Magufuli achana na Raila,sifa zake "chafu" Msaidizi wake wa karibu kazianika hadharani kupitia kitabu

Magufuli achana na Raila,sifa zake "chafu" Msaidizi wake wa karibu kazianika hadharani kupitia kitabu

iparamasa

JF-Expert Member
Joined
Nov 14, 2013
Posts
13,437
Reaction score
14,927
Raila ameanikwa mambo yake na aliyekuwa Msaidizi wake Mkuu,mshauri wake wa mambo ya kisiasa,kisheria na katiba kipindi cha serikali ya umoja wa kitaifa nchini kenya,MIGUNA MIGUNA,kama mnakumbuka,Raila alikuwa waziri Mkuu,wakati Mwai Kibaki ni Rais baada ya zile vurugu na mauaji baada ya Uchaguzi

MIGUNA MIGUNA alitunga kitabu kiitwacho "PEELING BACK THE MASK" humo kamuanika Raila Odinga mambo yake yote ya binafsi(vidosho)mpaka ya Ofisini kwake,Ofisi ya Waziri Mkuu wa Kenya,hakika kamuacha uchi na pengine ndio sababu urais atabaki kuuota ndotoni

Bwana MIGUNA ndiye alikuwa mtu wa karibu sana na Raila Odinga,anajua mambo yake,hivyo mtanzania mwenzetu yeyote anayemsogeza Raila kwa ukaribu wa kupitiliza lazima tumuangalie kwa jicho kali

UKURASA wa 512,MIGUNA MIGUNA anaandika kwamba Ofisi ya waziri mkuu Raila ilikuwa kama pango la wanyanganyi,watu wenye briefcase za mapesa,bahasha za khaki,wauza unga,watakatisha pesa,wezi waliingia bila tabu,anasema familia ya Raila ilitajirika ghafla baada ya yeye kuwa waziri mkuu na anasema familia ya Raila ilikuwa inasaka mabilioni kama watu waliopandwa na kichaa

JPM kwa kauli zake huwa anasema hapendi wapiga dili,sasa urafiki wake na Raila kwa nini asiuvunje?

UKURASA WA 511

Anasema Raila ana udhaifu wa ajabu kwa wanawake wa kila aina bila kujali kwamba ameoa,mkewe anaitwa Idda Odinga,lakini misafara ya wanawake ilikuwa inamtembelea na wakati mwingine kumletea chakula,anatoa mfano wa wanawake kama Rachel Shebesh,Ann kairuki,na easthet Passaris,na anasema kulikuwa na mgogoro mkubwa kati ya mke wa Raila na Bi Rachel Shebesh,ambaye Raila alifanya juu chini mpaka akampa ubunge wa kuteuliwa akiwa acha wanawake wengi walioipigania ODM

Mwandishi anasema kuna kipindi walimwalika Raila Canada,baadae wakamfanyia dhifa nyumbani,Mara akatokea binti mwenye kama asili ya kinyarwanda,mgeni ambaye hakualikwa,ila baadae raila akawaambia ni kidosho wake,na walipoenda kumsabahi asubuhi hoteliniI,wakapishana na kidosho huyo akitoka chumbani kwa raila(manyoya)

Anaendelea kusema Raila ni mdhaifu kwenye Pombe,ngono na pesa,kama alikuwa hanywi pombe basi yuko na wanawake anafanya ngono,yeyote mwenye pesa halali au haramu kwa Raila alikaribishwa

Je Mambo haya yanafaa? Nakushauri umpige chini

Pia mwandishi MIGUNA MIGUNA katika UKURASA wa 175,mbali na kutaja ofisi ya waziri mkuu Raila kuwa ni shimo la rushwa,anasema Raila alijaza ndugu zake serikalini

Anasema Raila alimteua kaka yake Oburu Oginga kuwa naibu waziri wa fedha,mpwa wake Jakayo Midiwo kuwa mnadhimu wa ODM, Dada yake Akinyi Wenwa kuwa balozi Los Angeles,dada yake Beryl Qchieng kuwa mkuu wa mfuko wa pensheni wa watumishi wa Reli,mpwa wake Carey Orege kuwa katibu mkuu wizara ya maendeleo ya mikoa,mpwa wake Paul Gondi kuwa Mkurugenzi wa Geothermal Development Company,mpwa wake Ochilo Ayacko kuwa mkurugenzi wa Kenya Nuclear Electricity Project,mpwa wake Joe Aged alimpa nafasi kubwa katika kampuni ya Kenya Power Lighting,mpwa wa mkewe Agnes Odhiambo kuwa mdhibiti wa bajeti,pia aliteua nduguye Alex Kazongo kuwa mkuu wa shirika la pensheni,na mwingine Edward Ouko kuwa mkaguzi wa mahesabu

