Magufuli alikuwa sahihi kutokuongeza mishahara ya watumishi kwa miaka 5. Uzembe umejaa makazini

Magufuli alikuwa sahihi kutokuongeza mishahara ya watumishi kwa miaka 5. Uzembe umejaa makazini

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari wakuu!

Mwaka jana katika harakati za kufuatilia mirathi ya mke wangu ambaye alifiwa na baba yake ikanilazimu nizitafute ofisi za PSSSF mkoa wa Temeke au Ilala maana mimi ni mkazi wa Dar es salaam.

Nikaingia website ya PSSSF nipate location za ofisi zao. Nikachukua details muhimu na namba za simu, nafika mahali ambapo wameandika kuwa ndipo ofisi za mkoa wa Temeke naambiwa kuwa walihama kitambo.

Napiga simu niwaulize walipo anapokea mwananchi anasema namba haimilikiwi na ofisi bali yeye. Nilipomuhoji anasema kuwa wengi tu humpigia kwa bahati mbaya wakikusudia kuwapigia PSSSF.

Leo tena naingia tovuti ya wizara ya fedha Salary Portal kuna mzee hapa kazini kasahau password na e-mail aliyofungulia haitumii sasa. Ikalazimika nichukue namba ya msaada, napiga anapokea mwananchi ambaye anasema haifahamu salary portal ja hajawahi kuwa mtumishi wa wizara ya fedha.

Sasa kama tu kufanya changes muhimu kwenye website muhimu hawataki au wanapuuzia kuna haja kweli ya kuwaongezea mshahara hawa watumishi?

Mimi ni mtumishi wa umma pia na ni muhanga wa kutopandishwa daraja na mshahara ila kwa hakika huku makazini kuna uzembe sana hasa mtu akishapata kibarua cha permanent.
 
Vitu hivi viwili ni vyema vikaenda sambamba. Wapo watumishi makini ila pia wapo wazembe na wapiga dili.
Mkuu, kutowajibika ni uzembe. Na wasio wajibika inapaswa wachukukiwe hatua accordingly.

Hivyo basi, wasio wajibika wasisaidiwe kubeba wajibu wao kwa kuwaponza wawajibikaji
 
Kama yeye ameona hawajawajibika amewawajibisha,je vipi nao wakiamua kumuwajibisha kwakua hajawajibika kwao? Unashauri nini mleta mada
 
Wewe jamaa hufai kuwa hakimu,hivi kweli kosa la watu Fulani idara moja ndio una generalize wote?.Maisha hayapo hivyo,hata Mungu angehukumu km wewe basi watu tungekuwa tulishapotea zamani sana.
Hapo tayari kataja idara 2 tofauti, Tena yawezekana zinatoka wizara tofauti.
Ni ukweli, kwenye ofisi za umma Kuna uzembe hasa.
 
Kuna mambo ukiyaangali unajisemea kimoyo moyo " acha tu Magufuli aendelee"
Kuna shithole zimekaa kwenye ofisi za umma hasa NIDA, police na uhamiaji vitambi vimejaa kinyesi, tija Ni zero halafu wanalalamika wasipopandishiwa mishahara
 
Back
Top Bottom