe hata dog akiingia kwa nyumba utapiga nduru mpaka Somalia wasikie.

SHILAWADU lazima tunyatie nyatie, ila hapo mnalo na bado hamjakoma tu.

Hizo kauli zitaibua panic sio mchezo, ila kama hizo hela mnalipiwa kama ruzuku na sio mkopo basi komaeni na kutoa huduma kwenye taasisi za serikali hadi mkataba uishe, sema najua mtafanya kazi kwa kusonya sonya sana.
 
Huyu jamaa huwa nguruwe sana,
WaaH.
Huelewi kitu ila unarukia tu mambo kwa Mihemko

Sikubaliani na Hali ya Maslahi ya Watumishi wa umma kwa sasa, ila MDs, MMeds majority wanalipiwa na Wizara ya Afya kwa Makubaliano ya Kupractice chini ya Wizara.

Kuna utaratibu wa Kuacha kazi serikalini ikiwa ni pamoja na Kurejesha mkwanja wa Wizara, sio Kukimbia kama huyo jamaa.

Hata ukiajiriwa private sector kuna utaratibu wa Kuacha kazi, sio kukimbia.
 
kugoma hawagomi, kuandamana kumeshindikana. huku Kenya pia tulishawakataa.

mi5 tena na tena.
Nyie wala hamna tofauti na sisi, Sonko na udogo wake alihenyesha watu miaka kadhaa huku akitumia hela za serikali kuhonga karibia Kenya nzima.
 
Nyie wala hamna tofauti na sisi, Sonko na udogo wake alihenyesha watu miaka kadhaa huku akitumia hela za serikali kuhonga karibia Kenya nzima.
Hatupo level moja bro. Daktari wa Kenya analipwa mara tano zaidi kumliko mwenzake wa Tanzania na bado kila siku wanagoma wakitaka nyongeza na marupurupu.

daktari wa Tanzania anaweza kuwa shamba-boy wa daktari wa Kenya, ukweli ama si kweli?
 
Mbona huwa wanafukuzwa hadharani na kukemewa kinyume ya sheria. Taratibu za kuacha kazi na kuajiriwa zipo. Mtu unampa laki tatu kaenda anapata Mil 5 kweli akatae kusema najitolea. Mtu anaondoka mwingine aje ajaze nafasi mbona wako wengi tu lakini sio kulazimishana. Mtu akiacha kazi ana clear kila kitu mpaka madeni ndio anapewa release letter.
 
Huelewi kitu ila unarukia tu mambo kwa Mihemko

Sikubaliani na Hali ya Maslahi ya Watumishi wa umma kwa sasa, ila MDs, MMeds majority wanalipiwa na Wizara ya Afya kwa Makubaliano ya Kupractice chini ya Wizara.

Kuna utaratibu wa Kuacha kazi serikalini ikiwa ni pamoja na Kurejesha mkwanja wa Wizara, sio Kukimbia kama huyo jamaa.

Hata ukiajiriwa private sector kuna utaratibu wa Kuacha kazi, sio kukimbia.

MATAGA hata hili unatetea, mengine kausha bana. Sasa hospitali alikokwenda kuajiriwa ina makosa gani hadi ifungiwe, mbona mnazidi kuwa hovyoo hata kuizidi Korea ya Kaskazini.
 
Welcome to Magufulistan, this way please, have a seat. [emoji15]
 
hatupo level moja bro. daktari wa Kenya analipwa mara tano zaidi kumliko mwenzake wa Tanzania na bado kila siku wanagoma wakitaka nyongeza na marupurupu.
daktari wa Tanzania anaweza kuwa shamba-boy wa daktari wa Kenya, ukweli ama si kweli?
unaumwa akili wewe.

yaani dactari wa kenya alipwe mara 5 zaidi ya watz alie njaa,kwani pesa yenu ina matatizo gani!!![emoji16][emoji16][emoji16]

mbona unaivua nguo kweupe.
 
MATAGA hata hili unatetea, mengine kausha bana. Sasa hospitali alikokwenda kuajiriwa ina makosa gani hadi ifungiwe, mbona mnazidi kuwa hovyoo hata kuizidi Korea ya Kaskazini.
Case za tz hamziwezi,nyinyi endeleeni kupiga campaign miaka miwili kabla ya uchaguzi.

Tena wewe kanoe panga vyema.
 
Watz mnalo jameni.

Bado naomba mwenye ufahamu wa hizi taarifa kwa kiundani atudadavulie, maana mbona naona kama hatari kwa kweli, hamna kitu cha hovyoo kama kuwa na katiba mbovu kwenye nchi, hapa hata kosa halipo kwa Magufuli, ila katiba. Yaani mkiwa na katiba mbovu lazime mumkome rais, hata mimi niwe rais kwenye nchi yenye katiba mbovu lazima mtakaa. Kha nawakomoa hadi raha.

Haileti mantiki, kama hizo hela ni mkopo basi haipaswi daktari apangiwe wapi pakufanya kazi, maana lazima achakarike namna gani atazirejesha na pia kujiboresha kimaisha, halafu kingine sijakielewa, hivi hiyo hospitali alikokwenda kuajiriwa inafungiwa kwa kosa lipi, jameni hata hili MATAGA team mnasifia?
Kosa lipi la katiba unalikusudia hapa?
 
Back
Top Bottom