ubongokid
JF-Expert Member
- Apr 30, 2017
- 2,154
- 4,184
Malenga naanza hima,ukweli kuambiana
Kweli i wazi daima,yapasa kukumbushana
Walo watemi wajanja,kweli wajaribu ficha
Hili mujarabu Dongo,kwako wangu Magufuli
Wengi walishapotea, katika hali ni tata
Tamko hukulitoa ,ya kwamba wao nguchiro
Vitisho kutamalika,watu kutiana hofy
Hili mujarabu dongo,Kwako wangu magufuli
Raia wako kulinda ,ni lako jukumu kuu
Sijifanye hauoni,ya kwamba hofu yatanda
Malenga tunajoficha,Uhuru tushapoteza
Hili mujarabu dongo,kwako wangu Magufuli
Mambosasa telekeza,hio ndio yako nia
Kutafutia sababu, Ya siro Kumtumbua
Wajua kweli i wazi,Wananchi watambu
Hili mujarabu dongo,Kwako wangu Magufuli
Hebu fikiri kwa kina,Mo ye anataka nini
Kosale kuwa tajiri,Uchumi kusimamia
Kama manji mgeuka,Mwamwona adui enu
Hili mujarabu dongo,Kwako wangu Magufuli
Kwa taadhima nasema,wewe ndiye jemadari
Wajibu wo kutulinda,na kutetea salama
kujifanya huusiki,kwa yako mambo makosa
Hili mujarabu dongo, kwako wangu Magufuli
Tambua tunatambua,zako hila twaziona
Wajifanya kuwananga,wawachezesha kamari
Wawagueza kafara,Madaraka kuyalinda
Hili Mujarabu dongo.Kwako wangu Magufuli
Kwa kina utafakari,Taifa ulitakalo
Maanani atazama,zako hila aziona
Atachukua hatua,adabu kukushikisha
Hili mujarabu dongo,kwako wangu Magufuli
Tamati nahitimisha,kweli nimeichokoza
Najua utakereka ,kwa lango dongo la kweli
Hilazo tunazijua,utwatuma vijana
Mamluki kutumia kutenda zako hisa
Mwishoni najisemea,uzalendo jambo gani
Fikiri yalo moyoni ,na hofu zao raia
Yakupasa tafakari,yale yawapendezayo
Hili mujaraby dongo,kwako wangu Magufuli
Kweli i wazi daima,yapasa kukumbushana
Walo watemi wajanja,kweli wajaribu ficha
Hili mujarabu Dongo,kwako wangu Magufuli
Wengi walishapotea, katika hali ni tata
Tamko hukulitoa ,ya kwamba wao nguchiro
Vitisho kutamalika,watu kutiana hofy
Hili mujarabu dongo,Kwako wangu magufuli
Raia wako kulinda ,ni lako jukumu kuu
Sijifanye hauoni,ya kwamba hofu yatanda
Malenga tunajoficha,Uhuru tushapoteza
Hili mujarabu dongo,kwako wangu Magufuli
Mambosasa telekeza,hio ndio yako nia
Kutafutia sababu, Ya siro Kumtumbua
Wajua kweli i wazi,Wananchi watambu
Hili mujarabu dongo,Kwako wangu Magufuli
Hebu fikiri kwa kina,Mo ye anataka nini
Kosale kuwa tajiri,Uchumi kusimamia
Kama manji mgeuka,Mwamwona adui enu
Hili mujarabu dongo,Kwako wangu Magufuli
Kwa taadhima nasema,wewe ndiye jemadari
Wajibu wo kutulinda,na kutetea salama
kujifanya huusiki,kwa yako mambo makosa
Hili mujarabu dongo, kwako wangu Magufuli
Tambua tunatambua,zako hila twaziona
Wajifanya kuwananga,wawachezesha kamari
Wawagueza kafara,Madaraka kuyalinda
Hili Mujarabu dongo.Kwako wangu Magufuli
Kwa kina utafakari,Taifa ulitakalo
Maanani atazama,zako hila aziona
Atachukua hatua,adabu kukushikisha
Hili mujarabu dongo,kwako wangu Magufuli
Tamati nahitimisha,kweli nimeichokoza
Najua utakereka ,kwa lango dongo la kweli
Hilazo tunazijua,utwatuma vijana
Mamluki kutumia kutenda zako hisa
Mwishoni najisemea,uzalendo jambo gani
Fikiri yalo moyoni ,na hofu zao raia
Yakupasa tafakari,yale yawapendezayo
Hili mujaraby dongo,kwako wangu Magufuli