Nduguye James Ogundo alimpa ujumbe wa Bodi ya mfuko wa maendeleo ya jumbo nafasi iliyokuwa na malipo manono

Pesa za kampeni za Raila Odinga zilikuwa zinashikwa na dada yake Akinyi Walkoa au binti yake Rosemary Akeyo au George Opondo

Hivyo Raila ni mkabila wa kutupwa,nakushauri mheshimiwa Rais uachane naye,atakushawishi na wewe uwe mkabila na uwe mtu wa kuendekeza undugu wa kupitiliza

Pia Msaidizi mwingine wa Raila aitwaye Carol Omondi inadaiwa alitajirika ghafla na kuwa bilionea mkubwa,na ni huyu alitumwa kwenda ikulu ya Uganda kwa museveni wakajadili suala la bomba la mafuta,MIGUNA anasema Msaidizi huyo aliporudi kutoka uganda alikuja na sura ya "mpiga dili" halisi anayeashiria kuwa dili limekubali,

Je kwa nini museveni alibadili msimamo wa kulijenga bomba kupitia Mombasa na akaamua kupitia Tanga? Kuna siri gani? Raila alikwepa nini kenya? Ana mkono kiasi gani na ushawishi kiasi gani kwenye bomba hili?mkataba wa bomba na ujenzi kwa nini ni siri? Je kwa nini ujenzi wa bomba la mafuta ulizinduliwa wakati wakenya wakielekea kwenye uchaguzi? Hasa kupiga kura?ilikuwa kwa amelekezo ya Raila uzinduzi ufanyike ili Uhuru Kenyatta apungukiwe kura kwa kuwa alishindwa kulibakiza bomba kenya? Kumbuka raila ni rafiki wa JPM na pia akiwa waziri mkuu alituma watu wake mara kadhaa ikulu ya uganda,je JPM na museveni walikuwa na ajenda iliyojificha kipindi cha uzinduzi?

Mbona kagame na museveni walichekelea sana JPM alipokuwa rais na ghafla wakavunja urafiki na kenya(coalition of the willing?)

Mwandishi huyo MIGUNA MIGUNA anasema mkono wa raila kwenye dili umefika mpaka kwenye migodi ya shaba Zambia na machimbo ya Dhahabu DRC,
Raila ni nani na anataka nini au ana maslahi gani anataka kuyalinda Tanzania? Hajui kuwa mkuu wetu hapendi dili?

Hivi urafiki wa JPM na Raila chanzo ni nini? Kama ni kupinga ufisadi,mbona Msaidizi wa raila anadai raila ni fisadi wa kutupwa?

Pia mwandishi anasema chuo kikuu cha Minnesota kilimwalika Raila nchini marekani,kikaonyesha nia ya kusaidia chuo kikuu cha maseno nchini kenya,raila akaulizwa na wahusika awape contact person,raila akamtaja mkewe Idda Odinga! Dili,hela isitoke nje ya familia

Kitabu kina story nyingi nzito kuhusu raila,Mimi nimezitoa kwa ufupi,lakini mwisho raila alimtimua kazi msaidizi wake kwa kuwa walishindwa kuelewana katika mambo ya kupinga rushwa,ukabila na ufisadi

Nenda Google ukidownload upate habari kamili

Je nini sababu ya JPM kumfanya huyu jamaa rafiki? Kwenye kampeni tulimchangia? Tsh ngapi?
 
😀Siku Ya Kufa Nyani Miti Yote Huteleza 😛
 
Si mjuzi sana wa Kujenga ama Kubomoa Urafiki na Mahusiano ya watu hata kama kuna masilahi...

Nawaachia wajuzi wa mambo hii...[emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Raila si kiongozi mzuri kwani mwaka 1982 alihusika na mapinduzi yaliyofanyika Kenya kwa muda na zaidi ya wakenya 2000 waliuawa. Raila yupo tayari kuona kenya ikisarambatika na watu kufa ili apate madaraka.
 
