Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hiyo siyo nguvu ya umma ila ni uhuni.
Uhuni mtu yeyote akiamua anaweza kuufaya, lakini matokeo yake ni kuvujika kwa amani.
Kama wao wameshaamua kuwa wanamtaka Lowassa nini kinawapeleka kwenye mkutano wa Magufuli?
Inaonekana kabisa kuwa kuna kundi lililojiandaa kufanya fujo na walishaandaa camera wapige hii picha ya video.
Ukawa badala ya kuchekelea vitu kama hivi inabidi mvikemee kwa sabau watanzania hawapendi vurugu, hawatamchagua mtu anayeandaa vikundi vya vurugu.
Bila ya kusukumwa na ushabiki wa vyama, kwa mtazamo wangu hivyo si vitendo vya kushabikia. Sioni tafauti na yale yaliyodaiwa kufanywa na Masaburi. Hata kama Mbeya ni ngome ya chama fulani, wafuasi wake hawapaswi kuanzisha vurugu kwa wagombea wa vyama vyengine. Je ikiwa hao waliofanyiwa fujo leo, siku wakija kulipiza kisasi watakapokuwa katika ngome yao, huko si ndio kuhatarisha amani?
Ninamshauri kila mwenye hekima alikemee hili na walio na uwezo wa kulizuwia wafanye hivyo. Pia ninawashashauri wapenda demokrasia wote wasubiri tarehe 25 Oktoba kuonesha hasira na mapenzi yao katika kisanduku cha kura, tujuwe mbovu na mbivu. Tanzania ni yetu sote. Uchaguzi utapita, Tanzania itabaki, na ningependa kuona imebakia Tanzania yenye amani kabla na baada ya uchaguzi.
Nategemea na nasubiri matusi na kejeli za baadhi ya watu, kama yanayoendelea kumkuta Raisi Karume kutoka kwa wanaCCM wenzake kwa kuwaambia waache lugha za matusi.we
Hiyo ilikua maeneo ya Soweto siku nyingi wakati akifanya Ziara mkoani mbeya, kwa leo Magufuli alikua sehemu za Iringa, Njombe kwa maana ya Makambako na Mbarali
Umepotea, hata uandishi wako inaonekana wewe na viroba mnafanana.
Hamumtaki leo wakati mlijazana kwa maelfu kumshangilia wakati alipokuja kufanya kampeni.
Nani alimwambia asimame pale?ukawa walijuaje atasimama pale na kuandaa kikundi?!??Kuhusu clip ya kuzomewa, ni kwamba hawa jamaa zetu wa UKAWA wana siasa za majitaka. Waliandaa kikundi maalum na mpiga picha za mnato na video kwa ajili ya kumzomea Dr. Magufuli. Hata wananchi waliokuwepo walikishangaa kikundi hicho.
jUKWAA LIMEINGILIWA NA LBA BUKU 7-MASAKI..hiyo ni kazi ya kitoto maana watu hawa wameandaliwa kuzomea hivyo kwetu wala sio tatzo tunajua muda utafika na ndipo mtakapokuja kujua kuwa magufuli ndio rais wetu
kiingereza cha kimagifuli hovyooo...rudi shule..!siku hizi mikutano inafanyikia barabarani au ndiyo walewale lower thinkers....................???????????????????????
Politiziano(politicians), ukisoma ulaya unakumbana na lugha za asili ya kilatini nazo ni kifaransa,Spanish, na kireno,pia kiitaliano. Sasa herufi Z inatamkwa (tz), kumbe ujue mazingira gani ametoka na unaona kabisa ndio bado kuchanganya lugha. Kwa msomi wala hana shida kwani anajua kukosea lugha sio shida kwani lugha nyingi zinakuchanganya katika kuzungumza. Kumbe unapohukumu ujue mazingira ya msomi ndio uhukumu. Se vuoi di imparare diversi lingua è così la vita di cambiamento. Take care.