Raila ameanikwa mambo yake na aliyekuwa Msaidizi wake Mkuu,mshauri wake wa mambo ya kisiasa,kisheria na katiba kipindi cha serikali ya umoja wa kitaifa nchini kenya,MIGUNA MIGUNA,kama mnakumbuka,Raila alikuwa waziri Mkuu,wakati Mwai Kibaki ni Rais baada ya zile vurugu na mauaji baada ya Uchaguzi

MIGUNA MIGUNA alitunga kitabu kiitwacho "PEELING BACK THE MASK" humo kamuanika Raila Odinga mambo yake yote ya binafsi(vidosho)mpaka ya Ofisini kwake,Ofisi ya Waziri Mkuu wa Kenya,hakika kamuacha uchi na pengine ndio sababu urais atabaki kuuota ndotoni

Bwana MIGUNA ndiye alikuwa mtu wa karibu sana na Raila Odinga,anajua mambo yake,hivyo mtanzania mwenzetu yeyote anayemsogeza Raila kwa ukaribu wa kupitiliza lazima tumuangalie kwa jicho kali

UKURASA wa 512,MIGUNA MIGUNA anaandika kwamba Ofisi ya waziri mkuu Raila ilikuwa kama pango la wanyanganyi,watu wenye briefcase za mapesa,bahasha za khaki,wauza unga,watakatisha pesa,wezi waliingia bila tabu,anasema familia ya Raila ilitajirika ghafla baada ya yeye kuwa waziri mkuu na anasema familia ya Raila ilikuwa inasaka mabilioni kama watu waliopandwa na kichwa

JPM kwa kauli zake huwa anasema hapendi wapiga dili,sasa urafiki wake na Raila kwa nini asiuvunje?

UKURASA WA 511

Anasema Raila ana udhaifu wa ajabu kwa wanawake wa kila aina bila kujali kwamba ameoa,mkewe anaitwa Idda Odinga,lakini misafara ya wanawake ilikuwa inamtembelea na wakati mwingine kumletea chakula,anatoa mfano wa wanawake kama Rachel Shebesh,Ann kairuki,na easthet Passaris,na anasema kulikuwa na mgogoro mkubwa kati ya mke wa Raila na Bi Rachel Shebesh,ambaye Raila alifanya juu chini mpaka akampa ubunge wa kuteuliwa akiwa acha wanawake wengi walioipigania ODM

Mwandishi anasema kuna kipindi walimwalika Raila Canada,baadae wakamfanyia dhifa nyumbani,Mara akatokea binti mwenye kama asili ya kinyarwanda,mgeni ambaye hakualikwa,ila baadae raila akawaambia ni kidosho wake,na walipoenda kumsabahi asubuhi hoteliniI,wakapishana na kidosho huyo akitoka chumbani kwa raila(manyoya)

Anaendelea kusema Raila ni mdhaifu kwenye Pombe,ngono na pesa,kama alikuwa hanywi pombe basi yuko na wanawake anafanya ngono,yeyote mwenye pesa halali au haramu kwa Raila alikaribishwa

Je Mambo haya yanafaa? Nakushauri umpige chini

Pia mwandishi MIGUNA MIGUNA katika UKURASA wa 175,mbali na kutaja ofisi ya waziri mkuu Raila kuwa ni shimo la rushwa,anasema Raila alijaza ndugu zake serikalini

Anasema Raila alimteua kaka yake Oburu Oginga kuwa naibu waziri wa fedha,mpwa wake Jakayo Midiwo kuwa mnadhimu wa ODM, Dada yake Akinyi Wenwa kuwa balozi Los Angeles,dada yake Beryl Qchieng kuwa mkuu wa mfuko wa pensheni wa watumishi wa Reli,mpwa wake Carey Orege kuwa katibu mkuu wizara ya maendeleo ya mikoa,mpwa wake Paul Gondi kuwa Mkurugenzi wa Geothermal Development Company,mpwa wake Ochilo Ayacko kuwa mkurugenzi wa Kenya Nuclear Electricity Project,mpwa wake Joe Aged alimpa nafasi kubwa katika kampuni ya Kenya Power Lighting,mpwa wa mkewe Agnes Odhiambo kuwa mdhibiti wa bajeti,pia aliteua nduguye Alex Kazongo kuwa mkuu wa shirika la pensheni,na mwingine Edward Ouko kuwa mkaguzi wa mahesabu

Nduguye James Ogundo alimpa ujumbe wa Bodi ya mfuko wa maendeleo ya jumbo nafasi iliyokuwa na malipo manono

Pesa za kampeni za Raila Odinga zilikuwa zinashikwa na dada yake Akinyi Walkoa au binti yake Rosemary Akeyo au George Opondo

Hivyo Raila ni mkabila wa kutupwa,nakushauri mheshimiwa Rais uachane naye,atakushawishi na wewe uwe mkabila na uwe mtu wa kuendekeza undugu wa kupitiliza

Pia Msaidizi mwingine wa Raila aitwaye Carol Omondi inadaiwa alitajirika ghafla na kuwa bilionea mkubwa,na ni huyu alitumwa kwenda ikulu ya Uganda kwa museveni wakajadili suala la bomba la mafuta,MIGUNA anasema Msaidizi huyo aliporudi kutoka uganda alikuja na sura ya "mpiga dili" halisi anayeashiria kuwa dili limekubali,

Je kwa nini museveni alibadili msimamo wa kulijenga bomba kupitia Mombasa na akaamua kupitia Tanga? Kuna siri gani? Raila alikwepa nini kenya? Ana mkono kiasi gani na ushawishi kiasi gani kwenye bomba hili?mkataba wa bomba na ujenzi kwa nini ni siri?

Mbona kagame na museveni walichekelea sana JPM alipokuwa rais na ghafla wakavunja urafiki na kenya(coalition of the willing?)

Mwandishi huyo MIGUNA MIGUNA anasema mkono wa raila kwenye dili umefika mpaka kwenye migodi ya shaba Zambia na machimbo ya Dhahabu DRC,
Raila ni nani na anataka nini au ana maslahi gani anataka kuyalinda Tanzania? Hajui kuwa mkuu wetu hapendi dili?

Hivi urafiki wa JPM na Raila chanzo ni nini? Kama ni kupinga ufisadi,mbona Msaidizi wa raila anadai raila ni fisadi wa kutupwa?

Pia mwandishi anasema chuo kikuu cha Minnesota kilimwalika Raila nchini marekani,kikaonyesha nia ya kusaidia chuo kikuu cha maseno nchini kenya,raila akaulizwa na wahusika awape contact person,raila akamtaja mkewe Idda Odinga! Dili,hela isitoke nje ya familia

Kitabu kina story nyingi nzito kuhusu raila,Mimi nimezitoa kwa ufupi,lakini mwisho raila alimtimua kazi msaidizi wake kwa kuwa walishindwa kuelewana katika mambo ya kupinga rushwa,ukabila na ufisadi

Nenda Google ukidownload upate habari kamili

Je nini sababu ya JPM kumfanya huyu jamaa rafiki? Kwenye kampeni tulimchangia? Tsh ngapi?

Mpaka muda huu yaani muda huu bado unaamini baba Jescah sio mpiga dili!?...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unataka umchagulie marafiki.?
Mnavuka mipaka sasa.?

Ipo siku mtasema abadili mke wa sasa hamfai..

Msafwa
Mpoloto, Mbeya
 
Sasa kama JPM hapeni wauza dawa huoni kuna haja ya Raila kuwa na urafiki na JPM ili amfundishe mazara ya unga?
Kuhusu vidosho hilo jambo halina mwenyewe, Rais wa Marekani Trump amerushwa vedio akiwa na makahaba lakini wamarekani walimchagua. Kwanza unataiwa ujuwe umuhimu wa kufanya ngono.
 
Yeye huyu sifa zake ni safi ?Mange apige bigula ndo muelewe sifa za huyu mtu ? Hakika safari inachelewa kwa mengi !kuna kituko duniani kilichozidi hiki ? Raila ni msafi kuliko tuonavyo akifananishwa na aliyeitwa masihi ! Mungu umenijibu yote niliyo omba juu ya ccm na wakwao.naomba sasa weka wazi sifa na misifa ya huyu aliye kukufuru na kukubali kuwa masihi wa ardhi ya nchi yetu,ili kuitia laana nchi.kwanini asiwakatalie watu wake kwamba yeye hafai hata kufanana na kiatu cha Masihi ? Nakuamini na kukutukuza Bwana wangu, tenda tena katika hili ili wafuasi wake na wote wafananao hivyo washuhudie Ukuu wako na wakuogope na kukoma kukutania maisha yao yote !,Amen

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1644d58a53a7e23b2924416983136548.jpg

Hamjawa huru kuongelea urafiki wetu
"to zat exktenti"

"PAMBANA NA HALI YAKO"
 
Back
Top Bottom